Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hf seh. ya 2 kur. 6-8
  • Uwe Mshikamanifu kwa Mwenzi Wako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mshikamanifu kwa Mwenzi Wako
  • Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1 TANGULIZA NDOA YAKO
  • 2 LINDA MOYO WAKO
  • Fuata Mwongozo wa Mungu ili Uwe na Ndoa Yenye Furaha
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Baada ya Siku ya Harusi
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Wajibika Sikuzote Katika Ndoa Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Mtendee Mwenzi Wako wa Ndoa kwa Heshima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
hf seh. ya 2 kur. 6-8
Mume akimfunika mke wake kwa mwamvuli anapomsaidia kuingia kwenye gari

SEHEMU YA 2

Uwe Mshikamanifu kwa Mwenzi Wako

“Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”​—Marko 10:9

Yehova anataka ‘tupende fadhili.’ (Mika 6:8) Kulingana na Biblia neno fadhili linamaanisha upendo unaofanya vitu au watu wawili washikamane. Hilo ni jambo muhimu katika ndoa kwa sababu ushikamanifu unahitajiwa ili watu waaminiane na kupendana.

Leo, watu wengi si washikamanifu kwa wenzi wao. Ili kuilinda ndoa yako, unapaswa kuazimia kufanya mambo mawili.

1 TANGULIZA NDOA YAKO

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Ndoa yako ni moja kati ya mambo ya maana zaidi maishani mwako. Hivyo, inapaswa kutangulizwa.

Yehova anataka umkazie fikira mwenzi wako na ‘mfurahie maisha’ pamoja. (Mhubiri 9:9) Anaonyesha waziwazi kwamba hupaswi kamwe kumpuuza mwenzi wako, badala yake, mnapaswa kutafuta njia za kufurahishana. (1 Wakorintho 10:24) Mwonyeshe mwenzi wako kwamba unamhitaji na unamthamini.

Mume akimletea mke wake kikombe cha kahawa; mume anarudi nyumbani na kumkuta mke akipika chakula

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Hakikisha kwamba unatumia wakati wa kutosha pamoja na mwenzi wako na umsikilize kwa makini

  • Usijifikirie mwenyewe tu

Mume na mke wakiwa kwenye tafrija

2 LINDA MOYO WAKO

BIBLIA INASEMA HIVI: “Kila mtu ambaye anaendelea kumtazama mwanamke na kumtamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.” (Mathayo 5:28) Hivyo, mtu akiendelea kufikiria mambo machafu kiadili anakosa kuwa mwaminifu kwa mwenzi wake wa ndoa.

Yehova anasema kwamba unapaswa ‘kuulinda moyo wako.’ (Methali 4:23; Yeremia 17:9) Ili kufanya hivyo, unapaswa kudhibiti macho yako. (Mathayo 5:29, 30) Fuata mfano wa mzee wa ukoo Ayubu, ambaye alifanya agano na macho yake ili asimtazame mwanamke mwingine kwa tamaa. (Ayubu 31:1) Azimia kabisa kutotazama ponografia. Epuka uhusiano wowote wa kimapenzi na mtu ambaye si mwenzi wako wa ndoa.

Mume akiwa na picha ya mke wake kwenye meza yake kazini

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Onyesha wazi kwamba wewe ni mshikamanifu kabisa kwa mwenzi wako

  • Fikiria hisia za mwenzi wako na ukatishe mara moja uhusiano wowote unaoweza kumuumiza

TIMIZA SEHEMU YAKO

Uwe mnyoofu na utambue udhaifu wako. (Zaburi 15:2) Usiaibike kuomba msaada. (Methali 1:5) Ikiwa una mawazo yasiyofaa, endelea kupambana. Usife moyo. (Methali 24:16) Yehova atakubariki ukijitahidi kubaki mshikamanifu kwa mwenzi wako.

JIULIZE . . .

  • Ninawezaje kutumia wakati mwingi zaidi pamoja na mwenzi wangu?

  • Je, mwenzi wangu ndiye rafiki yangu wa karibu zaidi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki