Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 18
  • Yakobo Anakwenda Harani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yakobo Anakwenda Harani
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yakobo Alithamini Mambo ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Yakobo Ana Jamaa Kubwa
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yehova Hubariki Jitihada Yenye Bidii Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 18
Yakobo anazungumza na wanaume wa Harani kuhusu Labani na binti yake Raheli

HADITHI YA 18

Yakobo Anakwenda Harani

UNAWAJUA wanaume hawa ambao Yakobo anazungumza nao? Akiisha kusafiri siku nyingi, Yakobo alikutana nao penye kisima. Walikuwa wakichunga kondoo zao. Yakobo akauliza: ‘Mnatoka wapi?’

‘Harani,’ wakasema.

‘Mnamjua Labani?’ Yakobo akauliza.

‘Ndiyo,’ wakajibu. ‘Tazama anakuja Raheli binti yake akiwa na kondoo zake.’ Unamwona Raheli (Rakeli) yule anakuja kutoka mbali?

Raheli akichunga kondoo za baba yake

Yakobo alipomwona Raheli akiwa na kondoo za mjomba wake, alikwenda kuondoa jiwe katika kisima ili kondoo wanywe maji. Kisha Yakobo akambusu Raheli na kujijulisha kwake. Raheli alifurahi sana, akaenda nyumbani kumwambia Labani baba yake.

Labani alifurahi sana Yakobo akae naye. Yakobo alipoomba kumwoa Raheli, Labani alifurahi. Lakini, alimwomba Yakobo afanye kazi katika shamba lake miaka 7 ili apewe Raheli. Yakobo alifanya hivyo kwa sababu alimpenda sana Raheli. Lakini ulipofika wakati wa arusi, unajua ilivyokuwa?

Labani alimpa Yakobo Lea binti yake mkubwa badala ya Raheli. Yakobo alipokubali kumfanyia Labani kazi muda wa miaka mingine saba, Labani alimpa Raheli pia awe mke wake. Siku hizo Mungu aliruhusu wanaume wawe na wake wengi. Lakini sasa, kama Biblia inavyoonyesha, imempasa mwanamume awe na mke mmoja tu.

Mwanzo 29:1-30.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki