Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 64 uku. 152-uku. 153 fu. 4
  • Danieli Ndani ya Shimo la Simba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Danieli Ndani ya Shimo la Simba
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Danieli Katika Shimo la Simba
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Aokolewa Asiliwe na Simba!
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Danieli Alimtumikia Mungu kwa Udumifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Dario—Mfalme Mwenye Haki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 64 uku. 152-uku. 153 fu. 4
Wanaume wenye wivu wanamkuta Danieli akisali mbele ya dirisha lililo wazi

SOMO LA 64

Danieli Ndani ya Shimo la Simba

Mfalme mwingine wa Babiloni alikuwa Dario Mmedi. Dario alitambua kwamba Danieli alikuwa mwanamume wa pekee. Akampa Danieli mamlaka juu ya wanaume wengine wote wenye mamlaka nchini. Wanaume hao walimwonea wivu Danieli nao wakataka kumuua. Walijua kwamba Danieli alisali kwa Yehova mara tatu kila siku, hivyo wakamwambia Dario hivi: ‘Ee mfalme, kunapaswa kuwa na sheria kwamba kila mtu asali kwako pekee. Yeyote atakayekosa kutii sheria hiyo anapaswa kutupwa ndani ya shimo lenye simba wengi.’ Dario alifurahishwa na wazo hilo, hivyo akatia sahihi sheria hiyo.

Mara tu Danieli aliposikia kuhusu sheria hiyo mpya, alienda nyumbani kwake. Akapiga magoti mbele ya dirisha lake lililokuwa wazi, na kusali kwa Yehova. Wale wanaume wenye wivu wakaingia kwa kishindo ndani ya nyumba ya Danieli na kumkuta akisali. Wakakimbia kwenda kwa Dario na kumwambia hivi: ‘Danieli hakutii. Anasali kwa Mungu wake mara tatu kila siku.’ Dario alimpenda Danieli, naye hakutaka afe. Mchana kutwa akawa anafikiria jinsi atakavyomwokoa Danieli. Lakini hata mfalme mwenyewe hangeweza kubadili sheria ambayo tayari alikuwa ametia sahihi. Alilazimika kuwaamuru watu wake wamtupe Danieli ndani ya shimo lenye simba wakali.

Usiku huo, Dario alikuwa na wasiwasi sana kumhusu Danieli hivi kwamba hakuweza kupata usingizi. Asubuhi ilipofikia, akakimbia kwenda kwenye shimo la simba na kumuuliza hivi Danieli: ‘Je, Mungu wako alikuokoa?’

Dario akasikia sauti. Ilikuwa sauti ya Danieli! Akamjibu hivi Dario: ‘Malaika wa Yehova alifunga vinywa vya simba. Hawakunidhuru hata kidogo.’ Dario alifurahi sana! Akaagiza kwamba Danieli atolewe kwenye shimo. Danieli hakuwa hata na mkwaruzo. Kisha mfalme akaamuru hivi: ‘Watupeni wanaume waliomshtaki Danieli ndani ya shimo la simba.’ Wanaume hao walipotupwa, simba wakawararua.

Dario akawaamuru watu wote hivi: ‘Kila mtu lazima amwogope Mungu wa Danieli. Alimwokoa Danieli kutoka katika shimo la simba.’

Je, wewe husali kwa Yehova kila siku, kama Danieli?

Danieli ndani ya shimo la simba

“Yehova anajua jinsi ya kuwakomboa kutoka kwenye jaribu watu wenye ujitoaji-kimungu.”​—2 Petro 2:9

Maswali: Danieli alifanya nini mara tatu kwa siku? Yehova alimwokoaje Danieli?

Danieli 6:1-28

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki