Wimbo 170
“Acheni Mungu Apatikane wa Kweli”
1. Yehova Mungu wa kweli
Hasemi uwongo.
Tumutegemee yeye;
Hajikani kamwe.
Atakuwa ni wa kweli;
Watu ni wawongo.
Kweli yake itadumu
Milele, milele.
2. Mungu ’lipotuma Mwana
Afanye mapenzi,
Kasema Mungu ni kweli,
Kwa neno na tendo.
Penzi la Yehova ’kawa
Ni sheria yake.
Alifurahia mema
Kaongoza watu.
3. Wajapodhihaki Neno
Wapende uwongo,
Kama Yesu, na tumwache
Mungu awe kweli.
Kwetu wahubiri Neno
Lina uamuzi.
Tunatafuta ukweli,
Twalitii Neno.