Wimbo Na. 53
Kufanya Kazi Pamoja kwa Umoja
Makala Iliyochapishwa
1. Katika zizi la Mungu.
Unabii watimia.
Kuna amani, umoja,
Na furaha tele.
Twapenda umoja;
Bila mizozo.
Katika kazi ya Mungu,
Kuna mengi ya kufanywa.
Tutumikie pamoja,
Ma’gizo tutii.
2. Tumwombe Yehova Mungu,
Tuwe na akili moja;
Upendo uongezeke;
Tuwe na amani.
Inaburudisha,
Inapendeza.
Na tuonyeshe undugu,
Mungu atupe amani.
Umoja wetu udumu,
Tutumikiapo.
(Ona pia Mika 2:12; Sef. 3:9; 1 Kor. 1:10.)