Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • it uku. 299
  • Malaki, Kitabu cha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaki, Kitabu cha
  • Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 39—Malaki
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Bwana wa Kweli Aja kwa Ajili ya Hukumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Yehova Huchukia Mwenendo wa Hila
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Ufahamu wa Kina wa Maandiko
it uku. 299

MALAKI, KITABU CHA

Kitabu cha mwisho cha Maandiko ya Kiebrania katika Biblia za kisasa za Kiswahili. Katika mapokeo ya Kiyahudi, kitabu cha Malaki kimewekwa miongoni mwa maandishi ya mwisho ya wale wanaoitwa manabii wadogo, kabla ya Maandishi (Hajiografa). Kitabu hiki kina tangazo la Yehova kwa Waisraeli kupitia Malaki.—Mal 1:1.

Hali zilivyokuwa katika Siku za Malaki. Malaki alipokuwa akitoa unabii, makuhani walikuwa katika hali mbaya sana. Tofauti na Sheria ilivyotaka, walikuwa wakikubali wanyama vilema, vipofu, na wagonjwa ili kuwatoa dhabihu katika madhabahu ya Yehova. (Mal 1:8; Law 22:19; Kum 15:21) Walishindwa kuwapa watu mwongozo na maagizo yanayofaa hivi kwamba wengi wao walijikwaa. (Mal 2:7, 8) Walitoa hukumu kwa upendeleo. (2:9) Mambo yote hayo yalikuwa na matokeo mabaya kwa Waisraeli kwa ujumla, nayo yaliwafanya waone utumishi wa Yehova kuwa usio na thamani. (3:14, 15) Hali hiyo ilionekana wazi Waisraeli walipoacha kuunga mkono utendaji wa hekalu kwa kutotoa sehemu ya kumi. Waliacha kabisa kujitoa kwa Yehova hivi kwamba walikuwa wakiwataliki wake zao na kuoa wanawake waliokuwa wakiabudu miungu ya uwongo. Pia, Waisraeli walikuwa wenye kufanya ulozi, uzinzi, uwongo, ulaghai, na wakandamizaji. (2:11, 14-16; 3:5, 8-10) Kwa sababu ya matendo hayo, Yehova aliwaonya mapema kwamba angekuja kuhukumu hekalu lake. (3:1-6) Wakati huohuo aliwahimiza watenda dhambi watubu, kwa kuwaambia hivi: “Nirudieni, nami nitawarudia”​—Mal 3:7.

Kipindi cha Uandikaji. Ushahidi wa mambo ya ndani unatoa msingi wa kujua wakati wa kumalizika kwa uandikaji wa kitabu cha Malaki. Kiliandikwa baada ya kutoka utekwa wa Babiloni kwa kuwa Waisraeli walikuwa chini ya uongozi wa gavana. Ibada ilikuwa ikifanyika hekaluni, jambo linaloonyesha kwamba lilikuwa limejengwa. (Mal 1:7, 8; 2:3, 13; 3:8-10) Hilo linatuleta katika kipindi cha Hagai (520 K.W.K.) na Zekaria (520-518 K.W.K.), manabii hao waliwasihi kwa bidii Waisraeli wamalize ujenzi wa hekalu. (Ezr 5:1, 2; 6:14, 15) Inaonekana hali za Waisraeli kuacha ibada safi na kushika sheria ya Mungu zinalingana na wakati Nehemia alipofika Yerusalemu muda mfupi baada ya mwaka wa 32 wa Mfalme Artashasta (karibu 443 K.W.K.). (Linganisha Mal 1:6-8; 2:7, 8, 11, 14-16; Ne 13:6-31.) Hivyo, sawa na kitabu cha Nehemia, huenda kitabu cha Malaki kilianza kuandikwa baada ya mwaka wa 443 K.W.K.

Upatano na Vitabu Vingine vya Biblia. Kitabu hiki kinapatana kabisa na Maandiko mengine yote. Mtume Paulo alinukuu kutoka Malaki 1:2, 3 alipokuwa akionyesha kwamba kuchaguliwa na Mungu ‘hakutegemei jinsi mtu anavyotamani au jitihada zake, bali kwa kutegemea Mungu, aliye na rehema.’ (Ro 9:10-16) Yehova anatajwa kuwa Muumba (Mal 2:10; linganisha Zb 100:3; Isa 43:1; Mdo 17:24-26) na mwenye haki, rehema, na Mungu asiyebadilika na asiyekosa kuwaadhibu wanaofanya dhambi kimakusudi.(Mal 2:2, 3, 17; 3:5-7, 17, 18; 4:1; linganisha Kut 34:6, 7; Law 26:14-17; Ne 9:17; Yak 1:17.) Umuhimu wa jina la Mungu unasisitizwa. (Mal 1:5, 11, 14; 4:2; linganisha Kum 28:58, 59; Zb 35:27; Mik 5:4.) Na kitia moyo kimetolewa cha kukumbuka Sheria ya Musa.​—Mal 4:4.

Kitabu hiki kiliwasaidia Waisraeli kufahamu kuhusu kuja kwa Masihi na siku ya Yehova. Ingawa kinataja kwamba Yehova yule anayemwita “mjumbe wangu,” mtu huyo angekuwa mtangulizi tu wa “mjumbe wa agano” aliye mkuu atakayekuja na Yehova. (Mal 3:1) Masimulizi yaliyoongozwa na roho katika Mathayo (11:10-14; 17:10-13), Marko (9:11-13), na Luka (1:16, 17, 76) kwa pamoja yanamtambulisha mtangulizi wa Yesu, Yohana Mbatizaji kuwa “mjumbe” na “Eliya” anayetajwa mwanzoni katika Malaki 3:1 na 4:5, 6.

[Sanduku katika ukurasa wa 299]

MAMBO MAKUU YA MALAKI

Tangazo linalosisitiza uwajibikaji kwa Yehova Mungu ikiwa viwango vyake vinapuuzwa

Limeandikwa na nabii Malaki, huenda miaka 95 hivi baada ya Wayahudi wa kwanza waliokuwa uhamishoni kurudi kutoka Babiloni

Yehova aliwapenda Waisraeli, hata hivyo walilidharau jina lake (1:1-14)

Yehova aliwapenda watu wake sawa tu na alivyompenda Yakobo, ingawa alimchukia Esau

Pamoja na hayo, makuhani wa taifa la Israeli walilidharau jina la Mungu, walikubali kutoa dhabihu wanyama walemavu na wagonjwa; wanyama ambao hawangeweza kumpa gavana mwanadamu

Makuhani na watu walaumiwa kwa kushindwa kudumu katika njia za Yehova (2:1-17)

Makuhani wameiacha njia ya Mungu na kufanya wengi “wajikwae kuhusiana na sheria,’ na hivyo ‘waliliharibu agano la Lawi’

Wengi wameoa wake kutoka mataifa ya kigeni, na baadhi ya Waisraeli wamewatendea kwa hila wake wa ujana wao kwa kuwataliki

Waisraeli wamemchosha Mungu kwa kudai kwamba anakubali wote wanaotenda mambo hayo mabaya

Bwana wa kweli atawahukumu na kuwasafisha watu wake (3:1-18)

Yehova atakuja hekaluni akiwa na mjumbe wa agano; atawasafisha na kuwatakasa Walawi, na zawadi ya Yuda itampendeza Yehova

Walozi, wazinzi, wale wanaoapa kwa uwongo, walaghai, na wanaokandamiza wengine watahukumiwa bila kukawia

Leta sehemu yote ya kumi katika ghala la Yehova ili upate mafuriko ya baraka

Kitabu cha kumbukumbu kitaandikwa kwa ajili ya wale wanaomwogopa Yehova; Watu wake watatambua tofauti katika ya mwadilifu na mwovu

Kuja kwa siku kuu ya Yehova na yenye kuogopesha (4:1-6)

Siku ya Yehova itawaharibu kabisa waovu, lakini “jua la uadilifu litawaangazia” wanaoliheshimu jina la Mungu

Kazi ya kurudisha itafanywa kwanza na nabii Eliya, kabla ya siku hiyo kuja

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki