Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 25
  • Kuuelewa Unabii wa Ezekieli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuuelewa Unabii wa Ezekieli
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Habari Zinazolingana
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Muhtasari wa Ezekieli
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Kitabu Cha Biblia Namba 28—Ezekieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • “Sasa Mwisho Umekufikia”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr uku. 25
Mkusanyo wa picha: Kuuelewa Unabii wa Ezekieli. 1. Maono: mwanamume aliyeonekana kama shaba, akiwa na kamba ya kitani na utete wa kupimia. 2. Mifano: chungu cha kupikia kilicho jikoni. 3. Maigizo: Ezekieli akijenga ukuta wa kuzingira kuzunguka tofali.

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 2A

Kuuelewa Unabii wa Ezekieli

UFAFANUZI—UNABII NI NINI?

Katika Biblia, kitenzi cha Kiebrania na·vaʼʹ, kinachotafsiriwa “kutoa unabii,” humaanisha hasa kutangaza ujumbe ulioongozwa na roho ya Mungu, hukumu, mafundisho ya maadili, au amri kutoka kwa Mungu. Pia, linaweza kumaanisha kutoa tangazo linalotoka kwa Mungu kuhusu jambo litakalotokea. Unabii wa Ezekieli unahusisha aina hizo zote za ufunuo kutoka kwa Mungu.—Eze. 3:10, 11; 11:4-8; 14:6, 7; 37:9, 10; 38:1-4.

JINSI ULIVYOWASILISHWA

  • Mwanamume aliyeonekana kama shaba, akiwa na kamba ya kitani na utete wa kupimia.

    MAONO

  • Chungu cha kupikia kikiwa jikoni.

    MIFANO

  • Ezekieli akijenga ukuta wa kuzingira kuzunguka tofali.

    VIELEZI

Kitabu cha Ezekieli kina maono, mifano, vielezi, na maigizo ya ujumbe wa unabii.

UTIMIZO

Nyakati nyingine unabii uliotolewa na Ezekieli una utimizo zaidi ya mmoja. Kwa mfano, unabii uliohusu kurudishwa kwa ibada safi ulitimizwa kwa kiwango kidogo watu wa Mungu waliporudi katika Nchi ya Ahadi. Lakini kama inavyozungumziwa katika Sura ya 9 ya kitabu hiki, unabii mwingi unaohusu kurudishwa kwa ibada safi unatimizwa leo na pia utatimizwa wakati ujao.

Wakati uliopita, tulifikiri kwamba sehemu nyingi za unabii wa Ezekieli zilikuwa na utimizo halisi na utimizo wa mfano. Hata hivyo, kitabu hiki hakisemi kwamba mtu, kitu, mahali, au tukio lolote ni ufananisho wa kinabii wa jambo fulani linalotimia siku zetu, isipokuwa kuwe na msingi wa Kimaandiko wa kufanya hivyo.a Badala yake, kitazungumzia utimizo mkubwa zaidi wa unabii wa Ezekieli. Pia, kitazungumzia masomo tunayojifunza kutokana na ujumbe wa Ezekieli na pia watu, maeneo, na matukio aliyotaja.

Angalia sura ya 2, fungu la 30

a Kwa maelezo zaidi kuhusu maana halisi na maana ya mfano (ufananisho), tazama gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2015, uku. 9-11, fu. 7-12; na “Maswali Kutoka kwa Wasomaji,” uku. 17-18 wa gazeti hilo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki