SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 13A
Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti
Hekalu Ambalo Ezekieli Aliona:
Ezekieli aliwafafanulia wahamishwa Wayahudi huko Babiloni kulihusu
Lina madhabahu ambapo dhabihu nyingi zinatolewa
Linakazia viwango vya Yehova vya uadilifu kuhusu ibada
Linakazia fikira zetu kwenye kurudishwa kwa ibada safi kulikoanza mwaka wa 1919
Hekalu Kubwa la Kiroho:
Paulo alilifafanua alipokuwa akiwaandikia Wakristo Waebrania
Lina madhabahu ambapo dhabihu moja inatolewa, “mara moja kwa wakati wote” (Ebr. 10:10)
Linafafanua uhalisi wa mpango wa kiroho ambao ulikaziwa zamani kupitia hema la ibada na mahekalu halisi—Mpango wa Yehova wa ibada safi kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Kristo
Linakazia fikira zetu kwenye kazi ambayo Kristo alifanya akiwa Kuhani Mkuu Zaidi kuanzia mwaka wa 29 hadi 33 W.K.