Wimbo Na. 126
Kazi Yetu ya Upendo
Makala Iliyochapishwa
1. Siku ya siku zote;
Ee, Yehova twaja kwako.
Umetuonyesha fadhili,
Tuseme nini!
Umebariki kazi,
Kazi zetu za upendo.
Sasa tuna jengo,
Twaona baraka zako.
(KORASI)
Ee, Yehova, Ni pendeleo,
Kulijenga jumba hili.
Twataka kukutumikia sikuzote,
Na kukusifu kwa yote.
2. Twaona tabasamu,
Tumepata marafiki!
Hatutasahau, la hasha,
hadi milele!
Roho yako, Ee, Bwana,
Imekuwa juu yetu.
Wastahili sifa;
Jina lako litukuzwe!
(KORASI)
Ee, Yehova, Ni pendeleo,
Kulijenga jumba hili.
Twataka kukutumikia sikuzote,
Na kukusifu kwa yote.
(Ona pia Zab. 116:1; 147:1; Rom. 15:6.)