Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 23 uku. 26
  • Habari Njema Yaenea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Njema Yaenea
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Piga Mbiu ya Ufalme wa Yehova kwa Ujasiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Uwe Jasiri​—Yehova Ni Msaidizi Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Kutetea Habari Njema Mbele ya Maofisa Wakuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • “Nisikilizeni Ninapojitetea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 23 uku. 26
Paulo akihubiri huko Athene

Sehemu ya 23

Habari Njema Yaenea

Paulo asafiri nchi kavu na baharini akihubiri

BAADA ya kuwa Mkristo, Paulo alitangaza kwa bidii habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu. Mtu huyo aliyekuwa mpinzani alikumbana na upinzani mkali mara nyingi. Mtume huyo mwenye bidii alisafiri sehemu mbalimbali akihubiri habari njema ya Ufalme ambao utatimiza kusudi la awali la Mungu kwa wanadamu.

Katika safari yake ya kwanza ya kuhubiri huko Listra, Paulo alimponya mwanamume aliyekuwa kilema tangu kuzaliwa. Umati ulianza kupaaza sauti kwamba Paulo na Barnaba, msafiri mwenzake ni miungu. Wanaume hao wawili walijaribu sana kuwazuia watu wasiwatolee dhabihu. Hata hivyo, baadaye umati huohuo ulichochewa na adui za Paulo, ukampiga kwa mawe na kumwacha akiwa mahututi. Paulo hakufa na baadaye alirudi katika jiji hilohilo kuwaimarisha wanafunzi kwa maneno ya kutia moyo.

Wakristo fulani Wayahudi walidai kwamba waamini wasio Wayahudi wanapaswa kutimiza matakwa fulani ya Sheria ya Musa. Paulo alikwenda Yerusalemu kwa mitume na wanaume wazee ili kuwasilisha tatizo hilo. Baada ya kuyachunguza Maandiko kwa makini na kwa mwongozo wa roho takatifu ya Mungu, wanaume hao waliyaandikia makutaniko na kuyashauri yajiepushe na ibada ya sanamu, kula damu na nyama zenye damu, na kuepuka uasherati. Amri hizo zilikuwa za “lazima,” hata hivyo, haikumaanisha kwamba walipaswa kufuata Sheria ya Musa.—Mdo. 15:28, 29.

Katika safari yake ya pili ya kuhubiri, Paulo alienda Beroya, eneo ambalo leo liko Ugiriki. Wayahudi waliokuwa wakiishi huko walilipokea neno kwa hamu, wakiyachunguza Maandiko kila siku ili kuyathibitisha mafundisho yake. Kwa mara nyingine tena, upinzani ukamfanya aondoke na kwenda Athene. Akiwa mbele ya Waathene wenye elimu, Paulo alitoa hotuba yenye kuchochea kwelikweli. Leo tunaweza kumwiga Paulo kwa kusema kwa busara, utambuzi, na ufasaha tunapohubiri.

Baada ya safari yake ya tatu ya kuhubiri, Paulo alienda Yerusalemu. Alipoenda hekaluni, Wayahudi fulani walizusha ghasia, wakitaka kumuua. Askari-jeshi Waroma wakaingilia kati na kumhoji Paulo. Kwa kuwa alikuwa raia wa Roma, baadaye alijitetea mbele ya Feliksi, gavana Mroma. Wayahudi hawakuwa na uthibitisho wowote kuhusu mashtaka yao dhidi ya Paulo. Ili kumzuia Festo, aliyekuwa pia gavana Mroma, asimtie mikononi mwa Wayahudi, Paulo alisema: “Ninakata rufani kwa Kaisari!” Festo akajibu: “Utaenda kwa Kaisari.”—Mdo. 25:11, 12

Wanajeshi wa Roma wakimsaidia Paulo kuutoroka umati wenye hasira

Kisha Paulo akasafirishwa kwa meli hadi Italia ili akahukumiwe. Baada ya meli yao kuvunjika, alilazimika kukaa katika kisiwa cha Malta wakati wa majira ya baridi kali. Mwishowe alipofika Roma, alikaa katika nyumba ya kukodi kwa miaka miwili. Hata ingawa alikuwa akilindwa na askari, mtume huyo mwenye bidii aliendelea kuwahubiria wote waliomtembelea kuhusu Ufalme wa Mungu.

—Inatoka kwenye Matendo 11:22–28:31.

  • Ni nini kilichotokea baada ya Paulo kumponya mtu aliyekuwa kilema jijini Listra?

  • Swali kuhusu kufuata Sheria ya Musa lilitatuliwaje?

  • Paulo alifika Roma jinsi gani, naye alifanya nini huko?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki