Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • su sura 19 kur. 145-151
  • “Tumesikia Kwamba Mungu Yu Pamoja na Ninyi Watu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Tumesikia Kwamba Mungu Yu Pamoja na Ninyi Watu”
  • Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “SISI TUTAENDA NA NINYI WATU”
  • WANATAMBULIKANA NAMNA GANI?
  • MIFANO INAYOSTAHILI KUFUATWA
  • Kitabu Cha Biblia Namba 38—Zekaria
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • ‘Penda Kweli na Amani’!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Jinsi Lilivyo Tukufu Jina la Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • ‘Alitangazwa Kuwa Mwadilifu kwa Matendo’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
su sura 19 kur. 145-151

Sura 19

“Tumesikia Kwamba Mungu Yu Pamoja na Ninyi Watu”

1, 2. (a) Unabii wa Zekaria 8:23 unatabiria wakati wetu nini? (b) Ni nani Mungu huyo anayetajwa hapo, na Biblia inakaziaje jina lake binafsi?

“SISI tutaenda na ninyi watu, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na ninyi watu.” Hivyo ndivyo Biblia ilivyotabiri kwamba watu kutoka mataifa yote wangekuwa wakisema wakati wetu. (Zekaria 8:23, New World Translation) Na ni nani Mungu huyu ambaye unabii wa Zekaria unaelekeza kwake? Hatuachwi katika shaka. Katika kitabu hicho kimoja cha Biblia kilicho kidogo kikilinganishwa na vingine, jina lake binafsi laonekana mara 135. Ni YEHOVA!

2 Yeye mwenyewe alisema hivi juu ya jina lake binafsi, Yehova: “Hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.” (Kutoka 3:15) Umaana wa jina hilo unaonyeshwa na uhakika wa kwamba linaonekana karibu mara 7,000 katika maandishi kamili ya awali ya Biblia ya Kiebrania—mara nyingi zaidi ya jumla yenye kuunganishwa pamoja ya mitajo ya cheo kama Bwana na Mungu. Kama ilivyotabiriwa, hizi “siku za mwisho” jina hilo limekuja kuhusishwa kwa kutokeza na kikundi kimoja cha watu.

“SISI TUTAENDA NA NINYI WATU”

3. Kama ilivyotabiriwa katika Zekaria 8:20-23, (a) ni nani ambao wangetafuta Yehova? (b) na kwa kushirikiana na nani?

3 Kwa habari hiyo, nabii Zekaria, wakati wa kujengwa upya kwa hekalu la Yehova katika Yerusalemu wa kale, aliongozwa na roho ya Mungu aandike: “Hivi ndivyo Yehova wa majeshi amesema, ‘Bado itakuwa ya kwamba jamii za watu na wakaaji wa miji mingi watakuja; na wakaaji wa mji mmoja hakika wataenda kwa wale wa mji mwingine, wakisema: “Na twende bila kufanya mchezo tukaulainishe uso wa Yehova na kutafuta Yehova wa majeshi. Mimi mwenyewe nitaenda pia.” Na jamii nyingi za watu na mataifa yenye nguvu yatakuja hakika kutafuta Yehova wa majeshi katika Yerusalemu na kuulainisha uso wa Yehova.’ Hivi ndivyo Yehova wa majeshi amesema, ‘Itakuwa siku hizo kwamba wanaume kumi kutoka lugha zote za mataifa watashika, ndiyo, hakika watashika rinda la mwanamume aliye Myahudi, wakisema: “Sisi tutaenda na ninyi watu, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na ninyi watu.”’”—Zekaria 8:20-23, New World Translation.

4. Kwa nini unabii huo hauhusu dini ya Wayahudi wala Jumuiya ya Wakristo?

4 Utimizo mdogo wa unabii huo uliotokea kuhusiana na kujengwa upya kwa hekalu Yerusalemu, kuanzia siku za Zerubabeli, ulielekeza mbele kwenye utimizo ulio mkubwa zaidi wakati wetu. Kuhusiana na watu gani? Bila shaka halingekuwa jambo la akili kwa wale ‘wanaotafuta Yehova’ kuendea watu ambao kwa ushirikina wanakataa hata kulitamka jina la Mungu, kama wafanyavyo Wayahudi wa asili wanaoshikilia ibada yao ya kimapokeo. Wala hawangeendea Jumuiya ya Wakristo, inayofuata mfano wa desturi ya Kiyahudi ya kuepuka kutumia jina la kimungu. Si Yerusalemu wa kidunia ambao watu katika wakati wetu wanaendea wakamwabudu Yehova. Kama Yesu alivyotabiri, Mungu alilihama hekalu lake huko, nalo liliharibiwa mwaka wa 70 W.K., lisipate kujengwa upya tena kamwe mpaka leo hii. Hilo lamwonyesha mtu ye yote aliye na akili kwamba Mungu hayupo pamoja na taifa la Israeli lisilo la Kikristo.—Mathayo 23:37, 38; linganisha 1 Wafalme 9:8, 9.

5. Maandiko yanatambulishaje (a) “Yerusalemu” unaowakilisha Yehova leo? (b) “mwanamume aliye Myahudi” ambaye kwa habari zake Zekaria alitabiri?

5 “Yerusalemu” unaomwakilisha leo Yehova unaelezwa katika Waebrania 12:22 kuwa “mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni.” Kama vile Yerusalemu wa kale ulivyokuwa mfano wenye kuonekana wa utawala wa Yehova, “Yerusalemu wa mbinguni” ni Ufalme wa Kimasihi wa Mungu alimotawazwa Yesu Kristo kuwa Mfalme mwishoni mwa Majira ya Mataifa mwaka wa 1914. (1 Mambo ya Nyakati 29:23; Luka 21:24) Serikali hiyo ina wawakilishi hapa duniani, wale wanaoitangaza kwa ushikamanifu kuwa ndiyo tumaini hakika la pekee kwa wanadamu. Wale waliokuwa wa kwanza kutangaza kwamba Ufalme umesimamishwa mwaka wa 1914 ni mabaki ya “kundi dogo.” Hao ndio “Israeli wa Mungu,” Israeli wa kiroho. Hao ndio wale ‘Wayahudi’ wa kiroho ambao Zekaria alitabiri habari zao. (Luka 12:32; Wagalatia 6:16; Warumi 2:28, 29) Kwa sababu ya upendo wao kwa Mungu na kuthamini kwao daraka la kujulisha kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli Mweza Yote, tangu mwaka wa 1931 wamekubali kuitwa jina Mashahidi wa Yehova.—Isaya 43:10-12.

WANATAMBULIKANA NAMNA GANI?

6. (a) Ni nini kimesadikisha mamilioni ya watu juu ya utambulishi wa watu ambao Mungu yu pamoja nao leo? (Fikiria jambo moja kwanza; yasome maandiko.) (b) Ni jambo au mambo gani ambayo yamekuwa yenye kukuvutia wewe binafsi?

6 Kwa sababu Wayahudi hao wa kiroho wametimiza kwa uaminifu daraka lao la kuwa Mashahidi wa Yehova, mamilioni ya watu wenye mioyo minyofu kuzunguka dunia wamesaidiwa ‘watafute Yehova.’ Wamekuja kufahamu kwamba Yehova yupo pamoja na watu hawa kweli kweli wanaochukua jina lake. Ni nini kinachowasadikisha hivyo? Mambo mengi, yenye kutokeza kati ya hayo ni haya:

(1) Imani zote za Mashahidi wa Yehova zinategemea Biblia—si maandiko machache tu bali Neno la Mungu lote. Badala ya kufundisha mambo yao wenyewe, Mashahidi wa Yehova wanajibu maulizo kwa kuonyesha yanayosemwa na Biblia. Wanamheshimu Yehova kwa kumwacha yeye aseme. (Linganisha Yohana 7:16-18.)

(2) Biblia inasema kwamba Mungu mwenyewe angechukua katika mataifa ‘watu kwa ajili ya jina lake.’ (Matendo 15:14) Ni wao binafsi ambao wangeita juu ya jina lake na wangejitahidi kulijulisha katika dunia yote. (Isaya 12:4, 5) Ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova ndio watu ambao kwa wazi wanahusiana na jina la binafsi la Mungu, Yehova.

(3) Mashahidi wa Yehova wana wingi wa chakula cha kiroho chenye kuridhisha. Mambo wanayojifunza kutoka Maandiko na matokeo ya hayo kwenye maoni yao juu ya maisha yanawafanya kuwa watu wenye furaha, tofauti na ulimwengu kwa ujumla. Hivyo ndivyo Yehova alisema watumishi wake wangekuwa. (Isaya 65:13, 14; linganisha Mathayo 4:4.)

(4) Mashahidi wa Yehova wanatumia Neno la Mungu ili kuweka kiwango cha mwenendo na kuongoza maamuzi yao katika mambo ya kila siku ya maisha—katika jamaa zao, kazini, shuleni, katika uchaguzi wa tafrija, katika kutambua mazoea yanayopasa kuepukwa, katika kuamua zilizo shughuli zinazofaa zaidi sana za kushiriki. Yehova aliahidi kwamba ‘yeye mwenyewe angenyosha mapito’ ya wale wanaofanya hivyo. (Mithali 3:5, 6)

(5) Uangalizi wa makundi ya Mashahidi wa Yehova unafuata mfano wa kundi la Mungu la karne ya kwanza. Katika kundi hilo wazee walikuwa mifano kwa kundi na wafanya kazi wenzi wa wengine kwa ajili ya Ufalme wa Mungu badala ya kuwa jamii yenye kujitukuza ya mapadri. (1 Petro 5:2, 3; 2 Wakorintho 1:24)

(6) Mashahidi wa Yehova hawajiingizi katika mambo ya kisiasa ya ulimwengu bali wanaifanya kazi ambayo Biblia imewekea Wakristo wa kweli wafanye, yaani, kuzihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika ulimwengu wote kuwa ushuhuda kabla mwisho haujaja. (Mathayo 24:14; linganisha Yohana 17:16; 18:36.)

(7) Mashahidi wa Yehova wanapendana kweli kweli, kama Yesu alivyosema wanafunzi wake wa kweli wangependana. Rangi ya ngozi, kabila alikotoka mtu, hali za kiuchumi, taifa, lugha—hakuna mojapo hayo linalomfanya mmoja amdharau mwingine. Ijapokuwa makosa ya kibinadamu, wao wameungana wote kweli kweli kuwa udugu wa mataifa yote, na wanampa Mungu sifa yote kwa sababu hiyo. (Yohana 13:35; linganisha Matendo 10:34, 35.)

(8) Kama Wakristo wa kwanza, Mashahidi wa Yehova katika nyakati za kisasa wanazidi tu kumtumikia Mungu bila kujali mateso. Kwa kumtumainia Mungu, hawalipi kisasi juu ya wapinzani. Kama ilivyokuwa zamani, Mungu amejithibitisha kuwa pamoja na watumishi wake awaokoe. (Yeremia 1:8; Isaya 54:17)

7. (a) Wale “watu kumi” ni nani? (b) Wanatoaje ushahidi kwamba Yehova amekuwa Mungu wao kweli kweli?

7 Hizo ni chache za sababu kwa nini, kama ilivyotabiriwa, “wanaume kumi kutoka lugha zote za mataifa” wanasema kwa usadiki wa kweli, wakiwaambia mabaki ya warithi wa Ufalme hivi: “Sisi tutaenda na ninyi watu, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na ninyi watu.” (Zekaria 8:23, New World Translation) Maandiko yanatumia “kumi” kufananisha ukamili wa mambo ya kidunia, hivyo “wanaume kumi” hao wanafananisha wote wanaofuata ibada ya kweli sasa kwa kushirikiana na “ndugu” za Kristo wapakwa-mafuta kwa roho. Wao hawashirikiani tu pamoja na mabaki kwenye mikutano yao bali wanajitambulisha kuwa waabudu wa Mungu wao, Yehova. Wanaweka maisha zao wakfu kupitia Yesu Kristo na kuonyesha hivyo kwa ubatizo wa maji, wakionyesha hivyo kwamba wanataka ‘kujiunga na Yehova.’ Kisha wanashiriki kwa furaha kazi inayofanywa duniani pote na mashahidi wake.—Zekaria 2:11; Isaya 61:5, 6.

MIFANO INAYOSTAHILI KUFUATWA

8. (a) Ni nini kilichomfanya malkia wa Sheba asafiri kwenda Yerusalemu? (b) Alipofika huko, alifanya nini, na matokeo yakawa nini? (c) Kumekuwaje watu walio kama yeye siku zetu? (Zaburi 2:10-12)

8 Baadhi ya watu wanaochukua hatua hiyo wanafanana na malkia wa Sheba siku za Sulemani. Toka mbali ‘yeye alikuwa akisikia habari za Sulemani juu ya jina la Yehova.’ Yeye hakuwa amepata kusema binafsi pamoja na Sulemani wala hakuwa amepata kuwako kwenye hekalu la Yehova katika Yerusalemu. Alikuwa na mashaka fulani juu ya kama yote aliyokuwa amesikia yangeweza kuwa ya kweli. Lakini akajitahidi aende kuchunguza, akisafiri kilometa 2,250 (maili 1,400) akitumia ngamia. Alipata majibu ya “maswali ya mafumbo” yake yote, kisha akapaaza sauti hivi: “Tazama, sikuambiwa nusu.” Aliweza kulazimika kukata shauri kwamba Yehova aliwapenda watu wake. (1 Wafalme 10:1-9) Watu fulani ambao wamekuwa wenye vyeo katika ulimwengu wamefuata mfano wake leo, na wengi kutoka hali zilizo za chini zaidi wamefanya hivyo. Wanaona ushahidi wa kwamba Mashahidi wa Yehova hawamtumainii mwanadamu bali Yesu Kristo, ambaye ndiye Sulemani Mkubwa Zaidi, kuwa Mfalme wao. Majibu wanayopewa kutoka Neno la Mungu yanaridhisha akili na mioyo yao, na wanahisi kuongozwa kuunganisha sauti zao katika kumbariki Yehova.—Linganisha Luka 11:31.

9. (a) Ni kwa njia gani mwelekeo wa Rahabu ulikuwa tofauti na ule wa malkia wa Sheba? (b) Ni nini kilichostahili kuangaliwa juu ya matukio yaliyoongoza kwenye kuhifadhiwa kwa Rahabu na nyumba yake? (c) Ni nini kinachowatambulisha watu walio mfano wa Rahabu leo?

9 Wengine ni kama Rahabu wa Yeriko, ambaye tayari alikuwa amesadikishwa na ripoti alizopokea kwamba Mungu wa Israeli alikuwa “ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.” (Yoshua 2:11) Wapelelezi kutoka Israeli walipoingia katika nchi, aliwakaribisha, akawaficha na kuhatirisha maisha yake ili awalinde. Alikuwa na imani na alitoa ushahidi wa imani hiyo kwa matendo yake, akajipanga na watu wa Yehova. (Waebrania 11:31; Yakobo 2:25) Alifuata kwa uangalifu maagizo aliyopewa ili apate kuhifadhiwa. Pia Rahabu alionyesha kuhangaikia kwa upendo baba na mama yake, ndugu na dada zake, kukiwafungulia njia ya kuja kuokolewa ikiwa wangeyatii matakwa ya kuokoka. (Yoshua 2:12, 13, 18, 19) Matokeo ni kwamba yeye na nyumba yake waliokolewa wakati Yeriko na wakaaji wake wenye kuabudu Baali walipoangamizwa. (Yoshua 6:22, 23) Hilo lina maana yenye nguvu sana wakati wetu. Linaonyesha kwamba Yehova ataokoa watu walio mfano wa Rahabu. Ni nini kinachoonyesha wako kama yeye? Wanamwamini Yehova, wanajitambulisha kuwa upande wa washiriki wa Israeli wa kiroho, wanafuata sana maelekezo yanayotolewa kwa njia ya kipitio hicho na wanajaribu kwa bidii wasaidie washiriki wa karibu sana wa jamaa na watu wengine wa ukoo wao wapate hekima ya kufanya kama hivyo.

10. (a) Kama unabii wa Zekaria unavyoonyesha, hasa ni kitu gani kinachovutia watu hata wakashirikiana na Mashahidi wa Yehova? (b) Sisi tunaweza kuonyeshaje, kwa mwelekeo na kwa vitendo, kwamba kumpenda Yehova ndiko kunakojaa mioyo yetu kweli kweli?

10 Bila shaka, Yehova Mungu mwenyewe ndiye anayevuta watu wa mataifa yote waje katika ushirika pamoja na Mashahidi. Neno lake linawavutia. Tunda la roho yake katika maisha za watumishi wake ni lenye kuwavutia. Wanapozijua sana sifa zake na matendo yake kwa wanadamu, wanautamani sana ule wakati ambao jina la Mungu litaondolewa malawama yote ambayo Shetani na wanadamu wasio na imani wamerundika juu yalo. Wao wenyewe wanaendesha mambo yao kwa njia itakayokuwa yenye kupendeza Muumba wao na itakayovuta wengine wamtukuze yeye. (1 Petro 2:12) Wanasali kwa mioyo yao yote kama Yesu alivyofundisha wanafunzi wake kusali: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Na, kwa kupatana na sala yao wanamtolea Mungu utumishi mtakatifu kwa umoja kamili pamoja na wale wanaotoa ushahidi ulio wazi wa kwamba wao ni ‘watu kwa ajili ya jina la Yehova.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki