Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lvs uku. 3
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Soma katika “Upendo wa Mungu”
  • Habari Zinazolingana
  • Upendo wa Mungu Unadumu Milele
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Kaa Katika Upendo wa Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Usiruhusu Upendo Wako Upoe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • “Kumpenda Mungu Humaanisha Hivi”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Pata Habari Zaidi
Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
lvs uku. 3

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Kwa wale wanaompenda Yehova Mungu na Neno lake, Biblia:

Yesu alisema: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Wazia jinsi ulivyohisi ulipojifunza kweli ya Biblia kwa mara ya kwanza! Ulisisimuka kujua kwamba katika ulimwengu uliojaa uwongo, tunaweza kujifunza kweli.—2 Timotheo 3:1.

Yehova Mungu anataka tujue kweli. Na kwa sababu tunawapenda wengine, tunataka kuwaeleza kuihusu. Lakini mengi zaidi yanahusika ili kumtumikia Mungu kwa njia inayofaa. Lazima tufanye yote tuwezayo kuishi kwa njia inayowafaa Wakristo kwa sababu tunaheshimu sana kanuni za Yehova. Yesu alieleza njia muhimu ambayo tunaweza kumthibitishia Mungu kwamba tunampenda. Alisema hivi: “Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile ambavyo nimeshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.”—Yohana 15:10.

Yesu anampenda sana Baba yake, naye hufanya kila kitu ambacho Baba yake anamtaka afanye. Tukimwiga Yesu kwa kuishi maisha yanayofaa, Yehova atatupenda na tutakuwa na furaha ya kweli. Kama Yesu alivyosema, ‘mkijua mambo haya, mtakuwa wenye furaha mkiyatenda.’—Yohana 13:17.

Ni tumaini letu kwamba kitabu hiki kitakusaidia kujifunza kuishi kupatana na kweli ya Biblia na kuwa rafiki ya Mungu. Tunasali kwamba utaendelea kukua katika upendo kwa Mungu na kudumu ‘katika upendo wa Mungu ili hatimaye upate uzima wa milele.’—Yuda 21.

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki