Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be funzo 31 uku. 190-uku. 193 fu. 2
  • Kuwaheshimu Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwaheshimu Wengine
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Habari Zinazolingana
  • Mifano ya Hali za Kawaida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutumia Vizuri Vielelezo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kwa Nini Unapaswa Kuheshimu Mamlaka?
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Je, Wewe Ni wa Kwanza Katika Kuonyesha Heshima?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be funzo 31 uku. 190-uku. 193 fu. 2

SOMO LA 31

Kuwaheshimu Wengine

Unahitaji kufanya nini?

Unahitaji kuwajali wengine na kuwaonyesha staha.

Kwa nini ni muhimu?

Mkristo ana wajibu wa kuonyesha heshima, na sifa hii inaweza kuwafanya wengine wakubali kwa urahisi ujumbe wako wa Biblia.

MAANDIKO yanatuambia ‘tuheshimu watu wa namna zote’ na ‘tusiseme kwa ubaya juu ya yeyote.’ (1 Pet. 2:17; Tit. 3:2) Kwa kweli, kila mtu tunayekutana naye ‘amekuja kuwako “katika ufanani wa Mungu.”’ (Yak. 3:9) Kristo alikufa kwa ajili ya kila mtu. (Yn. 3:16) Na watu wote wanahitaji kusikia habari njema na kuzifuata ili waokolewe. (2 Pet. 3:9) Watu wengine wana sifa au mamlaka zinazostahili heshima ya kipekee.

Kwa nini watu wengine hujaribu kukataa kuonyesha heshima ambayo Biblia inatuhimiza tuonyeshe? Desturi za mahali zinaweza kudai uonyeshe wengine heshima kulingana na jamii yao, rangi, jinsia, afya, umri, utajiri, au cheo chao. Kuenea kwa ufisadi miongoni mwa maafisa wa umma kumefanya wengi wasiheshimu wenye mamlaka. Katika nchi fulani watu hawaridhiki kamwe na hali yao maishani, kwa sababu labda wanafanya kazi kwa saa nyingi sana ili wapate angalau riziki, na wamezingirwa na watu ambao hawana heshima. Vijana hukazwa na rafiki zao kujiunga na maasi dhidi ya walimu wasiopendwa na watu wengine wenye mamlaka. Watu wengi huathiriwa na vipindi vya televisheni vinavyoonyesha jinsi watoto wanavyowazidi akili na kuwaongoza wazazi wao. Tunahitaji kujitahidi sana ili kuzuia mawazo kama hayo ya kilimwengu yasiathiri maoni yetu juu ya wengine. Lakini tunapowaheshimu wengine, inakuwa rahisi kuzungumza nao.

Kuwafikia Wengine kwa Njia ya Heshima. Mtu anayefanya kazi ya kidini anapaswa kuonyesha heshima kwa kuvaa vizuri na kutenda inavyotakikana. Adabu hutofautiana kulingana na mahali. Wengine huona ni kukosa adabu kuzungumza na mtu ukiwa umevaa kofia au mkono ukiwa mfukoni. Lakini mahali pengine si vibaya kufanya hivyo. Fikiria hali za mahali ili usije ukawaudhi watu. Ukifanya hivyo, unaweza kuepuka mambo yanayoweza kukuzuia usitangaze habari njema kwa njia bora.

Ndivyo ilivyo na salamu, hasa tunaposalimu watu wenye umri mkubwa. Kwa ujumla, ni kukosa adabu kwa vijana kuwaita watu wazima kwa majina yao ya kwanza ila tu kama wameruhusiwa. Kuna sehemu nyingine ambazo watu wazima pia hawapaswi kuwaita wageni kwa majina ya kwanza. Pia lugha fulani hutumia neno la wingi “nyinyi” au maneno mengine kuonyesha heshima kwa mtu mwenye umri mkubwa au mwenye mamlaka.

Salamu Zenye Heshima. Katika vijiji fulani unapaswa kumsalimu mtu unayekutana naye, ama njiani au uingiapo katika nyumba. Salamu hizo zinaweza kuwa kuamkiana kidogo, tabasamu, kutikisa kichwa, au kuinua macho. Kutomsalimu mtu huonwa kuwa kukosa heshima.

Hata hivyo, wengine wanaweza kufikiri unawapuuza hata ingawa umewasalimu. Kwa nini? Kwa sababu wanaona huwajali. Ni kawaida kwa watu kutambulishwa kwa kasoro fulani za mwili. Mara nyingi watu wenye ulemavu fulani na magonjwa hupuuzwa. Lakini, Neno la Mungu linatuonyesha jinsi tunavyopaswa kuwapenda na kuwaheshimu watu kama hao. (Mt. 8:2, 3) Kwa kadiri fulani sisi sote tumeathiriwa na dhambi ya Adamu tuliyorithi. Je, unaweza kuona unaheshimiwa ikiwa nyakati zote wengine wanakutambulisha kwa kasoro zako? Ungefurahi kutambuliwa kwa sifa zako nyingi nzuri, sivyo?

Heshima inahusu pia kutambua ukichwa. Kuna sehemu ambazo ni lazima uzungumze kwanza na kichwa cha familia kabla ya kuzungumza na wengine katika nyumba hiyo. Ingawa tumeagizwa na Yehova tuhubiri na kufundisha, tunatambua kwamba wazazi ndio wamepewa mamlaka na Mungu ya kuwazoeza watoto wao, kuwatia nidhamu, na kuwaongoza. (Efe. 6:1-4) Basi, tunapozuru nyumba fulani, kwa kawaida ni vizuri kuomba kuzungumza na wazazi kabla ya kuzungumza zaidi na watoto.

Ni lazima tuwaheshimu wazee kwa sababu kuishi kwingi ni kuona mengi. (Ayu. 32:6, 7) Nchini Sri Lanka, dada mmoja kijana aliye painia alitambua jambo hilo na likamsaidia alipomtembelea mzee fulani. Kwanza yule mzee alikataa kumsikiliza, akisema: “Wewe mtoto unawezaje kunifundisha Biblia?” Lakini akajibu: “Kwa kweli, sikuja kukufundisha bali kukueleza jambo fulani ambalo nilijifunza. Jambo hilo limenifurahisha sana hivi kwamba niliona niwaeleze wengine.” Majibu yenye heshima ya painia huyo yaliamsha upendezi wa mzee. “Basi, niambie, ulijifunza nini?” yule mzee akauliza. “Nimejifunza jinsi ya kuishi milele,” painia akajibu. Mzee huyo akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Si wazee wote watadai waheshimiwe, lakini wengi watafurahi wakiheshimiwa.

Lakini, wengine wanaweza kuonyesha heshima kupita kiasi. Katika visiwa vya Pasifiki na kwingineko, Mashahidi wakitumia salamu za kidesturi zenye heshima wanapomfikia mkuu wa kijiji au mkuu wa kabila fulani, wanaweza kusikilizwa na kuruhusiwa kuzungumza na wakuu hao na raia. Lakini haifai wala si lazima kumsifu mtu kupita kiasi. (Mit. 29:5) Vilevile, lugha fulani inaweza kutumia majina ya heshima, lakini kuonyesha staha ya Kikristo si kutumia kupita kiasi majina hayo ya heshima.

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Heshima. Biblia inatuhimiza tufafanue tumaini letu “kwa tabia-pole na staha yenye kina kirefu.” (1 Pet. 3:15) Kwa hiyo, ingawa ni rahisi kumkosoa mtu mwingine, je, kweli inafaa kumkosoa kwa njia inayomkosesha heshima? Ingefaa kusikiliza kwa subira, na labda kuuliza sababu inayomfanya ahisi hivyo, kisha tufikirie maoni yake tunaposababu naye katika Maandiko, sivyo?

Tunapokuwa jukwaani tuwaonyeshe wasikilizaji heshima kama ile tunayomwonyesha mtu tunayezungumza naye ana kwa ana. Msemaji mwenye heshima hawachambui wasikilizaji vikali wala hasemi mambo kama: “Mnaweza kufuata shauri hili kama mnataka.” Kuzungumza kwa njia hiyo huvunja wengine moyo. Ni afadhali kuwaona wasikilizaji kuwa watu wanaompenda Yehova na wanaotaka kumtumikia. Tumwige Yesu na kuonyesha fadhili tunaposhughulika na wale ambao wanaweza kuwa dhaifu kiroho, wasio na uzoefu, au ambao hawafuati shauri la Biblia haraka.

Wasikilizaji hutambua kwamba msemaji anawaheshimu akizungumza kana kwamba yeye mwenyewe anahitaji kufuata Neno la Mungu zaidi. Kwa hiyo, inafaa kuepuka kutumia sana neno “wewe” unapotumia maandiko. Kwa mfano, ebu ona tofauti iliyoko kati ya swali hili, “Je, unajitahidi kadiri uwezavyo?” na sentensi hii “Ni vizuri kila mmoja wetu ajiulize: ‘Je, ninajitahidi kadiri niwezavyo?’” Jambo linalokaziwa na kila mojawapo ya maswali hayo ni lilelile, lakini swali la kwanza linadokeza kwamba msemaji hahusishwi na mazungumzo. Swali la pili linamtia moyo kila mtu, pamoja na msemaji, kuchunguza hali zake mwenyewe na makusudio yake.

Epuka kujaribu kuchekesha watu eti ili tu wapasue kicheko. Hiyo inafanya ujumbe wa Biblia usiheshimiwe. Ni kweli kwamba tunafurahia utumishi wetu kwa Mungu. Na kunaweza kuwa na sehemu fulani za hotuba zetu ambazo zinaweza kuchekesha. Lakini kufanya mambo mazito kuwa vichekesho hakumheshimu Mungu wala wasikilizaji.

Salamu zetu, adabu zetu, na usemi wetu nyakati zote na zionyeshe kwamba tunawaona wengine kwa njia ambayo Yehova ametufundisha.

JINSI YA KUFAULU

  • Tambua jinsi Yehova anavyowaona watu.

  • Tambua ukichwa, umri, na wenye mamlaka.

  • Waruhusu watu wakueleze maoni yao.

  • Elewa wasikilizaji.

MAZOEZI: Mfikirie mtu ambaye anakuzidi sana kwa umri au unayemzidi sana kwa umri. Fikiria jinsi unavyoweza kumfikia, jambo unaloweza kusema ili kuanzisha mazungumzo, na jambo la kufanya ili kumheshimu na kuheshimu maoni yake. Fanya vile umepanga.

Jinsi ninavyoweza kuonyesha heshima zaidi

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki