Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • od kur. 4-5
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Akina Ndugu—Pandeni kwa Roho na Mjitahidi Kufikia Mapendeleo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Tumepangwa Kitengenezo Kulingana na Kitabu cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Kondoo wa Yehova Wahitaji Utunzaji Mwororo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Ndugu Vijana, Je, Mnajitahidi Kufikia Mapendeleo?
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
od kur. 4-5

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Wahubiri Wenzetu Wapendwa wa Habari Njema:

Ni pendeleo kubwa sana kuungana katika ibada ya Mungu pekee wa kweli, Yehova! Sisi ni “wafanyakazi wenzi wa Mungu,” na tumekabidhiwa kazi takatifu inayookoa uhai ya kuhubiri na kufundisha habari njema ya Ufalme wake uliosimamishwa. (1 Kor. 3:9; Mt. 28:19, 20) Ili tutimize kazi hiyo ya ulimwenguni pote kwa amani na umoja, ni lazima tufuate utaratibu mzuri.—1 Kor. 14:40.

Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa jinsi kutaniko la Kikristo linavyofanya kazi leo. Kinazungumzia mapendeleo na wajibu wako ukiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Ukithamini mapendeleo yako na kutimiza wajibu wako, ‘utaimarishwa katika imani.’—Mdo. 16:4, 5; Gal. 6:5.

Kwa hiyo, tunakutia moyo usome kitabu hiki kwa makini. Fikiria jinsi unavyoweza kutumia habari hizo maishani mwako. Kwa mfano, ikiwa umeanza kuhubiri na kutaniko hivi karibuni, unapaswa kuchukua hatua gani ili ubatizwe na kuwa Shahidi wa Yehova? Kwa upande mwingine, ikiwa umebatizwa, unaweza kufanya nini ili ukue kiroho na kupanua utumishi wako kwa Yehova? (1 Tim. 4:15) Ni kwa njia gani unaweza kuchangia amani kutanikoni? (2 Kor. 13:11) Tafuta majibu ya maswali hayo katika kitabu hiki.

Ikiwa wewe ni mwanamume uliyebatizwa, unaweza kufanya nini ili ustahili kuwa mtumishi wa huduma na baadaye mzee wa kutaniko? Kadiri maelfu ya wapya wanavyoendelea kumiminika katika tengenezo la Mungu, ndivyo kunavyokuwa na uhitaji mkubwa wa ndugu wanaostahili kuongoza. Kitabu hiki kitakusaidia kuelewa mambo yanayohusika ili ‘ujitahidi’ kufikia mapendeleo hayo ya kiroho.—1 Tim. 3:1.

Tunasali kwa dhati kwamba kitabu hiki kitakusaidia kutambua sehemu yako katika mpango wa Yehova na kuithamini. Tunawapenda sana ninyi nyote na tunaendelea kusali kwamba mtakuwa miongoni mwa wale ambao wataendelea kushangilia milele katika kumwabudu Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Zab. 37:10, 11; Isa. 65:21-25.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki