Wimbo 163
Tunda la Roho
1. Tunda la roho yake Mungu
Ni lazima tulizae,
Hivyo tumuletee sifa,
Tukaupate uzima.
Nyakati zote tuonyeshe
Upendo kama wa Mungu.
Na kufurahi sikuzote,
Furaha huvumilisha.
2. Tuwe na amani ya Mungu
Tusitawi na umoja.
Muhimu ustahimilivu,
Tuwavumilie wote.
Fadhili zina matokeo!
Huwasikizisha watu.
Wema wafanya tugawie
Wote shangwe ya Ufalme.
3. Imani hutupa ‘jasiri
Nguvu kwa kusudi letu.
Nao upole ni bora we!
Unapunguza matata.
Kujiweza kwahitajiwa,
Tusikakose kibali.
Kuzaa matunda huleta
Kibali, tuyadumishe.