SEHEMU YA 4
Ingojee Siku ya Yehova kwa Shangwe
Yehova aliwatumia manabii wake kuonya kuhusu jambo ambalo lingetokea wakati ujao, yaani, kumwagwa kwa hasira yake. Lakini hatupaswi kumwona kuwa Mungu mwenye hasira. Yeye ‘huwashangilia watu wake kwa vilio vya furaha.’ Tunapotazamia siku yake kuu, tuna kila sababu ya ‘kushangilia na kufurahia kwa moyo wote.’ (Sefania 3:14, 17) Utaonyeshaje hivyo kwa matendo na mtazamo wako? Kwa nini ushukuru kwa sababu ya mambo unayojifunza katika vile vitabu 12 vya kinabii?