Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 20
  • Dina Anaingia Katika Taabu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dina Anaingia Katika Taabu
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Epuka Marafiki Wabaya!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Ukimbieni Uasherati”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Yakobo Ana Jamaa Kubwa
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Pata Usalama Kati ya Watu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 20
Dina na Shekemu

HADITHI YA 20

Dina Anaingia Katika Taabu

UNAONA Dina anaenda kutembela nani? Ni wasichana wanaokaa Kanaani. Je! Yakobo baba yake atafurahia? Ili uweze kujibu ulizo hilo, jaribu kukumbuka Ibrahimu na Isaka walivyofikiria wanawake wa Kanaani.

Wanawake watatu wa Kanaani

Je! Ibrahimu alitaka Isaka aoe msichana wa Kanaani? Sivyo. Je! Isaka na Rebeka walitaka Yakobo aoe msichana wa Kanaani? Sivyo. Unajua sababu yake?

Ni kwa sababu watu hao wa Kanaani waliabudu miungu ya uongo. Hawakufaa kuwa waume wa wake, nao hawakufaa kuwa rafiki wa kushirikiana nao. Basi tunaweza kuwa na hakika kwamba Yakobo hangependezwa na urafiki wa binti yake pamoja na wasichana hao Wakaanani.

Bila shaka, Dina aliingia katika taabu. Je! unamwona mwanamume huyo Mkanaani katika picha anayemtazama Dina? Ni Shekemu. Siku moja Dina alipokuwa akitembelea, Shekemu alimchukua na kumlazimisha alale naye. Hilo lilikuwa kosa, kwa sababu ni wanaume na wanawake waaliooana tu ndio wanaotakiwa kulala pamoja. Ubaya huo ambao Shekemu alimtemtendea Dina uliongoza kwenye taabu nyingi zaidi.

Ndugu zake Dina waliposikia yaliyotokea, walikasirika sana. Simeoni na Levi, walikasirikika sana hata wakachukua panga wakaingia mjini na kuwafikia wanaume hao ghafula. Wao na ndugu zao wakamwua Shekemu na wanaume wengine wote. Yakobo alikasirika kwa sababu wanawe walifanya ubaya huo.

Taabu yote hiyo ilianza namna gani? Ni kwa sababu Dina alifanya urafiki na watu ambao hawakutii sheria za Mungu. Hatutaki tufanye urafiki na watu kama hao, sivyo?

Mwanzo 34:1-31.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki