Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 101 uku. 234-uku. 235 fu. 4
  • Paulo Apelekwa Roma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Paulo Apelekwa Roma
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Uwe Jasiri​—Yehova Ni Msaidizi Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • “Hakuna Hata Mmoja Wenu Atakayepotea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Piga Mbiu ya Ufalme wa Yehova kwa Ujasiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 101 uku. 234-uku. 235 fu. 4
Paulo na wengine wakiogelea au kushikilia vipande vya meli iliyovunjika karibu na pwani ya Malta

SOMO LA 101

Paulo Apelekwa Roma

Safari ya tatu ya kuhubiri ya Paulo iliishia kule Yerusalemu. Akiwa huko, alikamatwa na kutupwa gerezani. Wakati wa usiku, Yesu alimwambia hivi katika maono: ‘Utaenda Roma na kuhubiri huko.’ Paulo alichukuliwa kutoka Yerusalemu na kupelekwa Kaisaria ambako alifungwa kwa miaka miwili gerezani. Alipokuwa akishtakiwa mbele ya Gavana Festo, Paulo alisema hivi: ‘Acha nihukumiwe na Kaisari, huko Roma.’ Festo akamwambia: “Umekata rufaa kwa Kaisari; nawe utaenda kwa Kaisari.” Paulo alisafirishwa kwa meli kwenda Roma. Ndugu wawili Wakristo, Luka na Aristarko, walienda pamoja naye.

Baharini, walipatwa na dhoruba ambayo iliendelea kwa siku nyingi. Kila mtu aliyekuwa ndani ya meli hiyo alifikiri kwamba wangekufa. Lakini Paulo akawaambia: “Wanaume, malaika ameniambia hivi katika ndoto: ‘Usiogope, Paulo. Utafika Roma, na wale wote wanaosafiri pamoja nawe watakuwa salama.’ Iweni jasiri! Hatutakufa.”

Dhoruba hiyo iliendelea kwa siku 14. Mwishowe, wakaona nchi kavu. Kilikuwa kisiwa cha Malta. Meli hiyo ikagonga mwamba na kuvunjika vipande-vipande, lakini watu wote 276 waliokuwa ndani ya meli hiyo, wakafika salama kwenye nchi kavu. Baadhi yao waliogelea na wengine walishikilia vipande vya meli hiyo na kuelea hadi ufuoni. Watu wa Malta wakawasaidia na hata waliwasha moto ili wapate joto.

Miezi mitatu baadaye, wanajeshi wakampeleka Paulo hadi Roma kwa kutumia meli nyingine. Alipofika, akina ndugu walikuja kumpokea. Alipowaona, Paulo akamshukuru Yehova na kujipa nguvu. Ingawa Paulo alikuwa mfungwa, aliruhusiwa kuishi katika nyumba ya kukodiwa huku akilindwa na mwanajeshi. Aliishi pale kwa miaka miwili. Watu walikuja kumtembelea naye akawahubiria kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwafundisha kumhusu Yesu. Pia Paulo aliyaandikia barua makutaniko kule Asia Ndogo na Yudea. Kwa kweli, Yehova alimtumia Paulo kueneza habari njema kwa mataifa.

“Katika kila njia tunajipendekeza kuwa wahudumu wa Mungu, kwa kuvumilia mengi, kwa dhiki, kwa nyakati za uhitaji, kwa shida.”​—2 Wakorintho 6:4

Maswali: Kwa nini Festo alimpeleka Paulo Roma? Ni nini kilichompata Paulo alipokuwa akielekea Roma?

Matendo 21:30; 23:11; 25:8-12; 27:1–28:31; Waroma 15:25, 26

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki