Wimbo Na. 28
Wimbo Mpya
Makala Iliyochapishwa
1. Mwimbie Mungu, wimbo mupya kwa furaha;
Tangaza matendo yote afanyayo.
Musifu yeye, Ndiye Mungu wa ushindi;
Anapohukumu, hutenda kwa haki.
(KORASI)
Imbeni!
Twimbe wimbo mupya.
Imbeni!
Yehova Mufalme.
2. Shangilieni, pigeni vigelegele;
Jina lake sifu, na kumutukuza.
Jiunge nasi, tumwimbie Bwana wetu,
Piga tarumbeta, kinubi na zeze.
(KORASI)
Imbeni!
Twimbe wimbo mupya.
Imbeni!
Yehova Mufalme.
3. Bahari navyo vilivyomo vimusifu,
Uumbaji wote umwimbie sifa.
Mito, vijito, vyote vipige makofi,
Milima, vilima, vimusifu Yeye.
(KORASI)
Imbeni!
Twimbe wimbo mupya.
Imbeni!
Yehova Mufalme.
(Ona pia Zab. 96:1; 149:1; Isa. 42:10.)