Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 98 uku. 228-uku. 229 fu. 1
  • Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Kigezo Chenye Kupuliziwa Roho cha Kazi ya Mishonari ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Watu wa Yehova Waimarishwa Katika Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • “Wakizungumza kwa Ujasiri kwa Mamlaka ya Yehova”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 98 uku. 228-uku. 229 fu. 1
Mtume Paulo na Barnaba wakimhubiria gavana wa Saiprasi, Sergio Paulo

SOMO LA 98

Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi

Mitume walitii amri ya Yesu ya kueneza habari njema duniani kote. Katika mwaka wa 47 W.K., akina ndugu kule Antiokia waliwatuma Paulo na Barnaba katika safari ya kuhubiri. Wahubiri hao wawili wenye bidii walisafiri katika eneo lote la Asia Ndogo wakitembelea maeneo kama vile Derbe, Listra, na Ikoniamu.

Paulo na Barnaba walimhubiria kila mtu, iwe alikuwa tajiri au maskini, kijana au mzee. Watu wengi walikubali kweli kumhusu Kristo. Paulo na Barnaba walipomhubiria Sergio Paulo, aliyekuwa gavana wa Saiprasi, mwanamume fulani mlozi alianza kuwapinga. Paulo akamwambia mlozi huyo hivi: ‘Yehova yuko dhidi yako.’ Mara moja, mlozi huyo akawa kipofu. Gavana Sergio Paulo alipoona jambo hilo, akawa mwamini.

Paulo na Barnaba walihubiri kila mahali. Walihubiri nyumba kwa nyumba, sokoni, barabarani, na katika masinagogi. Walipomponya mwanamume aliyekuwa kilema huko Listra, watu walioshuhudia muujiza huo walifikiri kwamba Paulo na Barnaba walikuwa miungu na kwa hiyo wakataka kuwaabudu. Lakini Paulo na Barnaba wakawakataza wakisema: ‘Mwabuduni Mungu peke yake! Sisi ni wanadamu tu.’ Kisha, Wayahudi fulani wakafika na kuuchochea umati dhidi ya Paulo. Umati huo ukampiga kwa mawe, ukamkokota nje ya jiji, na kumwacha huko wakiwazia alikuwa amekufa. Hata hivyo, Paulo bado alikuwa hai! Mara moja, akina ndugu wakaja kumchukua na kumrudisha jijini. Baadaye, Paulo alirudi Antiokia.

Katika mwaka wa 49 W.K., Paulo alifunga safari nyingine. Baada ya kuwatembelea akina ndugu kule Asia Ndogo, alienda mbali zaidi akihubiri habari njema kufikia Ulaya. Alienda katika maeneo ya Athene, Efeso, Filipi, Thesalonike na sehemu nyingine. Sila, Luka, na mwanamume kijana anayeitwa Timotheo walisafiri pamoja na Paulo. Walishirikiana kuanzisha makutaniko na kuyasaidia yawe imara. Paulo aliishi Korintho kwa mwaka mmoja na nusu, akiwaimarisha akina ndugu huko. Alihubiri, akafundisha, na kuyaandikia makutaniko barua nyingi. Pia, alifanya kazi ya kutengeneza mahema. Mwishowe, Paulo alirudi Antiokia.

Mtume Paulo akihubiri sokoni

Baadaye, katika mwaka wa 52 W.K., Paulo alisafiri kwa mara ya tatu akianzia Asia Ndogo. Alisafiri mbali kaskazini hadi Filipi kisha akashuka kuingia Korintho. Paulo aliishi Efeso kwa miaka kadhaa, akifundisha, akiponya, na kusaidia kutaniko hilo. Pia, alitoa hotuba kila siku katika ukumbi wa shule. Watu wengi walisikiliza na kubadili njia zao. Hatimaye, baada ya kuhubiri habari njema katika maeneo mengi, Paulo akaenda Yerusalemu.

“Basi, nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.”​—Mathayo 28:19

Maswali: Ukitumia ramani iliyo katika Biblia yako (Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, Nyongeza B13), je, unaweza kuona jinsi Paulo alivyosafiri alipokuwa akihubiri?

Matendo 13:1–23:35

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki