Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yc somo la 7 kur. 16-17
  • Je, wakati fulani unajihisi mpweke na kuogopa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, wakati fulani unajihisi mpweke na kuogopa?
  • Wafundishe Watoto Wako
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Kuna Wakati Unapojihisi Mpweke na Mwenye Woga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je, Utakuwa Mwaminifu Kama Eliya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Wafundishe Watoto Wako
yc somo la 7 kur. 16-17
Mvulana mpweke, mwenye woga

SOMO LA 7

Je, Wakati Fulani Unajihisi Mpweke na Kuogopa?

Hebu mwangalie mvulana huyu mdogo kwenye picha hii. Anaonekana ni mpweke na anaogopa, sivyo? Je, umewahi kuhisi hivyo?— Kila mtu huhisi hivyo nyakati fulani. Biblia inazungumza kuhusu marafiki wa Yehova ambao walihisi upweke na kuogopa. Mmoja wao ni Eliya. Acha tujifunze kumhusu.

Malkia Yezebeli akizungumza kwa hasira

Yezebeli alitaka kumuua Eliya

Eliya aliishi Israeli miaka mingi iliyopita, kabla Yesu hajazaliwa. Mfalme wa Israeli, Ahabu, hakuwa akimwabudu Mungu wa kweli, Yehova. Ahabu na mke wake, Yezebeli, walikuwa wakimwabudu mungu wa uwongo Baali. Hivyo, watu wengi nchini Israeli wakaanza kumwabudu Baali. Malkia Yezebeli alikuwa mkatili sana na alitaka kuwaua watu wote waliokuwa wakimwabudu Yehova, kutia ndani Eliya! Je, unajua Eliya alifanya nini?—

Eliya alikimbia! Alienda mbali jangwani na kujificha ndani ya pango. Unafikiri kwa nini alifanya hivyo?— Naam, aliogopa. Lakini Eliya hakupaswa kuogopa. Kwa nini? Kwa sababu alijua kwamba Yehova angeweza kumsaidia. Kabla ya tukio hilo, Yehova alikuwa amemwonyesha Eliya nguvu zake. Wakati fulani, Yehova alijibu sala ya Eliya kwa kutuma moto kutoka mbinguni. Kwa hiyo, Yehova angeweza kumsaidia Eliya wakati huu pia!

Yehova ajibu sala ya Eliya kwa kutuma moto kutoka mbinguni; Eliya akiwa pangoni; Eliya akiwa na furaha baada ya kusikia maneno ya Yehova yenye kutia moyo

Yehova alimsaidiaje Eliya?

Eliya alipokuwa ndani ya pango, Yehova alizungumza naye na kumuuliza: ‘Unafanya nini hapa?’ Eliya akajibu: ‘Mimi tu ndiye niliyebaki ninayeendelea kukuabudu. Nimebaki peke yangu, na ninaogopa kwamba nitauawa.’ Eliya alifikiri kwamba waabudu wengine wote wa Yehova wameuawa. Lakini Yehova akamwambia Eliya: ‘Hapana, si kweli. Bado kuna watu wengine elfu saba ambao wananiabudu. Uwe jasiri. Bado una kazi nyingi ya kufanya!’ Je, unafikiri Eliya alifurahi kusikia hivyo?—

Unaweza kujifunza nini kutokana na yale yaliyompata Eliya?— Hupaswi kujihisi mpweke na kuogopa. Una marafiki ambao wanampenda Yehova na wanakupenda pia. Jambo lingine ni kwamba, Yehova ana nguvu nyingi sana, na nyakati zote atakusaidia! Je, umefurahi kujua kwamba kwa kweli wewe si mpweke?—

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 1 Wafalme 19:3-18

  • Zaburi 145:18

  • 1 Petro 5:9

MASWALI:

  • Je, watu wote Israeli walimwabudu Yehova katika siku za Eliya? Walimwabudu nani?

  • Kwa nini Eliya alikimbia na kujificha ndani ya pango?

  • Yehova alimwambia nini Eliya?

  • Tunaweza kujifunza nini kutokana na yale yaliyompata Eliya?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki