Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bh uku. 199-uku. 201 fu. 4
  • Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa
  • Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unabii wa Kimasihi Unathibitisha Kwamba Yesu Alikuwa Ndiye Masihi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kutabiri Kuhusu Masihi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Walimngoja Masihi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yesu Kristo—Ufunguo Uongozao Kwenye Ujuzi Juu ya Mungu
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
Pata Habari Zaidi
Biblia Inafundisha Nini Hasa?
bh uku. 199-uku. 201 fu. 4

NYONGEZA

Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa

ILI kutusaidia kumtambua Masihi, Yehova Mungu aliwaongoza manabii wengi wa Biblia waandike habari kuhusu kuzaliwa, huduma, na kifo cha Mkombozi aliyeahidiwa. Unabii wote huo wa Biblia ulitimizwa maishani mwa Yesu Kristo. Unabii huo ni sahihi sana na una habari kamili. Kwa mfano, hebu tuchunguze unabii mbalimbali uliotabiri kuzaliwa kwa Masihi na maisha yake ya utotoni.

Nabii Isaya alitabiri kwamba Masihi angetokea katika ukoo wa Mfalme Daudi. (Isaya 9:7) Kwa kweli, Yesu alizaliwa katika ukoo wa Daudi.—Mathayo 1:1, 6-17.

Mika, nabii mwingine wa Mungu alitabiri kwamba hatimaye mtoto huyo angekuwa mtawala na kwamba angezaliwa “Bethlehemu Efratha.” (Mika 5:2) Wakati ambapo Yesu alizaliwa, kulikuwa na miji miwili huko Israeli iliyokuwa ikiitwa Bethlehemu. Mji mmoja ulikuwa karibu na Nazareti, kaskazini mwa nchi hiyo, nao ule mwingine ulikuwa karibu na Yerusalemu huko Yuda. Mji wa Bethlehemu, uliokuwa karibu na Yerusalemu, ulikuwa ukiitwa Efratha zamani. Yesu alizaliwa katika mji huo, kama vile tu unabii ulivyokuwa umetabiri!—Mathayo 2:1.

Unabii mwingine wa Biblia ulitabiri kwamba Mwana wa Mungu angeitwa “kutoka Misri.” Mtoto huyo, Yesu, alipelekwa Misri. Alirudishwa kutoka huko baada ya kifo cha Herode, na hivyo, unabii huo ukatimia.—Hosea 11:1; Mathayo 2:15.

Katika chati yenye kichwa “Unabii Kumhusu Masihi,” maandiko yaliyoorodheshwa chini ya kichwa “Unabii” yanaeleza mambo mengi zaidi kumhusu Masihi. Tafadhali linganisha maandiko hayo na yale yaliyo chini ya kichwa “Utimizo.” Kufanya hivyo kutaimarisha zaidi imani yako katika ukweli wa Neno la Mungu.

Unapochunguza maandiko hayo kumbuka kwamba maandiko yenye unabii yaliandikwa mamia ya miaka kabla ya kuzaliwa kwa Yesu. Yesu alisema: “Mambo yote yaliyoandikwa katika sheria ya Musa na katika Manabii na Zaburi juu yangu lazima yatimizwe.” (Luka 24:44) Biblia inaonyesha wazi kwamba unabii huo ulitimia kabisa!

UNABII KUMHUSU MASIHI

TUKIO

UNABII

UTIMIZO

Azaliwa katika kabila la Yuda

Mwanzo 49:10

Luka 3:23-33

Azaliwa na bikira

Isaya 7:14

Mathayo 1:18-25

Mzao wa Mfalme Daudi

Isaya 9:7

Mathayo 1:1, 6-17

Yehova amtangaza kuwa Mwanawe

Zaburi 2:7

Mathayo 3:17

Akosa kuaminiwa

Isaya 53:1

Yohana 12:37, 38

Aingia Yerusalemu akiwa amepanda punda

Zekaria 9:9

Mathayo 21:1-9

Asalitiwa na mtu wa karibu

Zaburi 41:9

Yohana 13:18, 21-30

Asalitiwa kwa vipande 30 vya fedha

Zekaria 11:12

Mathayo 26:14-16

Akaa kimya mbele ya waliomshtaki

Isaya 53:7

Mathayo 27:11-14

Mavazi yake yapigiwa kura

Zaburi 22:18

Mathayo 27:35

Atukanwa akiwa kwenye mti wa mateso

Zaburi 22:7, 8

Mathayo 27:39-43

Hakuna mfupa wake uliovunjwa

Zaburi 34:20

Yohana 19:33, 36

Azikwa pamoja na matajiri

Isaya 53:9

Mathayo 27:57-60

Afufuliwa kabla ya mwili wake kuharibika

Zaburi 16:10

Matendo 2:24, 27

Akwezwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu

Zaburi 110:1

Matendo 7:56

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki