Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 49
  • Safari Nyingine ya Kuhubiri Galilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Safari Nyingine ya Kuhubiri Galilaya
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Safari Nyingine ya Kuhubiri Galilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kuhubiri Galilaya na Kuwazoeza Mitume
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Iweni Wavunaji Wenye Furaha!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 49

Sura 49

Safari Nyingine ya Kuhubiri Galilaya

BAADA ya miaka miwili hivi ya kuhubiri kwa bidii nyingi, je! Yesu sasa ataanza kupunguza bidii yake na kustarehe? Tofauti na hilo, yeye anafanya utendaji wake wa kuhubiri kwa kuanza safari nyingine bado, safari ya tatu ya Galilaya. Yeye anazuru majiji na vijiji vyote katika eneo hilo, akifundisha katika masinagogi na kuhubiri habari njema za Ufalme. Yale anayoona katika safari hii yanamsadikisha hata zaidi kuliko wakati mwingine wowote juu ya uhitaji wa kuzidisha kazi yake ya kuhubiri.

Kokote Yesu aendako, yeye anaona umati wenye uhitaji wa ponyo la kiroho na faraja. Wao ni kama kondoo wasio na mchungaji, waliochunwa ngozi na kutawanyika, naye anawahurumia. Anawaambia wanafunzi wake: “Naam, mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache. Basi, mwombeni Bwana-Mkubwa wa mavuno apeleke nje wafanyakazi katika mavuno yake.”

Yesu ana mpango wa tendo. Yeye anawaita wale mitume 12, aliokuwa amewachagua karibu mwaka mmoja mapema. Yeye awagawanya kuwa jozi, akifanyiza vikoa sita vya wahubiri, na kuwapa maagizo. Aeleza hivi: “Msiiendee njia ya mataifa, na msiingie katika jiji la Samaria; bali, badala ya hivyo, endeleeni kuwaendea wale kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Mwendapo, hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa zile mbingu umekaribia karibu.’”

Ufalme huu ambao wapaswa kuhubiri juu yao ni ule ambao Yesu aliwafundisha kuombea katika ile sala ya kiolezo. Ufalme huo umekaribia karibu katika maana ya kwamba Yesu Kristo, Mfalme aliyechaguliwa na Mungu, yupo. Ili kuthibitisha madai ya wanafunzi wake kuwa mawakili wa serikali hiyo yenye uwezo upitao wa kibinadamu, Yesu awapa uwezo wa kuwaponya wagonjwa na hata kufufua wafu. Yeye anawaagiza kufanya utumishi huo bure.

Halafu yeye anawaambia wanafunzi wake wasifanye matayarisho ya mambo ya kimwili kwa ajili ya safari yao ya kuhubiri. “Msijipatie dhahabu au fedha au shaba kwa ajili ya vibeti vyenu vya mishipini, au mfuko wa chakula kwa ajili ya safari yenu, au nguo za ndani mbili, au makubazi au fimbo; kwa kuwa mfanyakazi anastahili chakula chake.” Wale wanaothamini ujumbe ule wataitikia na kuchanga chakula na nyumba. Kama Yesu asemavyo: “Jiji lolote au kijiji chochote kile mwingiacho, tafuteni nani katika hicho anastahili, na kukaa humo mpaka mwondokapo.”

Ndipo Yesu anawapa maagizo ya jinsi ya kuwaendea wenye nyumba wakiwa na ujumbe wa Ufalme. “Mnapokuwa mkiingia katika nyumba,” anaagiza, “wasalimuni watu wa nyumba hiyo; na ikiwa nyumba hiyo yastahili, acheni amani mnayoitakia iikalie; lakini ikiwa haistahili, acheni amani kutoka kwenu iwarudie nyinyi. Kokote kule ambako yeyote hawakaribishi au kusikiliza maneno yenu, mwondokapo nyumba au jiji hilo kung’uteni mavumbi kutoka kwenye nyayo zenu.”

Kuhusu jiji ambalo lakataa ujumbe wao, Yesu afunua kwamba hukumu juu yalo itakuwa kali kweli kweli. Yeye anaeleza: “Kweli kweli mimi nasema kwenu nyinyi, Itavumilika zaidi kwa bara la Sodoma na Gomora katika Siku ya Hukumu kuliko kwa jiji hilo.” Mathayo 9:35–10:15; Marko 6:6-12; Luka 9:1-5, NW.

▪ Ni wakati gani Yesu anaanza safari ya tatu ya kuhubiri Galilaya, nayo inamsadikisha juu ya nini?

▪ Anapowatuma mitume wake 12 kuhubiri, yeye anawapa maagizo gani?

▪ Kwa nini ni sahihi kwa wanafunzi kufundisha kwamba Ufalme umekaribia karibu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki