Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ll seh. ya 8 kur. 18-19
  • Kifo cha Yesu Kina Maana Gani Kwako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kifo cha Yesu Kina Maana Gani Kwako?
  • Msikilize Mungu Uishi Milele
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu ya 8
    Msikilize Mungu
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Kristo—Alitumwa na Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Msikilize Mungu Uishi Milele
ll seh. ya 8 kur. 18-19

SEHEMU YA 8

Kifo cha Yesu Kina Maana Gani Kwako?

Yesu alikufa ili tuweze kuishi. Yohana 3:16

Wanawake wanalitazama kaburi la Yesu lililo tupu

Siku tatu baada ya Yesu kufa, wanawake fulani walienda kwenye kaburi lake na kulipata likiwa tupu. Yehova alikuwa amemfufua Yesu.

Yesu anawatokea mitume wake kisha anapaa mbinguni

Baadaye, Yesu aliwatokea mitume wake.

Ndiyo, Yehova alimfufua Yesu akiwa kiumbe wa roho mwenye nguvu, na asiyeweza kufa. Wanafunzi wa Yesu walimwona akipaa kwenda mbinguni.

  • “Mshahara” wa dhambi ni nini?​—Waroma 6:23.

  • Yesu alifungua njia ya kupata uzima wa milele.​—Waroma 5:21.

Mungu alimfufua Yesu na kumfanya awe Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Danieli 7:13, 14

Akiwa kwenye kiti chake katika Ufalme, Yesu anawatawala watu walio katika paradiso duniani

Yesu alitoa uhai wake ili kulipa fidia kwa ajili ya wanadamu. (Mathayo 20:28) Hivyo, kupitia fidia hiyo Mungu anafanya iwezekane kwetu kuishi milele.

Yehova alimchagua Yesu kuwa Mfalme juu ya dunia. Atatawala pamoja na watu waaminifu 144,000, ambao wanafufuliwa kutoka duniani na kwenda kuishi mbinguni. Yesu na hao 144,000 wanafanyiza serikali ya kimbingu yenye uadilifu, yaani, Ufalme wa Mungu.—Ufunuo 14:1-3.

Ufalme wa Mungu utaifanya dunia kuwa paradiso. Hakutakuwa tena na vita, uhalifu, umaskini, na njaa. Watu watakuwa na furaha kwelikweli.—Zaburi 145:16.

  • Ufalme wa Mungu utaleta baraka gani?​—Zaburi 72.

  • Tunapaswa kusali Ufalme wa Mungu uje.​—Mathayo 6:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki