Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 8 uku. 26-uku. 27 fu. 1
  • Abrahamu na Sara Walimtii Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Abrahamu na Sara Walimtii Mungu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Abrahamu Alikuwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ibrahimu—Rafiki ya Mungu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Unaweza Kuiga Imani ya Abrahamu na Sara!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Yehova Alimwita “Rafiki Yangu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 8 uku. 26-uku. 27 fu. 1
Abrahamu na Sara wakifungasha mizigo yao ili kuondoka Uru

SOMO LA 8

Abrahamu na Sara Walimtii Mungu

Jiji la Uru lilikuwa jirani na mji wa Babeli, ambako watu waliabudu miungu mingine tofauti na Yehova. Lakini kulikuwa na mwanamume mmoja aliyeishi katika jiji la Uru, ambaye alimwabudu Yehova pekee. Mwanamume huyo aliitwa Abrahamu.

Yehova alimwambia Abrahamu hivi: ‘Nenda utoke katika nchi yako na kutoka kwa watu wa jamaa yako, mpaka katika nchi ambayo nitakuonyesha.’ Kisha Mungu akamwahidi hivi: ‘Nami nitakufanya uwe taifa kubwa, nitawafanyia watu mambo mazuri katika dunia yote kwa sababu yako.’

Ingawa Abrahamu hakujua mahali alikokuwa akienda, alimtumaini Yehova. Kwa hiyo Abrahamu na Sara mke wake, Tera baba yake, na Loti mpwa wake walitii, wakachukua mizigo yao na kuanza safari ndefu.

Abrahamu alikuwa na umri wa miaka 75, yeye na familia yake walipofika katika nchi ambayo Yehova alitaka kuwaonyesha. Nchi hiyo iliitwa Kanaani. Mungu alizungumza na Abrahamu na kumwahidi hivi: ‘Nitaupa uzao wako nchi hii.’ Lakini Abrahamu na Sara walikuwa wazee sana na hawakuwa na mtoto. Kwa hiyo Yehova angetimiza ahadi hiyo jinsi gani?

Abrahamu na familia yake wakisafiri kuelekea nchi ya Kanaani

“Kwa imani, Abrahamu . . . alitii kwa kutoka na kwenda mahali ambapo angepokea kuwa urithi; aliondoka, ingawa hakujua mahali alipokuwa akienda.”​—Waebrania 11:8

Maswali: Yehova alimwambia Abrahamu afanye nini? Yehova alimwahidi Abrahamu nini?

Mwanzo 11:29–12:9; Matendo 7:2-4; Wagalatia 3:6; Waebrania 11:8

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki