Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 52
  • Yesu Alisha Maelfu kwa Muujiza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Alisha Maelfu kwa Muujiza
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alisha Maelfu kwa Mwujiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Alisha Maelfu kwa Mikate na Samaki Wachache
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Analisha Watu Wengi Chakula
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yesu Analisha Maelfu ya Watu
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 52

Sura 52

Yesu Alisha Maelfu kwa Muujiza

WALE mitume 12 wamefurahia ziara nzuri ajabu ya kuhubiri katika sehemu zote za Galilaya. Sasa, muda mfupi tu baada ya Yohana kuuawa, wanarudia Yesu na kusimulia mambo mazuri ajabu waliyoona. Anapoona kwamba wamechoka na kwamba watu wengi sana wanakuja na kwenda hivi kwamba wao hawana hata wakati wa kula, Yesu anasema: ‘Acheni sisi twende peke yetu wenyewe mahali pa upweke ambapo nyinyi mnaweza kupumzika vya kutosha.’

Wakipanda mashua yao, labda karibu na Kapernaumu, wanaelekea mahali palipo mbali kabisa, kwa wazi mashariki mwa Yordani mbele ya Bethsaida. Hata hivyo, watu wengi wanawaona wakiondoka, na wengine wanapata kujua jambo hilo. Wote hao wanapiga mbio kuwatangulia wakiwa kandokando ya ufuo, na wakati mashua inapotua, watu hao wanakuwa pale kuwalaki.

Anapotoka mashuani na kuuona umati ule mkubwa, Yesu anasukumwa na sikitikio kwa sababu watu hao ni kama kondoo wasio na mchungaji. Kwa hiyo yeye anaponya wagonjwa wao na kuanza kuwafundisha mambo mengi.

Wakati unapita kwa haraka, na wanafunzi wa Yesu wanamjia na kusema: “Mahali hapa pako peke yapo, na tayari saa imeenda sana. Waage waende zao, ili waende na kuingia sehemu za mashambani na vijiji vinavyozunguka wakajinunulie kitu cha kula.”

Hata hivyo, katika kujibu Yesu anasema: “Nyinyi wapeni kitu cha kula.” Ndipo, kwa kuwa Yesu tayari anajua jambo ambalo atafanya, yeye anatahini Filipo kwa kumuuliza: “Tutanunua wapi mikate ili hawa wale?”

Kwa maoni ya Filipo hali hiyo haiwezekani. Kwani, kuna wanaume 5,000, na labda watu wanaozidi sana 10,000 kuhesabu pia wanawake na watoto! Filipo anaitikia kwamba “mikate ya kima cha dinari [wakati huo dinari ilikuwa mshahara wa siku nzima] mia mbili haiwatoshi, ili kwamba kila mmoja apate kidogo.”

Labda ili aonyeshe jinsi isivyowezekana kulisha watu wengi hivyo, Andrea ajitolea kusema: “Hapa yupo kivulana aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wadogo wawili,” akiongezea, “lakini hivi ni nini miongoni mwa wengi hivyo?”

Kwa kuwa ni wakati wa masika, kabla tu ya Sikukuu ya Kupitwa 32 W.K., kuna manyasi mengi mabichi. Hivyo Yesu awaagiza wanafunzi wake waambie watu waketi kwenye manyasi wakiwa vikundi-vikundi vya 50 na vya 100. Yeye anachukua ile mikate mitano na samaki wawili, anatazama mbinguni, na kutamka baraka. Kisha anaanza kuimega mikate ile na kugawanya samaki wale. Anawapa wanafunzi wake, ambao, nao, wanawagawia watu. Jambo la kustaajabisha ni kwamba, watu wale wote wanakula mpaka wanashiba!

Baadaye Yesu anawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni pamoja vipande vilivyobakia, ili kwamba kitu chochote kisitapanywe.” Wanapofanya hivyo, wanajaza vikabu 12 vyenye masazo kutokana na walivyokula! Mathayo 14:13-21; Marko 6:30-44; Luka 9:10-17; Yohana 6:1-13, NW.

▪ Kwa nini Yesu anatafutia wanafunzi wake mahali pa faragha?

▪ Yesu anapeleka wanafunzi wake wapi, na kwa nini uhitaji wao wa pumziko unakosa kutimizwa?

▪ Saa inapoendelea sana, wanafunzi wanahimiza nini, lakini Yesu anatunzaje wale watu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki