Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • th somo la 12 uku. 15
  • Kuzungumza kwa Hisia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzungumza kwa Hisia
  • Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Habari Zinazolingana
  • Shauku
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kujitahidi Kugusa Moyo
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Zungumza kwa Hisia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
Pata Habari Zaidi
Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
th somo la 12 uku. 15

SOMO LA 12

Kuzungumza kwa Hisia

Andiko lililotajwa

1 Wathesalonike 2:7, 8

MUHTASARI: Zungumza na wasikilizaji kwa njia inayoonyesha unawapenda na unataka kuwasaidia.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Wafikirie wasikilizaji wako. Unapojitayarisha, jaribu kuwazia jinsi wasikilizaji wako wanavyohisi na matatizo wanayokabili. Unapofanya hivyo, utazungumza kwa hisia.

  • Chagua maneno yako kwa uangalifu. Tafuta maneno ya kuwaburudisha, kuwafariji, na kuwaimarisha wasikilizaji wako. Epuka kutumia maneno yatakayowaudhi wasikilizaji bila sababu ya msingi, na usizungumze vibaya kuwahusu watu wasiomwabudu Yehova au kuhusu mambo wanayoamini.

  • Onyesha upendezi. Kwa sauti ya fadhili na ishara zinazofaa za mwili, waonyeshe wasikilizaji wako kwamba unawapenda. Hakikisha kwamba uso wako unaonyesha hivyo pia. Jaribu kutabasamu mara nyingi.

    Dokezo linalofaa

    Usilazimishe au kutia chumvi unapoonyesha hisia. Unaposoma tokeza hisia zinazoonyeshwa kwenye habari unayosoma, lakini usifanye hivyo kupita kiasi hivi kwamba ujielekezee fikira. Jitahidi kuzungumza na wasikilizaji kwa sauti yenye fadhili na upendo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki