Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 6 kur. 46-53
  • Ulimwengu Ulioharibiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Ulioharibiwa
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “HAWAKUJALI”
  • KUOKOLEWA KWA WATU WENYE UTAWA
  • Kwa Nini Noa Alipata Kibali cha Mungu—Je, Hilo Linatuhusu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je! Wewe Walaani Vikali Ulimwengu Kupitia Imani Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Noa Auhukumu Ulimwengu kwa Imani Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ukombozi Wakaribia kwa Ajili ya Watu wa Ujitoaji Kimungu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 6 kur. 46-53

Sura 6

Ulimwengu Ulioharibiwa

1. (a) Je! zamani uharibifu wa ulimwengu umepata kuelekea wanadamu? (b) Kwa nini imetupasa tushukuru kwa vile Noa hakupuuza onyo la uharibifu huo?

WAKATI mmoja zamani, uharibifu wa ulimwengu ulikuwa ukikaribia sana. Watu wa mataifa yote wanaweza kushukuru kwa vile kati ya wazee wao alikuwamo mtu ambaye hakupuuza onyo la Mungu juu ya gharika ya dunia yote. Kwa sababu Noa alisikiliza akatii, yeye na mkeye, wanaye watatu na wake zao waliokoka. Sisi tumetoka katika ukoo wao.—Mwanzo 10:1, 32.

2. Kwa nini Mungu aliharibu ulimwengu huo?

2 Mungu aliuharibu ulimwengu huo kwa sababu alijua kwamba dunia ilikuwa imejaa jeuri. “Maovu ya mwanadamu [yalikuwa] makubwa duniani.” (Mwanzo 6:3, 5, 13) Hali zilifanana sana na zile zilizo katika karne yetu ya 20.

3. Ni nini kilichokuwa kimeifanya hali iwe mbaya sana?

3 Ni nini kilichokuwa kimefanya hali hiyo katika siku za Noa iwe mbaya sana? Sababu ya maana inafunuliwa katika andiko la Mwanzo 6:2, linaloripoti hivi: “Wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.” Lakini hilo lilikuwa na ubaya gani? Hao hawakuwa wanaume wa kibinadamu wa vivi hivi walioamua kuoa. Hao “wana wa Mungu” walikuwa malaika, viumbe wa kiroho, walioona wanawake warembo na pia raha zilizo katika ndoa, kisha wakachukua umbo la kibinadamu. (Linganisha Ayubu 1:6.) Kuvaa miili ya kibinadamu na kuoa kwao kulikuwa vitendo vya kumwasi Mungu. Maandiko yanaeleza kwamba “wakayaacha makao yao yaliyowahusu” na kwamba uhusiano wao na wanawake ulikuwa ‘usio wa asili,’ upotovu. (Yuda 6, 7; 1 Petro 3:19, 20) Watoto wao wa uzazi wenye mchanganyiko walikuwa wakubwa isivyo kawaida. Hao waliitwa Wanefili, au “waangushaji,” kwa sababu walikuwa wenye kuonea watu wengine.—Mwanzo 6:4.

4. (a) Kwa nini Noa alionyeshwa na Mungu kibali? (b) Ni matayarisho gani yaliyofanywa ili kuhifadhi uhai?

4 Ajapoishi katikati ya ulimwengu huo wenye ufisadi, Noa alipata kibali machoni pa Yehova. Kwa nini? Kwa sababu “Noa alikuwa mutu wa haki.” Yeye aliyafahamu masuala yaliyotokezwa katika Edeni, akajithibitisha kuwa asiye na kosa, “mtu wa ukamilifu.” (Mwanzo 6:8, 9, Zaïre Swahili Bible; The Jerusalem Bible) Ili ahifadhi Noa na jamaa yake, na pia aina za kila namna ya wanyama wa nchi kavu na viumbe wenye kuruka, Yehova alimwagiza ajenge safina, jengo kubwa mno mfano wa sanduku. Kama Mungu alivyoeleza: “Tazama mimi ninaleta gharika ya maji juu ya dunia ili niharibu mwili wote ambao ndani yake nguvu ya uhai inatenda utoke chini ya mbingu. Kila kitu kilicho katika dunia kitaisha.” (Mwanzo 6:13-17, New World Translation) Kwa hekima, Noa alimsikiliza Mungu na kumtii.

5. Gharika ilienea kadiri gani?

5 Gharika ikaja mwaka wa 2370 K.W.K., kama inavyoonyeshwa na orodha ya tarehe ya Biblia yenye mambo mengi. Ulikuwa ndio uharibifu mkubwa kuliko mwingine wote katika historia ya kibinadamu, hata kufika wakati wa sasa. Ulikuwa mkubwa sana hata “milima mirefu yote iliyokuwako chini ya mbingu ikafunikizwa.” (Mwanzo 7:19) Kwa Gharika “ulimwengu wa wakati ule ukapata uharibifu.” (2 Petro 3:6, New World Translation) Lakini labda mtu atauliza, ‘Ikiwa hata milima iliyokuwa mirefu zaidi ilifunikwa kwa maji, yako wapi maji hayo sasa?’ Kwa wazi yapo apa hapa duniani.

6. Baada ya Gharika, maji yote yalienda wapi?

6 Na ifahamike kwamba Biblia haisemi kwamba milima yo yote katika siku za Noa ilikuwa mirefu kama Mlima Kilimanjaro. Wanasayansi wamesema kwamba zamani milima mingi ilikuwa ya chini kuliko ilivyo sasa na ya kwamba milima mingine hata imesukumwa juu kutoka chini ya bahari nyingi. Zaidi ya hayo, imeaminiwa kwamba kulikuwa na wakati bahari kuu zenyewe zilipokuwa ndogo zaidi nazo kontinenti (bara) zilikuwa kubwa kuliko zilivyo sasa, kama inavyoshuhudiwa na mikondo ya mito inayopenya sana chini ya hizo bahari kuu. Lakini kwa habari ya hali ya sasa, gazeti National Geographic, katika toleo lake la Januari 1945, liliripoti hivi: “Kuna maji mengi sana katika bahari kuu kiasi cha mara kumi ya nchi kavu iliyo juu ya usawa wa bahari. Kama ungeitia nchi kavu hiyo kwa usawa katika bahari, maji yangeifunika dunia nzima, iende chini kilindini maili moja na nusu.” Hivyo, baada ya maji ya mafuriko kuanguka, lakini kabla kuinuliwa kwa milima na kushushwa kwa mabonde ya bahari hakujayafanya maji yakauke katika nchi kavu na kabla miamba ya barafu katika nchi zenye baridi nyingi haijaongezeka, kulikuwako maji ya kutosha kuifunika “milima mirefu yote,” kama Biblia inavyosema.—Mwanzo 7:17-20; 8:1-3; linganisha Zaburi 104:8, 9.

7, 8. Kuondoa Biblia, kuna habari gani juu ya Gharika?

7 Bila shaka gharika ya dunia yote yenye nguvu hivyo lazima iwe ilitia mkazo usioweza kusahauliwa kamwe kwa wale walioishi wakaiokoka. Vizazi vilivyokuwa vikija vingesimuliwa habari zayo. Kwa kuwa maandishi ya Biblia yanasema kwamba mataifa yote ni ukoo wa kikundi kile kile cha waokokaji wa Gharika, ni jambo la akili kutazamia kwamba katika sehemu zote za dunia kungekuwako ushahidi wa kumbukumbu fulani la mapema la uharibifu huo mkubwa. Je! ndivyo ilivyo? Bila shaka!

8 Watoto wa waokokaji hao wa Gharika walipohamia sehemu za mbali na kadiri wakati ulivyopita, habari hizo zilipotolewa kisha masimulizi hayo yakabadilishwa kulingana na mawazo ya kidini ya mahali fulani. Lakini katika hekaya za kale kuzunguka ulimwengu, watu wanakumbuka gharika kuu iliyoharibu wanadamu wote, wachache wakahifadhiwa. Haiwezi kuwa kwamba ni kwa sababu mambo hayo yanalingana sawasawa. Kumbukumbu la hayo linapatikana katika Mesopotamia na sehemu nyingine za Esia, katika Australia na visiwa vya Pasifiki, miongoni mwa makabila ya Wahindi kule Amerika Kaskazini na Kusini, katika hadithi zilizosimuliwa miongoni mwa Wagiriki wa kale na Waroma, katika Skandinevia, na miongoni mwa makabila ya Kiafrika. Masimulizi mengi kati ya hayo yanataja wanyama kuwa walihifadhiwa katika mashua pamoja na wanadamu. Kulingana na habari za Biblia, masimulizi fulani yanasema kwamba ndege walipelekwa nje wakaone wakati maji yalipokuwa yamepungua. (Linganisha Mwanzo 7:7-10; 8:6-12.) Hakuna tukio jingine la kale linalokumbukwa sana kote kote kama gharika.

9. Ni mazoea gani yanayoonyesha kumbukumbu la matukio ya “mwezi wa pili” katika kalenda ya Noa?

9 Mambo ya kihistoria yanayohusiana na Gharika yamegeuza desturi mpaka wakati wetu huu. Namna gani? Biblia inaripoti kwamba Gharika ilianza “mwezi wa pili, siku ya kumi na saba ya mwezi.” “Mwezi wa pili” huo unalingana na sehemu ya mwisho ya Oktoba na sehemu ya kwanza ya Novemba ya kalenda yetu. (Mwanzo 7:11) Kwa hiyo ni jambo linalostahili kuangaliwa kwamba watu wengi kuzunguka ulimwengu wanaadhimisha Siku ya Wafu au Karamu Kuu ya Wazee Waliokufa katika wakati huo wa mwaka. Ni kwa sababu gani wanaadhimisha wakati huo? Kwa sababu desturi hizo zinaonyesha kumbukumbu la uharibifu ule uliofanyizwa na Gharika.a

10. Kwa nini masimulizi ya Biblia juu ya Gharika ni yenye kutegemeka zaidi na yenye faida ya kibinafsi iliyo kubwa zaidi sana?

10 Hata hivyo, ni Biblia pekee iliyo na ushuhuda sahihi juu ya jambo lililotukia. Aliyoona Noa na kuyapitia yalikuja kutiwa baadaye katika Biblia. Karne nyingi baadaye, Mungu mwenyewe, alipokuwa akisema kupitia nabii Isaya, aliyataja “maji ya Noa.” (Isaya 54:9, Zaïre Swahili Bible) Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu aliyakumbuka matukio ya siku za Noa. Baadaye, alipokuwa duniani, Huyo, Yesu Kristo, alisema juu ya Gharika kuwa ni uhakika wa kihistoria na akaeleza sababu iliyofanya wengi sana wafe wakati huo.

“HAWAKUJALI”

11. Kwa nini watu wengi sana waliharibiwa katika Gharika?

11 Yesu hakusema kwamba kila mtu kuondoa nyumba ya Noa alikuwa mhalifu mwenye jeuri. Badala yake, alieleza hivi: “Kama walivyokuwa siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiozwa, mpaka siku ambayo Noa aliingia katika safina; nao hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwakumba wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa mtu [Yesu Kristo] kutakavyokuwa.”—Mathayo 24:37-39, New World Translation.

12. Kwa nini ‘kutojali’ kwao kulikuwa jambo la hatari sana?

12 Halikuwa kosa kwao kula na kunywa kwa kiasi wala kuoana kwa njia ya heshima. Lakini walipoonywa juu ya msiba wa dunia yote, kuendelea kwao kuweka maisha zao juu ya shughuli hizo za kibinafsi kulionyesha kwamba hawakuamini kweli kweli ama Noa ama Yehova Mungu, ambaye ujumbe wake wa kuonya alikuwa akitangaza Noa. Kama wangaliamini, wangaliulizia-ulizia habari ya jinsi wokovu ungewezekana kisha wachukue hatua ya haraka watimize matakwa. Labda baadhi ya watu hao walikubali kwamba jambo fulani lapasa kufanywa ili kukomesha jeuri iliyoenea kote kote siku hizo, lakini bila shaka gharika ya dunia yote haikuonekana kwao kuwa jambo linaloweza kutokea. Basi, kama Yesu alivyoeleza, “hawakujali [ujumbe wa Mungu kupitia Noa] mpaka gharika ikaja na kuwakumba wote.” Hilo liliandikwa uwe mfano wa kutuonya sisi.

13. (a) Kama ilivyotabiriwa, watu wengi leo wanatendaje wanapoambiwa kwamba Kristo yupo bila kuonekana, na kwa nini? (b) Petro anasema kuwa wanapuuza nini?

13 Vilevile mtume Petro aliyeongozwa na roho ya Mungu alitoa onyo alipoandika hivi: “Katika siku za mwisho [tulimo sasa] watakuja wadhihaki pamoja na dhihaka yao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe na kusema: ‘Ku wapi huku kuwapo kwake kulikoahidiwa? Kwani, tangu ile siku mababu zetu walipolala usingizi wa kifo, mambo yote yaendelea sawasawa kama yalivyokuwa tangu mwanzo wa kuumba.’” Watu kama hao hawataki kutozwa hesabu na mtu ye yote. Hivyo wanaondoa katika akili zao lile wazo la kuwapo kwa Kristo na kutakavyomaanisha kwa wale wanaofuatia njia ya maisha isiyo ya kumwogopa Mungu. Lakini Petro anaendelea kusema: “Kulingana na tamaa yao, wanakosa kufahamu uhakika huu, kwamba tangu zamani zilikuwako mbingu na dunia zikisimama imara nje ya maji na katikati ya maji kwa lile neno la Mungu; na kwa njia hizo ule ulimwengu wa wakati huo ulipatwa na uharibifu wakati ulipogharikishwa kwa maji. Lakini kwa neno lile lile zile mbingu na dunia zilizopo sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto nazo zimewekewa ile siku ya hukumu na ya kuharibiwa watu wasiomwogopa Mungu.”—2 Petro 3:3-7, New World Translation.

14. Kwa nini kutimizwa kwa “lile neno la Mungu” wakati wa uumbaji na siku za Noa kumepasa kutufanye tufikiri kwa uzito leo?

14 Wale wanaodhihaki wanapuuza uhakika wa kwamba “lile neno la Mungu” halikosi kutimizwa. Ili kukanusha maoni yao, mtume Petro anaturejeza nyuma kwenye wakati wa uumbaji. Wakati huo Mungu alisema: “Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.” Akiisha kutamka hivyo, “Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga.” Hivyo “lile neno la Mungu,” usemi wake wa kusudi, lilitimizwa. (Mwanzo 1:6, 7) Pia neno lake lilitimizwa alipoamuru kuwe na gharika ya dunia yote siku za Noa na akatumia maji hayo ili auharibu “ule ulimwengu wa wakati huo.” Na utakuja uharibifu juu ya mfumo wa mambo wa sasa usiomwogopa Mungu, kwa neno la Mungu lile lile lisilokanushika.

15. (a) Kwa nini andiko la 2 Petro 3:7 halitabiri kuchomwa kwa Dunia-sayari? (b) Basi, ni “mbingu” gani na “dunia” gani ambazo “zimewekwa akiba kwa ajili ya moto”?

15 Kilichotukia wakati huo wa Gharika kilikuwa mfano wa mambo yatakayokuja. Dunia haikuharibiwa wakati huo, lakini watu wasiomwogopa Mungu ndio walioharibiwa. Basi, ni nini maana ya usemi wa kwamba “mbingu na dunia zilizopo sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto”? (2 Petro 3:7; 2:5, New World Translation) Lakini, moto halisi ungefanya nini na jua ambalo tayari ni lenye moto sana na nyota katika mbingu zetu zinazoonekana? Na kuchomwa kwa dunia halisi kungepatanaje na kusudi la Mungu la kuifanya iwe Paradiso? Kwa wazi, bila shaka “mbingu na dunia zilizopo sasa,” zinazotajwa hapa, ni za mfano. (Linganisha Mwanzo 11:1; 1 Wafalme 2:1, 2; 1 Mambo ya Nyakati 16:31.) “Mbingu” hizo zinafananisha mamlaka za kiserikali zenye kuinuka juu ya wanadamu kwa ujumla, na “dunia” ni jamii ya kibinadamu isiyomwogopa Mungu. Hizo zitaharibiwa kabisa-kabisa kana kwamba kwa moto, katika ile siku kuu ya Yehova. Wale wanaoendelea kudhihaki onyo la kimungu juu ya hilo wanaweka maisha zao katika hatari kubwa.

KUOKOLEWA KWA WATU WENYE UTAWA

16. Kama inavyoonyeshwa katika 2 Petro 2:9, ufunguo wa kwenye wokovu ni nini?

16 Masimulizi hayo ya Gharika yanaonyesha kiwazi sana jambo tunalohitaji sisi leo tulizingatie moyoni. Ni jambo gani? Baada ya kuelekeza kwenye jambo ambalo Mungu alifanya katika siku za Noa, mtume Petro anamalizia hivi: “Yehova ajua jinsi ya kuokoa watu wenye utawa katika jaribu, bali kuwaweka akiba watu wasio haki kwa siku ya hukumu wakatiliwe mbali.” (2 Petro 2:9, New World Translation) Basi, ufunguo wa kwenye wokovu ni mtu kuwa mwenye utawa.

17. Noa alionyeshaje ushahidi wa kuwa mwenye utawa?

17 Maana ya hilo ni nini? Kwa wazi Noa alikuwa mtu mwenye utawa. “Noa alitembea pamoja na Mungu wa kweli.” (Mwanzo 6:9, New World Translation) Yeye alifuatia mwendo wa maisha uliopatana na mapenzi ya Yehova yaliyofunuliwa. Alikuwa na uhusiano wa kibinafsi ulio karibu sana na Mungu. Kujenga safina na kukusanya namna namna za ndege na wanyama wote kulikuwa kazi kubwa mno. Noa hakuwa na mwelekeo wa kusema ngoja-tuone. Yeye alikuwa na imani. Noa akafanya “sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.” (Mwanzo 6:22; Waebrania 11:7) Watu walihitaji kukumbushwa njia za uadilifu za Yehova na kuonywa juu ya uharibifu uliokuwa ukija juu ya wasiomwogopa Mungu. Noa alifanya hivyo pia akiwa “mhubiri wa uadilifu.”—2 Petro 2:5, New World Translation.

18. Kwa nini, bila shaka, kila mtu aliyeokoka Gharika alikuwa na utawa huo?

18 Vipi mke wa Noa, wanaye na wake zao—walitakwa kufanya nini? Masimulizi ya Biblia yanakaza fikira juu ya Noa kwa sababu yeye alikuwa kichwa cha jamaa, lakini bila shaka wengine pia walikuwa watu wenye utawa. Kwa nini hivyo? Kisa cha watoto wa Noa kilikuja kutajwa na Yehova baadaye akimwambia nabii wake Ezekieli ili aonyeshe kwamba, ikiwa Noa angekuwa akiishi katika Israeli wakati huo, watoto wake hawangeweza kutazamia wokovu kwa kutegemea uadilifu wa baba yao. Walikuwa na umri wa kutosha kuweza kutii au kutotii, hivyo walihitaji wao binafsi waonyeshe ushahidi wa utawa wao kwa Yehova na njia zake za uadilifu.—Ezekieli 14:19, 20.

19. Hivyo, imetupasa tuwe tukifanya nini, na jinsi gani?

19 Kwa sababu bila shaka uharibifu wa ulimwengu unakaribia sana, Biblia inatuomba sana tuendelee kuuweka karibu sana akilini na kujithibitisha kwamba sisi, pia, ni watu wenye utawa. (2 Petro 3:11-13) Katika sehemu zote za dunia, kuna watu leo kutoka kati ya wazao wa Noa, wanaolifuata shauri la hekima hilo na watakaokuwa waokokaji wa kuingia katika “dunia mpya.”

[Maelezo ya Chini]

a The Worship of the Dead, (London; 1904), cha Kanali J. Garnier, kurasa 3-8; Life and Work at the Great Pyramid (Edinburgh; 1867), Buku la 2, cha Profesa C. Piazai Smyth, kurasa 371-424.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki