Wimbo 118
Kutegemeza Nyumba ya Mungu
1. Tufikirie nyumba ya Mungu
Tusipuze, mahali pakeye,
Nyumba aliyoichagua
Jina lake lije likae humo.
Kama Nehemia karudisha
’Bada katika ‘nyumba ya Mungu,’
Tuheshimu yeye kwa “zaka” zetu,
Tuonyeshe pendo kwa moyo wote.
(Korasi)
2. Jama’ ya Mungu ina umoja,
Ni jamaa aangaliayo.
‘Wakiliye,’ mwaminifu kwake,
Hivyo amani hukaa humo.
“Vitu vyenye thamani” tulete;
“Malimbuko” yanamuheshimu.
Hubariki jamaa yake vema,
Tutumikie kwa shangwe daima.
(KORASI)
Nyumba Mungu tegemeza.
‘Njoni mwabudu,’ twasihi.
Nyumbake ni jamaake;
Atakaa nao daima.