Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 4 uku. 16-uku. 17 fu. 2
  • Hasira Yasababisha Mauaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hasira Yasababisha Mauaji
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ndugu Waliositawisha Mitazamo Tofauti
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Mwana Mzuri na Mbaya
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Kumtolea Yehova Dhabihu Zenye Kukubalika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 4 uku. 16-uku. 17 fu. 2
Kaini anakasirika Abeli anapomtolea Yehova dhabihu

SOMO LA 4

Hasira Yasababisha Mauaji

Baada ya Adamu na Hawa kufukuzwa katika bustani ya Edeni, walizaa watoto wengi. Mtoto wa kwanza aliitwa Kaini, naye alikuwa mkulima, na mtoto wa pili, Abeli, alikuwa mchungaji wa wanyama.

Siku moja Kaini na Abeli walimtolea Yehova dhabihu. Je, unajua dhabihu ni nini? Ni zawadi ya pekee. Yehova alifurahishwa na dhabihu ya Abeli, lakini alichukizwa na dhabihu ya Kaini. Jambo hilo lilimkasirisha sana Kaini. Yehova alimwonya Kaini kwamba hasira ingeweza kusababisha afanye jambo baya. Hata hivyo, Kaini hakusikiliza.

Badala yake Kaini alimwambia Abeli hivi: ‘Twende shambani.’ Walipokuwa peke yao shambani, Kaini alimshambulia ndugu yake na kumuua. Yehova angefanya nini kuhusu jambo hilo? Yehova alimwadhibu Kaini kwa kumfukuza aende mbali na familia yao. Kaini hakuruhusiwa kurudi tena nyumbani.

Kaini anamkaribia Abeli wakiwa shambani

Tunajifunza nini? Tunajifunza kwamba tunaweza kukasirika mambo yanapoenda kinyume na matarajio yetu. Tunapoona kwamba tumeanza kukasirika—au tunapoonywa na wengine kuhusu hasira—tunapaswa kukubali kurekebishwa na kujitahidi kudhibiti hisia hizo kabla hazijaanza kututawala.

Kwa sababu Abeli alimpenda Yehova na alifanya mambo mema, sikuzote Yehova atamkumbuka. Mungu atamfufua Abeli wakati atakapoifanya dunia kuwa paradiso.

“Kwanza fanya amani na ndugu yako, kisha urudi na kutoa zawadi yako.”​—Mathayo 5:24

Maswali: Watoto wawili wa kwanza wa Adamu na Hawa walikuwa nani? Kwa nini Kaini alimuua ndugu yake?

Mwanzo 4:1-12; Waebrania 11:4; 1 Yohana 3:11, 12

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki