Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 4/1 kur. 163-166
  • Je! Unaweza Kumngoja Yehova?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unaweza Kumngoja Yehova?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUNGOJA KUONDOLEWA KATIKA UPINZANI
  • TUMAINI LENYE NGUVU UNAPOPATWA NA UGONJWA
  • HUENDA NDOA IKAHITAJI KUNGOJA
  • Furahia Kumngojea Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Uwe Mwenye Furaha Unapomngojea Yehova kwa Subira
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Je, Unajua Jinsi ya Kungoja?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Je, Uko Tayari Kungoja kwa Subira?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 4/1 kur. 163-166

Je! Unaweza Kumngoja Yehova?

“LAKINI mimi, nitamtazamia [Yehova]; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.” Ndivyo alivyosema nabii Mika.​—Mik. 7:7.

Je! wewe unalo tumaini lenye nguvu katika Mungu kama yeye alivyokuwa nalo? Je! unaweza kumngoja Yehova? Unapotumainia kupata jambo fulani lenye kupendeza lisilopatikana wakati huo, je! unaonyesha kutokusubiri kama kwa mtoto au unaonyesha wazi tumaini tulivu katika Yehova? Unapokutana na msiba, je! wewe ‘unamngojea Mungu wa wokovu wako’?

Kungoja si kwepesi sikuzote. Zaidi ndivyo ilivyo ambapo mtu ametumainia kupata kitu fulani kwa muda mrefu. Kama vile mithali iliyoongozwa na roho ya Mungu isemavyo, “Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.” (Mit. 13:12) Hata hivyo, wakati unapita kwa mwendo ulio sawasawa, nazo baraka zinatujia tunapofanya yote tuwezayo kuhakikisha matokeo yafaayo na kuyafikiria mapenzi ya Yehova kwetu katika kufanya mipango. Vile vile, nyakati nyingine tunapokea baraka zisizotazamiwa, kutoka upande usiotazamiwa hata kidogo, na kwa hizi vile vile tu wenye shukrani kwa Yehova.

Nyakati nyingine tunakutana na hali tusizoweza kuazimia kwa uwezo wetu wa kibinadamu. Halafu? Umngoje Yehova​—ndiyo, “Umtumaini Yehova”! Siyo kwa kuketi tu bila kufanya lo lote, bali kwa kusali kwa Yehova kwa bidii aongoze mambo kisha kuyaacha matokeo kwa matumaini mikononi mwake.​—Zab. 27:14, NW; Mit. 20:22.

Ni muhimu kufahamu kwamba, ingawa Yehova ajua twahitaji mambo fulani, yeye hatufungulii njia ya kuvipata vyote vilivyotazamiwa papo hapo sikuzote. Kwanza, huenda tusiwe tayari kwa daraka linalokuja pamoja na zawadi au pendeleo linalotakiwa. Hivyo pana uhitaji wa subira.

Vile vile, nyakati nyingine huenda tufikiri twahitaji jambo fulani la pekee, lakini huenda likawa halihitajiwi kweli kweli; huenda kwa kweli likawa lenye madhara kwetu. Kwa sababu hii Yehova hatufungulii njia ya kulipatia. Bila shaka, kwa kujitahidi huenda mwishowe tukapata tamaa mbaya au ya upumbavu, lakini hatutapata furaha ya kweli ama uradhi kwa njia hii. Bali, twajiletea wenyewe ugumu na masumbufu ya bure kwa sababu ya kutoyafikiria mapenzi ya Yehova kwetu sisi na kutokumngoja.

Je! wewe ni kijana? Basi huenda ukawa kama vijana wengi katika kutaka kukua kwa haraka ili uyapate mapendeleo na haki zinazofurahiwa na watu wazima. Vijana wengine wanaona kwamba uongozi wa wazazi una vizuizi vingi mno nao wanaitamani siku ambapo wanaweza kuwa huru na uzuizi wa wazazi. Lakini Yehova kwa hekima na kwa upendo amepanga kwamba kutokukomaa kwa vijana, upumbavu na harara yao, vizuiwe na wazazi wao mpaka wameweza kujitwalia daraka la mtu mzima. Hivyo kungoja ndiyo njia ya hekima; ni kuukubali mpango wa Yehova. Lakini siyo kungoja bila ya kufanya lo lote.

Mtu anapokuwa angali ujanani, kuna mengi ya kujifunza na kuna na nafasi nyingi za kupatia ujuzi, ufundi na kujiweza. Kwa kuwasikiliza wazazi wako kwa makini na waalimu unaweza kuuongeza ujuzi wako kila siku katika sehemu nyingi na kupata mazoezi bora kusudi kwamba uweze kujitunza mwenyewe nyumaye katika maisha.

Je! wewe unafikia cheo cha mwangalizi, au unataka kuwa mtumishi wa huduma katika kundi la Kikristo? (Flp. 1:1; 1 Tim. 3:1) Wakati wahitajiwa ili upate kustahili. Biblia yaonyesha kwamba ye yote anayewekwa hivyo hapaswi kuwa “mwanamume aliyegeuka hivi karibuni.” (1 Tim. 3:6, 10, NW) Wala cheo cha “mzee” kisingeweza kujazwa kwa kufaa na mtu ambaye angali ni kijana. Lazima awe amekwisha kujipatia heshima kwa sababu ya kuwa na maamuzi mazuri na uwezo wa kutoa onyo lenye busara. Yampasa awe na ufahamu wa magumu ya maisha. Lazima awe na msingi mzuri wa ujuzi wa Biblia kusudi aweze kuionyesha nia ya Yehova ya mambo katika kulifundisha kundi na katika kuadhibu inavyohitajiwa. Haya yote yanachukua wakati. Yanahitaji jitihada ya kipekee kuongeza uwezo mbalimbali wa mtu. Vile vile inahitaji kumngoja Yehova.

KUNGOJA KUONDOLEWA KATIKA UPINZANI

Pengine katika nyumba yako mna mwenzi asiyeamini au mzazi. Huenda yeye akawa amekupinga vikali kwa miaka mingi ulipotaka kuhudhuria mikutano ya Kikristo au kushiriki katika kuzihubiri habari njema. Unasali kwa ajili ya kuondolewa kwa mambo haya. Je! unaomba kwamba mpinzani aondolewe? Bila shaka sivyo! Bali, kwamba apate kuwa mwenye busara zaidi, kwamba upendo wa Mungu upate kuulainisha moyo wake na kwa njia hiyo apate kuwa mwamini mwenzetu ndani ya nyumba hiyo. Lakini mara nyingi sana hii inachukua wakati. Kwa sasa, kuliko kutamani ondoleo hili bila ya kufanya lo lote, kuna mambo ya wazi yawezayo kufanywa.

Kwa mfano, mtume Petro awaambia wake za Kikristo ili waweze kuwapata waume zao wasioamini bila ya mabishano. Kwa njia gani? Kwa utiifu uwapasao wake na kwa kujipamba wenyewe kwa roho ya upole. Pengine maendeleo yaweza kufanywa katika mambo haya. Mke na watoto wasipokipa kichwa cha nyumba nafasi ya manung’uniko ya haki, bila shaka hii itamvuta, hata ikiwa itachukua miaka mingi.​—1 Pet. 3:1, 2.

Mume mmoja aliiandikia Watch Tower Society: “Muda mfupi uliopita niliketi nami nikarudia kufikiri juu ya miaka kumi na miwili iliyopita ya maisha yangu. Mchanganuo huu ulinihuzunisha. Nikaona namna ambavyo nilikuwa nimekuwa mbaya sana kwa mke wangu, na hali yeye alivumilia kila kitu kwa unyenyekevu. . . . Kadiri ambavyo nilizidi kuwa mkatili, ndivyo alivyozidi kuonyesha upendo na rehema.” Sasa anaungana naye katika ibada ya Kikristo na utendaji, kwa furaha kuu ya mkewe na baraka. Yeye anafurahi kwamba alimngoja Yehova.

Je! wewe unasumbuliwa na udhalimu fulani? Huenda ukawa kati ya watu wachache wa kitaifa au wa jamii inayobaguliwa kwa njia mbalimbali nchini mwako. Au, huenda hata ukafungwa kwa sababu ya kutoridhiana juu ya jambo fulani lisilokufaa kama Mkristo. Maelekeo ya kawaida ni kulipiza kisasi. Huenda ukaona uchungu mwingi na kuacha chuki ijae moyoni mwako juu ya wale wa taifa jingine au juu ya wale walio na mamlaka. Lakini je! ni mwendo gani umfaao Mkristo?

Ikiwa yote yamekwisha kufanywa kutafuta ondoleo kwa wenye mamlaka au kwa njia ya yale uwezayo kufanya mwenyewe kwa amani, mngoje Yehova! “Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee [Yehova], naye atakuokoa.” (Mit. 20:22) Yesu aliutoa mfano ulio mwema kupita yote. Alipotendewa vibaya, hakutisha wala kuwatukana watesi wake. (1 Pet. 2:21-23) Baki ukiwa na uhakika wa kwamba udhalimu haupiti bila ya kuonwa na Mungu. Katika wakati wa Yehova uliowekwa, “watenda mabaya wataharibiwa, bali wamngojao [Yehova] ndio watakaoirithi nchi.” (Zab. 37:9) Pengine tunaelekea kutousubiri wakati huo ufike, lakini Mungu anawakumbuka watu wa namna zote kwa upendo.​—1 Tim. 2:4.

Je! haja yako ya uvumilivu wenye subira imekuwa kubwa kama ile ya Mkristo mchanga katika Ulaya aliyekamatwa kwa mara ya nne kwa sababu ya kutokuridhiana juu ya kutokuwamo kwake kwa Kikristo, na hivi nyuma ya kwisha kutumikia miaka kumi na mitatu na siku moja gerezani? Yeye aliendelea kumngoja Yehova. Yeye anaamini kwamba ‘Yehova ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu wakatiliwe mbali.’ (2 Pet. 2:9) Anaamini kwamba karibuni sana sasa Mungu atasimamia haki na uadilifu kwa njia ya ufalme wa kimbinguni mikononi mwa Mfalme wa Amani wake, Kristo Yesu. Je! wewe unayo imani hiyo?

TUMAINI LENYE NGUVU UNAPOPATWA NA UGONJWA

Je! wewe umepatwa na afya mbaya? Pengine umefanya yote uwezayo kwa akili uiendeleze afya yako kwa ulaji uliosawazika, pumziko, mazoezi na utabibu. Nini kiwezacho kufanywa sasa? Mngoje Yehova! Siyo kwa ajili ya kuponywa kwa mwujiza, lakini kwa ajili ya nguvu za kuvumilia, kwa ajili ya maamuzi mema katika kuchagua ni matibabu gani ya wakati ujao yatakayokuwa bora, kwa ajili ya ondoleo ambalo taratibu yake mpya italeta.

Ijapokuwa hatuhesabu magonjwa yetu yote na maumivu kuwa yamesababishwa na kujitia kwa moja kwa moja kwa Ibilisi, kama vile katika kisa cha Ayubu, hata hivyo twaweza kuwa na hakika yeye anajaribu nyakati nyingine kujipatia nafasi yake watu wa Yehova wanapokuwa katika hali yao ya kimwili iliyodhoofishwa ili awavunje moyo na hata kuwaachisha tumaini. Twauhitaji msaada wa Yehova. Mtunga zaburi Daudi alisali: “Nalimngoja [Yehova] kwa saburi, akaniinamia akakisikia kilio changu.” (Zab. 40:1) Hata wewe waweza kusali hivyo unapomngoja Yehova. Yehova hawaachi watumishi wake. Yeye anawapa nguvu za kuvumilia wakiendelea kumtumaini yeye.

Lakini namna gani daktari akimwarifu mtu kwamba kifo chakaribia? Kunakuwako sababu kubwa zaidi ya kumtumainia Yehova! Madaktari wamekosea; lakini ikiwa uchunguzi wake ni wa haki wakati huu, ni wazo lenye kusisimua kama nini kwamba haitampasa mtu kungoja muda mrefu kaburini mbele ya kusimama akiwa hai tena katika ufufuo chini ya ufalme wa Mwana wa Mungu. Yesu alisema: “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” Ayubu alisali kwamba Mungu amfiche katika Sheol na kumkumbuka katika wakati uliowekwa. (Yohana 5:28, 29; Ayubu 14:13-15) Ndiyo, tukiwa na faraja hiyo yenye nguvu, twaweza kukutana hata na kifo!

HUENDA NDOA IKAHITAJI KUNGOJA

Je! tamaa yako ni kuoa au kuolewa lakini kuna ugumu wa kumpata mtu afaaye? Au je! unahitaji kungoja kwa sababu u mchanga mno au mpaka hali fulani imetimizwa? Ingawa haitupasi tuazimie kwamba Yehova analeta watu fulani pamoja leo kwa ajili ya ndoa, hata hivyo twaweza kumngoja yeye katika mambo haya vile vile. Namna gani hivyo, wasema? Kwa kujipatanisha na takwa lake lenye hekima na upendo kwamba imetupasa tuoe au kuolewa “katika Bwana tu,” yaani, tuoe au kuolewa na mwabudu mwenzetu wa Yehova peke yake. (1 Kor. 7:39) Ikiwa twampenda Yehova kweli kweli, huo hautakuwa mzigo kwetu. Upendo uo huo wa Mungu utatuvuta kujaza maisha zetu na kazi ambayo Mungu amewapa watumishi wake wote waifanye. Hii itajaza siku zetu na utendaji, na maisha zetu na kusudi. Tunapomngoja Yehova tutakuwa na ‘mengi sana ya kutenda katika kazi ya Bwana, tukijua ya kwamba taabu yetu siyo bure.’​—1 Kor. 15:58.

Tunapomngoja mwenzi wa ndoa afaaye twaweza kuutumia wakati huo kusitawisha kujiweza, kujiendeleza kama Wakristo. Tutakuwa wenye kuyafikiri mambo ya kiroho zaidi, wenye uwezo zaidi wa kuchukua madaraka, na kwa njia hiyo kuwa wenye kupendeza zaidi kama mwenzi. Nyuma yake huenda tukakutana na mwamini mwenzetu apendezaye anayetafuta sifa zile zile katika mwenzi. Hata iweje, sisi hatukuwa wasiotenda, pengine katika njia yenye uzito, yenye mvunjo, wala hatukujiruhusu tuwe na wasiwasi wa moyoni. Tumekuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova nasi tumekuwa tukifanya maendeleo ya Kikristo.

Maandiko yana mifano tele ya wale waliomngoja Yehova nao wakabarikiwa sana. Juu ya hawa, Paulo aliandika: “Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi.”​—Ebr. 11:13.

Tofauti na watumishi hawa waaminifu wa kale, sisi tupo pale pale mlangoni pa taratibu mpya ambayo ‘waliiona tokea mbali.’ Kwa hiyo, kwa uhakikisho wenye nguvu na tuendelee kumngoja Yehova kwa uvumilivu, kwa maana ‘Yehova hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia.’ “Wewe umngoje [Yehova], uishike njia yake, naye atakutukuza uirithi nchi, wasio haki watakapoharibiwa utawaona.”​—2 Pet. 3:9, 13; Zab. 37:34.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki