WIMBO NA. 107
Mungu—Kielelezo cha Upendo
Makala Iliyochapishwa
1. Yehova Mungu ni kielelezo.
Mungu ni Upendo.
Atuongoza kwa upendo wake.
Tuonyeshe sifa zake.
Alimtoa Yesu Mwana wake.
Kwa dhambi zetu; tupate wokovu.
Upendo huo—Hauna kifani!
Mungu wetu, Mungu ni ’Pendo.
2. Tumwige Mungu, tuwe na upendo
Kwa ndugu na dada.
Tuwe tayari kuwasaidia,
Wa zamani; wapya pia.
Tuwaonyeshe upendo mwororo.
Tusibague huyu au yule.
Tuwasamehe watukoseapo.
Tuwapende; tupende wote.
3. Kupenda Mungu kunatuchochea,
Daima; Milele.
Yehova Mungu anatuhimiza:
‘Onjeni na Mwone kweli’
Twaunganishwa na upendo wake,
Neno la Mungu linatusafisha.
Na roho yake inatuchochea.
Mungu wetu, Mungu ni ’Pendo.
(Ona pia Rom. 12:10; Efe. 4:3; 2 Pet. 1:7.)