Wimbo 154
Yehova, Muumba Wetu
1. Yehova aliumba dunia vema.
Akawapa watu waishi humo.
Jeshi la malaika likafurahi
Kwa uumbaji; ni bora kabisa.
2. Na dunia itakuwa Paradiso.
Ndilo kusudi la Yehova Mungu.
Na dhambi ilitokezwa na uasi.
Twafurahi, karibu itakoma.
3. Ufalme utanyosha mambo kabisa.
Tunausubiri wakati huo.
Twaenda kutangaza habari njema,
Tuwape watu nuru ya ukweli.
4. Tunakazia Yehova macho yetu,
Yeye ni Muumba, na asifiwe.
Kwa hekima kafanyia watu vyote!
Twamusifu na kumutumikia.