Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bh uku. 219-uku. 220
  • Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”
  • Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Habari Zinazolingana
  • Babiloni Mkubwa Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • “Tokeni Kati Yao”
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Babuloni Mkubwa—Kaanguka na Kuhukumiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kuomboleza na Kushangilia Mwisho wa Babuloni
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
Pata Habari Zaidi
Biblia Inafundisha Nini Hasa?
bh uku. 219-uku. 220

NYONGEZA

Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”

KITABU cha Ufunuo kina majina ambayo yana maana ya mfano. (Ufunuo 1:1) Kwa mfano, kinataja mwanamke ambaye jina “Babiloni Mkubwa” limeandikwa katika paji la uso wake. Kinasema kwamba mwanamke huyo ameketi juu ya “umati na mataifa.” (Ufunuo 17:1, 5, 15) Kwa kuwa hakuna mwanamke halisi anayeweza kufanya hivyo, lazima Babiloni Mkubwa awe mwanamke wa mfano. Kwa hiyo, kahaba huyo wa mfano anawakilisha nini?

Kwenye Ufunuo 17:18, mwanamke huyohuyo wa mfano anatajwa kuwa “lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.” Jina “jiji” linarejelea kikundi cha watu. Kwa kuwa ‘jiji hilo kubwa’ linaongoza “wafalme wa dunia,” lazima yule mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa awe shirika lenye uvutano ulimwenguni pote. Linaweza kuitwa milki ya ulimwengu. Milki ya aina gani? Ya kidini. Ona jinsi maandiko mengine katika kitabu cha Ufunuo yanavyotusaidia kufikia uamuzi huo.

Milki inaweza kuwa ya kisiasa, ya kibiashara, au ya kidini. Mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa si milki ya kisiasa kwa sababu Neno la Mungu linasema kwamba “wafalme wa dunia,” au wanasiasa wa ulimwengu huu, “walifanya uasherati” naye. Uasherati wake ni mapatano ambayo amefanya na watawala wa dunia na ndiyo sababu anaitwa “kahaba mkubwa.”—Ufunuo 17:1, 2; Yakobo 4:4.

Babiloni Mkubwa hawezi kuwa milki ya kibiashara kwa sababu “wanabiashara wa dunia,” watamlilia atakapoharibiwa. Isitoshe, wafalme na wanabiashara watamwangalia Babiloni Mkubwa wakiwa “mbali.” (Ufunuo 18:3, 9, 10, 15-17) Kwa hiyo, ni wazi kwamba Babiloni Mkubwa, si milki ya kisiasa wala ya kibiashara, bali ni milki ya kidini.

Hilo linathibitishwa na ile taarifa ya kwamba Babiloni Mkubwa anapotosha mataifa yote kwa ‘mazoea yake ya kuwasiliana na pepo.’ (Ufunuo 18:23) Kwa kuwa mazoea yote ya kuwasiliana na pepo hutokana na dini na roho waovu, haishangazi kwamba Biblia inamwita Babiloni Mkubwa “makao ya roho waovu.” (Ufunuo 18:2; Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Pia, milki hiyo inapinga vikali dini ya kweli, ikiwatesa “manabii” na “watakatifu.” (Ufunuo 18:24) Kwa kweli, Babiloni Mkubwa anachukia sana dini ya kweli hivi kwamba anawatesa kikatili na hata kuwaua “mashahidi wa Yesu.” (Ufunuo 17:6) Hivyo, ni wazi kwamba mwanamke huyo anayeitwa Babiloni Mkubwa anawakilisha milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo, inayotia ndani dini zote zinazompinga Yehova Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki