Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 7/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ni Nini Hutendeka Katika Harusi za Mashahidi wa Yehova?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Ongeza Shangwe na Heshima ya Siku Yako ya Arusi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Arusi Zenye Kuheshimika Machoni pa Mungu na Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 7/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Je! inafaa Wakristo waadhimishe siku ya arusi yao kila mwaka?​—D. Y., Venezuela.

Si jambo linalopingana na Maandiko kwa watu waliooana kuadhimisha siku ya arusi yao kila mwaka katika njia ya akili na adabu nzuri. Wala si jambo la maana sana.

Kwa msingi siku hiyo inakumbusha tukio lililotukia wakati fulani uliopita. Kuna matukio mengi yanayoadhimishwa kila mwaka. Wapagani wameadhimisha kila mwaka mambo ya pekee yaliyotukia. Hata watumishi wa Mungu wamefanya hivyo. (Kut. 12:14, 24-27; Yohana 10:22, 23; 1 Kor. 11:23-26) Bila shaka, maadhimisho haya au kumbukumbu za kila mwaka zinazotajwa katika Biblia zilihusiana sana na ibada ya kweli. Hata hivyo, tunaweza kuona kutokana na hili kwamba si maadhimisho yote yanayoweza kusemwa kwamba hayafai. Inategemea sana jambo linaloadhimishwa na namna linavyoadhimishwa.

Bila shaka Mkristo ataepuka maadhimisho yanayohusiana na mazoea yanayopingana na Biblia au ya dini ya uongo. (Yohana 4:24) Lakini leo, kwa kawaida mwadhimisho wa siku ya kila mwaka ya arusi si jambo la kidini. Lakini je! desturi ya kuadhimisha siku ya arusi ilitokana na dini ya kipagani ya kale? Kwa wazi sivyo. Encyclopedia Americana (1971 ed.) kinasema hivi: “Mazoea ya jamaa ya kuadhimisha siku ya arusi ya kila mwaka inaelekea yalianza katika Ulaya ya Magharibi. Mtajo ulio wa zamani sana katika vitabu vya Kiingereza unaonekana katika karne ya 17.”​—Vol. 28, uku. 564.

Kuadhimisha siku ya arusi yao kila mwaka ni jambo la kawaida sasa kwa mume na mke katika nchi nyingine. Wakristo waliooana wanafanya hivyo pia. Wakiongozwa na dhamiri zao wanaona kwamba wanaweza kuvitia nguvu vifungo vya ndoa yao kwa kukumbuka kwa utulivu na kwa faragha wakati wenye furaha walipopata kuwa mume na mke. Katika siku ya kila mwaka ya arusi yao wanaweza kujikumbusha juu ya maendeleo waliyoyafanya katika kujenga ndoa yenye furaha na watie nguvu azimio lao la kuendelea kufanya hivyo.

Watu wengine waliooana wanaweza kufurahia kushiriki furaha ya siku ya arusi yao ya kila mwaka pamoja na rafiki zao wachache Wakristo pamoja na jamaa zao, kutia na watoto wao. Wakifanya hivyo, kuna mambo machache ya kukumbukwa ambayo yanapaswa kusawazishwa.

Katika mkutano wo wote wa watu wengi au mwadhimisho, uangalifu unahitajiwa ili mambo yasipite kiasi. Hata mwadhimisho mdogo unaweza kuwa usiozuilika au uongoze kwenye mwenendo usiofaa, kama inavyoelekea ilifanyika mara kwa mara kati ya Wayahudi katika karne ya kwanza. (Yohana 2:10) Bila shaka hiyo haingewafaa Wakristo. (1 Pet. 4:3, 4) Wala haingefaa wale wanaoadhimisha kuwapa wanadamu heshima inayopita kiasi, kana kwamba wawili waliooana ambao wanaadhimisha siku ya arusi yao ya kila mwaka wanapaswa kuabudiwa. Biblia inaonyesha waziwazi kwamba ibada inapaswa kumwendea Muumba peke yake, wala si kiumbe cho chote duniani, kiwe mnyama au mwanadamu. (Kum. 1:24, 25) Ikiwa watu wawili waliooana wamefanikiwa katika ndoa, ni vyema. Wengine wanaweza kuwafurahia kwa kufaa. Lakini je! hilo haliwezi vilevile kuchochea shukrani za kumsifu Mwanzilishi wa ndoa? Anapaswa kukumbukwa na lo lote linalofanywa linapaswa kumtukuza Yeye.

Kwa kusema hayo yaliyopo hapo juu sisi hatupendekezi kwamba wale waliooana ambao hawafuati desturi hii ya kuadhimisha siku ya arusi yao ya kila mwaka waanze kufanya hivyo. Kwa kweli, sisi hatuwatii moyo watu waadhimishe au waache kuadhimisha siku ya arusi yao ya kila mwaka. Wale waliooana wanaweza kuamua wao wenyewe namna watakavyofanya bila kulaumiwa na wengine. Hali au dhamiri za wawili waliooana zinaweza kuwaongoza wasiadhimishe jambo hilo. Hata hivyo wengine wanaweza kuadhimisha. Ikiwa ndivyo, basi, uamuzi juu ya vile watakavyofanya hivyo unaweza kufanywa kupatana na shauri hili: “Mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu,”​—1 Kor. 10:31.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki