Utangulizi wa Sehemu ya 4
Katika sehemu hii tutajifunza kuhusu Yosefu, Ayubu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo mengi mabaya kutoka kwa Ibilisi. Baadhi yao walitendewa isivyo haki, wakafungwa gerezani, wakawa watumwa, na hata wengine wakauawa. Hata hivyo, Yehova aliwalinda katika njia mbalimbali. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe jinsi ambavyo watumishi hao wa Yehova walivumilia mambo mabaya bila kuruhusu imani yao idhoofike.
Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha yeye ni mwenye nguvu kuliko miungu yote ya Wamisri. Kazia jinsi ambavyo Yehova aliwalinda watu wake wakati uliopita na jinsi anavyofanya hivyo leo.