Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rk seh. ya 7 kur. 18-19
  • Mambo Ambayo Mungu Aliahidi Kupitia Manabii

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Ambayo Mungu Aliahidi Kupitia Manabii
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Habari Zinazolingana
  • Upatano wa Biblia Yote
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Ainabinadamu?
    Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
  • Mpango wa Mungu wa Kuwakomboa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
rk seh. ya 7 kur. 18-19

Sehemu ya 7

Mambo Ambayo Mungu Aliahidi Kupitia Manabii

MANABII wa kale walimwamini Mungu. Waliamini ahadi zake na kuishi kulingana nazo. Ahadi hizo zilitia ndani nini?

Mara baada ya Adamu na Hawa kuasi katika Edeni, Mungu aliahidi kwamba angemchagua mtu ambaye angeponda kichwa cha “nyoka” anayewakilisha “yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani,” na kumharibu milele. (Mwanzo 3:14, 15; Ufunuo 12:9, 12) Mtu huyo angethibitika kuwa nani?

Miaka 2,000 baada ya kutoa unabii huo, Yehova alimwahidi nabii Abrahamu kwamba Yule Anayekuja angetokana na uzao wake. Mungu alimwambia Abrahamu: “Kupitia kwa uzao wako mataifa yote ya dunia hakika yatajibariki kwa sababu wewe umeisikiliza sauti yangu.”—Mwanzo 22:18.

Mnamo 1473 K.W.K., Mungu alimpa nabii Musa habari zaidi kuhusu “uzao” huo. Musa aliwaambia wana wa Israeli: “Nabii kutoka katikati yako mwenyewe, kutoka kwa ndugu zako, kama mimi, ndiye ambaye Yehova Mungu wako atakuinulia—ninyi mnapaswa kumsikiliza yeye.” (Kumbukumbu la Torati 18:15) Kama Musa, nabii huyo anayekuja angetoka miongoni mwa wana wa Abrahamu.

Pia, nabii huyo angekuwa mzao wa Mfalme Daudi naye angekuwa mfalme mkuu. Mungu alimwahidi Mfalme Daudi: ‘Nitainua uzao wako baada yako, ambao utatoka ndani ya viuno vyako; nami kwa kweli nitaufanya imara ufalme wake.’ (2 Samweli 7:12, 13) Mungu pia alifunua kwamba mzao huyo wa Daudi ataitwa “Mkuu wa Amani,” akaongeza: “Hakutakuwa na mwisho kwa habari ya wingi wa huo utawala wa kifalme na kwa amani, juu ya kiti cha ufalme cha Daudi na juu ya ufalme wake ili kuufanya imara na kuutegemeza kwa njia ya haki na kwa njia ya uadilifu, kuanzia sasa na kuendelea mpaka wakati usio na kipimo.” (Isaya 9:6, 7) Ndiyo, Kiongozi huyo mwadilifu atairudisha amani na haki ulimwenguni pote. Lakini angetokea wakati gani?

Abrahamu, Musa,Daudi, Yesu, na uzao ulioahidiwa ungemponda nyoka kichwa

“Uzao” ulioahidiwa . . . ungetokana na uzao wa Abrahamu, ungekuwa nabii kama Musa, ungetokana na ukoo wa Daudi, ungetokea mwaka wa 29 W. K., ungemponda nyoka, Shetani

Baadaye malaika Gabrieli alimwambia hivi nabii wa Mungu, Danieli: “Nawe ujue na ufahamu kwamba tangu kutolewa kwa lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi, kutakuwa na majuma 7, pia majuma 62.” (Danieli 9:25) Hayo yalikuwa majuma 69 ya miaka—kila juma likiwa na miaka 7—ambayo jumla yake ni miaka 483. Ilianza mwaka wa 455 K.W.K. mpaka mwaka wa 29 W.K.a

Je, kweli Masihi, nabii aliye kama Musa na ambaye ni “uzao” uliosubiriwa kwa muda mrefu, alikuja mwaka wa 29 W.K.? Acheni tuone.

a Ona ukurasa wa 197-199 wa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Ungejibu Namna Gani?

  • “Uzao” ulioahidiwa wa Abrahamu utamfanya nini Shetani?

  • Mungu aliahidi nini kupitia Musa?

  • Daudi alijifunza nini kuhusu “uzao”?

  • Malaika Gabrieli alimwambia nini Danieli?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki