Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 64
  • Sulemani Anajenga Hekalu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sulemani Anajenga Hekalu
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Hekalu kwa Ajili ya Yehova
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Sulemani Atawala kwa Hekima
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Je, Yeye Ni Mfano Mzuri au Ni Onyo Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Hekalu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 64
Akiwa katika hekalu jipya, Sulemani anasali kwa Yehova Mungu

HADITHI YA 64

Sulemani Anajenga Hekalu

KABLA Daudi hajafa, alimpa Sulemani ramani ya Mungu ya kujenga hekalu la Yehova. Katika mwaka wa nne wa kutawala kwake, Sulemani anaanza kujenga hekalu, linamalizwa baada ya miaka saba na nusu. Makumi ya maelfu ya wanaume wanajenga hekalu hilo. Na pesa nyingi sana zinatumiwa kulijenga kwa sababu dhahabu na fedha nyingi zinatumiwa ndani.

Anaagiza sanduku la agano liwekwe katika chumba cha ndani cha hekalu, na vitu vingine vilivyowekwa katika hema vinawekwa katika chumba kingine.

Hekalu hilo linapomalizika, kunakuwa na sherehe kubwa. Sulemani anapiga magoti mbele ya hekalu na kusali, kama unavyomwona katika picha. ‘Hata mbingu yote haikutoshi wewe,’ Sulemani anamwambia Yehova, ‘namna gani hekalu dogo hili. Lakini, Ee Mungu, tafadhali wasikilize watu wako wanaposali kuelekea mahali hapa.’

Sulemani anapomaliza sala yake, moto unashuka kutoka mbinguni. Unazichoma dhabihu za wanyama zilizotolewa. Na nuru yenye kung’aa kutoka kwa Yehova inajaa hekalu. Hiyo inaonyesha kwamba Yehova anasikiliza, na kwamba anapendezwa na hekalu na sala ya Sulemani. Badala ya kwenda kuabudu katika hema, watu wanakwenda katika hekalu.

Mfalme Sulemani aliyezeeka pamoja na mmoja wa wake zake, akiabudu sanamu

Sulemani anatawala kwa hekima muda mrefu, na watu wanafurahi. Lakini Sulemani anaoa wanawake wengi wa nchi nyingine wasiomwabudu Yehova. Unaweza kumwona mmoja wao akiabudu mbele ya sanamu? Mwishowe wake zake wanamgeuza Sulemani, anaabudu miungu mingine. Unajua yanayotokea Sulemani anapofanya hivyo? Anakuwa mkali, na watu hawana furaha tena.

Kwa hiyo Yehova anamkasirikia Sulemani, naye anamwambia hivi: ‘Nitakunyang’anya ufalme nimpe mwingine. Sitafanya hivyo wakati wa maisha yako, bali wakati wa utawala wa mwanao. Ebu tuone hayo yanavyokuwa.

1 Nyakati 28:9-21; 29:1-9; 1 Wafalme 5:1-18; 2 Nyakati 6:12-42; 7:1-5; 1 Wafalme 11:9-13.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki