Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 5 uku. 8
  • Mungu Ambariki Abrahamu na Familia Yake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Ambariki Abrahamu na Familia Yake
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Gharika Mpaka Kukombolewa Katika Misri
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yehova—“Mungu Anayetoa Amani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Mwanzo—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • “Je, Mimi Niko Mahali pa Mungu?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 5 uku. 8
Abrahamu akiwa ameshika kisu cha kuchinjia huku Isaka akiwa amelazwa juu ya madhabahu

SEHEMU YA 5

Mungu Ambariki Abrahamu na Familia Yake

Wazao wa Abrahamu wapata ufanisi. Mungu amlinda Yosefu nchini Misri

YEHOVA alijua kwamba kuna wakati ambapo mwana wake mpendwa atateseka na kufa. Unabii uliorekodiwa katika Mwanzo 3:15 ulidokeza hilo. Je, Mungu angeweza kuwasaidia wanadamu waelewe jinsi kifo cha mwana wake kingemhuzunisha? Biblia ina mfano halisi uliotokea. Mungu alimwagiza Abrahamu amtoe dhabihu Isaka mwana wake mpendwa.

Abrahamu alikuwa na imani kubwa. Kumbuka kwamba Mungu alikuwa ameahidi kwamba Mkombozi, au Uzao ulioahidiwa, angetokea katika ukoo wa Isaka. Akiwa na imani kwamba Mungu atamfufua Isaka ikihitajika, Abrahamu alikuwa tayari kutii na kumtoa mwana wake mwenyewe awe dhabihu. Lakini malaika wa Mungu akamzuia Abrahamu dakika ya mwisho. Akimsifu Abrahamu kwa nia yake ya kumtolea Mungu kitu kilichokuwa na thamani zaidi kwake, Mungu alirudia ahadi Yake aliyokuwa amemtolea.

Baadaye, Isaka alipata wana wawili, Esau na Yakobo. Tofauti na Esau, Yakobo alithamini mambo ya kiroho naye akathawabishwa. Mungu alibadili jina la Yakobo likawa Israeli, na wana 12 wa Israeli wakawa vichwa vya makabila ya Israeli. Lakini familia hiyo ilipataje kuwa taifa kubwa?

Mambo yalianza wakati ambapo wengi kati ya wana hao walianza kumwonea kijicho Yosefu, ndugu yao mdogo. Walimuuza utumwani, naye akapelekwa Misri. Hata hivyo Mungu alimbariki kijana huyo mwenye ujasiri. Ijapokuwa alikabili hali ngumu, Yosefu aliteuliwa na Farao, mtawala wa Misri, na kupewa mamlaka kubwa. Hilo lilitokea wakati barabara, kwa kuwa njaa kali ilimfanya Yakobo awatume baadhi ya wana wake waende Misri kununua vyakula—naye Yosefu ndiye aliyekuwa akisimamia ugawanyaji wa chakula! Baada ya kuungana tena na ndugu zake wenye toba, Yosefu aliwasamehe na kupanga familia nzima ihamie Misri. Walipewa eneo zuri sana, ambapo wangeweza kukaa na kupata ufanisi. Yosefu alielewa kwamba Mungu alikuwa ameelekeza mambo hivyo ili atimize ahadi Zake.

Yosefu ajitambulisha waziwazi mbele ya ndugu zake

Yakobo alimalizia maisha yake huko Misri, akiwa na familia yake iliyokuwa ikizidi kuongezeka. Alipokuwa akikaribia kufa, alitabiri kwamba Mkombozi, au Uzao ulioahidiwa, angekuwa Mtawala mwenye nguvu ambaye angezaliwa katika ukoo wa mwana wake Yuda. Kabla hajafa miaka kadhaa baadaye, Yosefu alitabiri kwamba siku moja, Mungu angeitoa familia ya Yakobo nchini Misri.

—Inatoka kwenye Mwanzo sura ya 20 hadi 50; Waebrania 11:17-22.

  • Mungu alimwagiza Abrahamu afanye nini, na hilo lingewasaidia wanadamu kuelewa nini?

  • Yosefu alifikaje Misri, na matokeo yalikuwa nini?

  • Yakobo alitabiri nini kabla ya kufa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki