Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yc somo la 3 kur. 8-9
  • Rahabu alimwamini Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Rahabu alimwamini Yehova
  • Wafundishe Watoto Wako
  • Habari Zinazolingana
  • Rahabu Alisikiliza Habari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Rahabu Awaficha Wapelelezi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • ‘Alitangazwa Kuwa Mwadilifu kwa Matendo’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Rahabu—Atangazwa Kuwa Mwadilifu kwa Matendo ya Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Wafundishe Watoto Wako
yc somo la 3 kur. 8-9
Rahabu aenda darini walipojificha wapelelezi

SOMO LA 3

Rahabu Alimwamini Yehova

Sasa ngoja tuwazie tupo ndani ya jiji la Yeriko. Jiji hili liko katika nchi ya Kanaani. Mahali hapa watu hawamwamini Yehova. Mwanamke anayeitwa Rahabu anaishi katika jiji hili.

Rahabu alipokuwa msichana mdogo, alisikia hadithi kuhusu jinsi Musa alivyoyatenganisha maji ya Bahari Nyekundu na kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri. Pia, alisikia jinsi ambavyo Yehova aliwasaidia Waisraeli washinde vita dhidi ya maadui zao. Sasa anasikia kwamba Waisraeli wamepiga kambi karibu na Yeriko!

Rahabu aliwaficha wapelelezi kwa sababu alimwamini Yehova

Jioni moja, Waisraeli wawili wanaingia Yeriko ili kulipeleleza jiji. Wanafika kwenye nyumba ya Rahabu. Naye anawakaribisha ndani ili walale. Usiku, mfalme wa Yeriko anagundua kwamba wapelelezi wako ndani ya jiji na wameenda nyumbani kwa Rahabu. Kwa hiyo, mfalme anawatuma watu ili wakawakamate. Rahabu anawaficha wapelelezi hao darini na anawaambia watu waliotumwa na mfalme: ‘Wapelelezi hao walikuwa hapa, lakini tayari wameondoka jijini. Ikiwa mtawafuata sasa, mnaweza kuwakamata!’ Je, unajua kwa nini Rahabu anawaficha wapelelezi hao?— Kwa sababu anamwamini Yehova na anajua kwamba atawapa Waisraeli nchi ya Kanaani.

Kabla wapelelezi hawajaondoka kwenye nyumba ya Rahabu, waliahidi kwamba Rahabu na familia yake hawataharibiwa wakati jiji la Yeriko litakapoharibiwa. Je, unajua wanamwambia afanye nini?— Wanamwambia hivi: ‘Chukua kamba hii nyekundu, na uining’inize nje ya dirisha lako. Ikiwa utafanya hivyo, kila mtu aliye nyumbani mwako atakuwa salama.’ Rahabu anafanya kila kitu ambacho wale wapelelezi walimwambia afanye. Je, unajua kilichotokea baadaye?—

Ile kamba nyekundu yaning’inia dirishani kwa Rahabu, kwenye ukuta wa Yeriko

Yehova alimwokoa Rahabu na familia yake

Siku chache baadaye, Waisraeli wanalizunguka jiji kimyakimya. Kwa siku sita wanalizunguka jiji mara moja kwa siku. Lakini katika siku ya saba, wanalizunguka jiji mara saba. Kisha wote wanapaaza sauti kubwa. Yehova anaziangusha kuta za jiji. Lakini nyumba ambayo kamba nyekundu inaning’inia dirishani haianguki! Je, unaiona nyumba hiyo?— Rahabu na familia yake wako salama!

Unajifunza nini kutoka kwa Rahabu?— Rahabu alimwamini Yehova kwa sababu ya mambo yote mazuri ambayo alikuwa amejifunza kumhusu. Wewe pia unajifunza mambo mengi mazuri kuhusu Yehova. Je, unamwamini Yehova kama Rahabu alivyomwamini?— Tunajua kwamba unamwamini!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Yoshua 2:1-24; 6:1-5, 14, 15, 20-25

  • Waebrania 11:31

MASWALI:

  • Rahabu alisikia hadithi gani alipokuwa msichana mdogo?

  • Rahabu aliwasaidiaje wapelelezi Waisraeli? Kwa nini aliwasaidia?

  • Wapelelezi walimwahidi nini Rahabu?

  • Unajifunza nini kutoka kwa Rahabu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki