Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 96
  • Yesu na Mtawala Kijana Tajiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu na Mtawala Kijana Tajiri
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu na Mtawala Kijana Tajiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Yesu Amjibu Mtawala Kijana Aliye Tajiri
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Mtawala Tajiri Anafanya Uamuzi Usiofaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Baraka ya Yehova Inatajirisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 96

Sura 96

Yesu na Mtawala Kijana Tajiri

YESU anapoendelea kupitia wilaya ya Perea kuelekea Yerusalemu, mwanamume kijana akimbia na kupiga magoti mbele yake. Mwanamume huyo anaitwa mtawala, labda ikimaanisha kwamba ana cheo mashuhuri katika sinagogi la kwao au hata kwamba yeye ni mshiriki wa Sanhedrini. Pia, yeye ni tajiri sana. “Mwalimu Mwema,” yeye auliza, “ni lazima mimi nifanye nini ili nirithi uhai wa milele?”

“Kwa nini waniita mwema?” Yesu ajibu. “Hakuna mtu mwema, isipokuwa mmoja, Mungu.” Yaelekea kwamba mwanamume huyo kijana atumia neno “mwema” kama cheo, kwa hiyo Yesu anamjulisha kwamba cheo hicho ni cha Mungu tu.

“Ingawa hivyo,” Yesu anaendelea kusema, “ikiwa wewe wataka kuingia katika uhai, zishike amri kwa kuendelea.”

“Zipi?” mwanamume huyo auliza.

Akitaja tano za Amri Kumi, Yesu ajibu hivi: “Kwani, Ni lazima wewe usiue, Ni lazima wewe usifanye uzinzi, Ni lazima wewe usiibe, Ni lazima usitoe ushahidi wa bandia, Heshimu baba yako na mama yako.” Na akiongezea amri iliyo ya maana hata zaidi, Yesu asema: “Ni lazima wewe upende jirani yako kama wewe mwenyewe.”

“Mambo haya yote mimi nimeyashika kutoka ujana wangu na kuendelea,” mwanamume huyo ajibu kwa weupe wote wa moyo. “Ningali ninapungukiwa nini?”

Kwa kusikiliza ombi la mwanamume huyo lenye juhudi na bidii nyingi ya moyoni, Yesu ahisi upendo kwake. Lakini Yesu ahisi kwa fahamu zake kwamba mwanamume huyu ana ushikamano mwingi kwa mali za kimwili, na kwa hiyo amwonyesha wazi uhitaji wake: “Jambo moja linakosekana kuhusu wewe: Enda, kauze vitu ulivyo navyo na kuwapa maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni, nawe uje uwe mfuasi wangu.”

Yesu atazama, bila shaka akiwa na sikitiko, huku mwanamume huyo akiinuka na kugeuka aende zake kwa huzuni yenye kina kirefu. Utajiri wake wampofusha asiione thamani ya hazina ya kweli. “Itakuwa vigumu kama nini,” Yesu aomboleza, “kwa wale wenye pesa kuingia katika ufalme wa Mungu!”

Maneno ya Yesu yawashtua wanafunzi. Lakini wao washangaa hata zaidi aendeleapo kutaja kanuni ya ujumla: “Kwa uhakika, ni rahisi zaidi ngamia kupitia jicho la sindano ya kushonea kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”

“Kwa uhakika, ni nani awezaye kuokolewa?” wanafunzi wataka kujua.

Akiwatazama moja kwa moja, Yesu ajibu hivi: “Kwa wanadamu haiwezekani, lakini sivyo ilivyo kwa Mungu, kwa maana mambo yote yawezakana kwa Mungu.”

Kwa kuona kwamba wao wamefanya chaguo lenye kutofautiana sana na lile la mtawala kijana tajiri, Petro asema hivi: “Tazama! Sisi tumeacha vitu vyote na kukufuata wewe.” Kwa hiyo anauliza hivi: “Kutakuwako nini hasa kwa ajili yetu?”

“Katika kuumba upya,” Yesu anaahidi, “Mwana wa binadamu aketipo juu ya kiti chake kitukufu cha ufalme, nyinyi ambao mmenifuata mtaketi wenyewe pia juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.” Ndiyo, Yesu anaonyesha kwamba kutakuwako kuumba upya kwa hali zilizopo duniani ili mambo yawe kama yalivyokuwa katika bustani ya Edeni. Na Petro na wanafunzi wale wengine wataipokea thawabu ya kutawala pamoja na Kristo juu ya Paradiso hiyo ya duniani pote. Kwa uhakika, thawabu hiyo nzuri ajabu inastahiki kufanyiwa dhabihu yoyote!

Ingawa hivyo, hata sasa kuna thawabu fulani-fulani, kama vile Yesu anavyotaarifu kwa uthabiti: “Hakuna mmoja ambaye ameacha nyumba au akina ndugu au akina dada au mama au baba au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema ambaye hatapata mara mia sasa katika kipindi hiki cha wakati, nyumba na akina ndugu na akina dada na akina mama na watoto na mashamba, pamoja na minyanyaso, na katika mfumo wa mambo unaokuja uhai wa milele.”

Kama vile Yesu anavyoahidi, kokote ambako wanafunzi wake waenda ulimwenguni, wao wakiwa pamoja na Wakristo wenzao huona shangwe ya uhusiano wenye ukaribu na wenye thamani kubwa kuliko ule ambao wao huuonea shangwe wakiwa pamoja na washiriki wa jamaa ya kiasili. Yaonekana kwamba yule mtawala kijana tajiri anapoteza thawabu hii na hata ile ya uhai wa milele katika Ufalme wa kimbingu wa Mungu.

Baadaye Yesu aongezea hivi: “Hata hivyo, wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho wa kwanza.” Yeye amaanisha nini?

Amaanisha kwamba watu wengi walio “wa kwanza” katika kuona shangwe ya mapendeleo ya kidini, kama yule mtawala kijana tajiri, hawatauingia Ufalme. Watakuwa “wa mwisho.” Lakini wengi, kutia na wanafunzi wanyenyekevu wa Yesu, ambao hudharauliwa kwa kuonwa na Mafarisayo wenye kujihesabia uadilifu kuwa ni “wa mwisho”—kuwa ni watu wa dunia, au ‛am ha·’aʹrets—watakuwa “wa kwanza.” Kuwa kwao “wa kwanza” kwamaanisha watapokea pendeleo la kuwa watawala wenzi wa Kristo katika Ufalme. Marko 10:17-31; Mathayo 19:16-30; Luka 18:18-30, NW.

▪ Kwa wazi, yule mwanamume kijana tajiri ni mtawala wa aina gani?

▪ Kwa nini Yesu akataa kuitwa mwema?

▪ Tukio la mtawala kijana latoaje kielezi cha hatari ya kuwa tajiri?

▪ Yesu awaahidi wafuasi wake thawabu gani mbalimbali?

▪ Walio wa kwanza wanakuwaje wa mwisho, na wa mwisho wa kwanza?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki