Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 4/1 kur. 166-168
  • Upendo Wako wa Kweli Ni Wenye Nguvu za Kadiri Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Wako wa Kweli Ni Wenye Nguvu za Kadiri Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TAMAA YA KWELI
  • YAEPUKE MAELEKEO YA KUSEMA UONGO
  • Kuna Sababu ya Kuwaogopa Wafu?
    Amkeni!—2009
  • “Kifo Kimemezwa Milele”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Ni Nini Hutokea Tunapokufa?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Hofu ya Kifo—Unaweza Kuishindaje?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 4/1 kur. 166-168

Upendo Wako wa Kweli Ni Wenye Nguvu za Kadiri Gani?

TAMASHA yenyewe ilikuwako katika Queens, mji wa New York. Mwanamke mmoja alikuwa amemwomba mwuza nyama wake amsagie kipande fulani cha nyama. Lakini, mbele ya kuweza kukisaga, mwanamume aliyesimamia kazi hii alichukua kipande kingine cha nyama ovyo ovyo mahali pa kile kingine, naye akasisitiza kwamba mwuza nyama ampe mnunuzi hiki. Alipopewa nyama hiyo iliyosagwa, mnunuzi akamwuliza mwuza nyama: “Hii ndiyo nyama niliyokuambia usage?”

Ungejibuje wewe? Je! ungesema kweli?

Mnunuzi alikuwa na haki ya kuyajua mambo ya hakika. Na hali, chini ya hali hizo, haikuwa vyepesi kwa mwuza nyama kumwambia kweli, na kwa njia hiyo aufunue wazi udanganyifu wa mwanamume aliyesimamia kazi. Hata hivyo, yeye alifanya hivyo. Matokeo yake ni kwamba alifukuzwa.

Je! wewe ungalifanya alivyofanya yeye?

TAMAA YA KWELI

Inapoelekea kutumikia faida zao, ni kawaida kwa watu kusema uongo. Lakini je! wewe unapendezwa unapodanganywa?

Sisi twapenda kusikia kweli. Wazazi wanapenda kusikia kweli kwa watoto wao. Watoto wanataka wazazi wao wawaambie kweli. Serikali inatamani raia waiambie kweli, nao raia wanataka kweli kwa serikali yao. Lakini kinachopaswa zaidi kutupendeza sisi ni kwamba Mungu Mwenye Nguvu Zote anataka kuvisikia vinywa vyetu vikisema kweli. Neno lake lasema: “Mkaseme kweli kila mtu na jirani yake.”​—Efe. 4:25.

Ukristo unatajwa katika Biblia kama “njia ya kweli,” naye mtume Yohana alizungumza juu ya “watenda kazi pamoja na kweli.” (2 Pet. 2:2; 3 Yohana 8) Kwa wazi watu “waliomo katika kweli” (NW) wasingeweza kushughulika katika uongo.

Wakristo wa kwanza Anania na Safira wanatoa mfano unaofunua kuchukizwa kwa Mungu na udanganyifu wa makusudi. Wao walikuwa wameuza sehemu ya mali na kusingizia kuchanga vyote vilivyopatikana katika uuzaji vikatumiwe na Wakristo wenzao; lakini kwa kweli walikuwa wamejibakizia fedha fulani. Hivyo walifanya shauri kulitolea kundi maoni ya kwamba walikuwa wakarimu kupita walivyokuwa. Kwa ajili ya udanganyifu huu​—hila iliyopangwa kwa makusudi ya kusema uongo​—Mungu aliwaua.​—Matendo 5:1-11.

Kwa wazi, Mungu anayaona mazoea ya kusema uongo kama kosa zito. “Waongo wote,” Biblia yasema, wataingia katika “lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Ufu. 21:8) Basi, bila shaka imetupasa tujihadhari kwamba hatuuachi mfano huo wa kusema uongo uanze kusitawi katika maisha zetu.

YAEPUKE MAELEKEO YA KUSEMA UONGO

Lakini si vyepesi sikuzote kusema kweli. Nyakati nyingine, kwaweza kuwako maelekeo yenye nguvu ya kusema uongo, zaidi wakati ambapo mtu amefanya kosa analokusudia kulificha.

Kwa mfano, wakati fulani uliopita wazee wa Kikristo walitembelea nyumba ya mshiriki wa kundi wakazungumze naye waliyoyaangalia kama mambo yasiyo ya kawaida katika mwenendo wake. Yeye hakutaka kulizungumza shauri hili, na kwa hiyo akamtuma mshiriki wa jamaa yake mlangoni akiwa na maagizo akawaambie wazee hayupo nyumbani. Kufuata hapo, uongo wake ulipojulikana, alitoa udhuru juu yake kama uongo ‘mdogo’ tu. Hata hivyo, ulikuwa uongo, naye alimtia mshiriki mwingine wa jamaa katika uongo huo.

Sisi sote, wakati mmoja au mwingine na katika njia fulani au nyingine, tutakosea katika tunayoyasema. “Ikiwa ye yote hafanyi hivyo,” mwanafunzi Yakobo asema, “huyu ni mtu mkamilifu.” (Yak. 3:2, NW) Huenda tulitia chumvi tuliposema jambo fulani, au kwa njia nyingine tukasema uongo. Kwa mfano, huenda tulionyesha kukubali na hata uchangamfu kwa ajili ya shauri fulani ili tumpendeze mtu fulani na hali kwa kweli hatukujisikia hivyo.

Je! wewe wajisikiaje juu yako mwenyewe usemapo mambo yasiyo kweli? Je! inakutia nguvu kujiheshimu kwako au inakudhoofisha? Je! unakuwa mfano maishani mwako kusema mambo ya uongo? Yajapokuwa mambo yanayotiwa ndani huenda yakawa yenye matokeo madogo tu, matokeo ya uongo yaweza kuwa mazito isivyotazamiwa.

Kwa mfano, tuseme kwamba mwanamke anamwambia jirani, mtoto wake akisikia, kwamba yeye ‘anayapenda kweli kweli mapambo yake ya nguo.’ Halafu nyumaye, katika mazungumzo nyumbani, anamtajia mumewe kwamba majirani wanayo mapambo mapya ya nguo na kwamba yeye ‘hayapendi hata kidogo.’ Je! mtoto wake, anayemsikia akisema haya, hatadhani kwamba ni sawa kugeuza maana? Kwa hiyo, ijapokuwa hakuna kosa kuwa mwenye busara, kuna uhitaji wa kufikiria kama maneno yetu yataelekeza kwenye utovu wa heshima kwa kweli.

Bila shaka, mwendo wa hekima ni kutumia uangalifu juu ya ukweli wetu, na kutokuipuza michomo ya dhamiri. Katibu wa msimamizi wa bidhaa katika duka la idara ya Chicago alitumia uangalifu. Mkubwa wake alimwambia: “Ye yote akipiga simu, waambie mimi sipo.” Huenda dhamiri za watu wengine zikawaruhusu kusema hivi. Lakini, alipolifikiria shauri hili, dhamiri ya katibu ilimsumbua. Kwa hiyo alimweleza mkubwa wake kwa sababu gani, kama Mkristo, asingeweza kuwaambia watu kwamba hakuwapo na hali alikuwapo kweli afisini mwake. Mkubwa wake akamheshimu kwa ajili ya heshima nyingi kwa kweli.

Kweli, huenda maneno mengi yakaonwa kama uongo ‘mdogo.’ Lakini tusipojihadhari kuuepuka, je! hakuna hatari kwamba huenda tukaelekezwa kwenye kosa zito zaidi?

Bila shaka, si kila mtu atakayeuona ubora wa upendo wenye nguvu wa Mkristo kwa ajili ya kweli. Kwa mfano, mmoja wa mashahidi wa Yehova, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili ya kampani ya kutengeneza nchi katika Holden, Massachusetts, alipigiwa simu na benki ya mahali pake. Ilitaka kuhakikisha tarakimu fulani katika orodha ya uuzaji wa vifaa. Lakini, tarakimu zilizokuwamo ndani ya nakala ya faili zilikuwa tofauti na zile benki ilizokuwa nazo.

Mkubwa wake aliporudi, Shahidi akauliza jambo hili, naye mkubwa akakasirika. Orodha yenye makosa ya uuzaji, ikionyesha tarakimu kubwa zaidi, ilikuwa imepewa benki. Hili lilifanywa, alieleza mkubwa, ili kupata fedha zaidi kutoka kwa benki na kwa ajili ya makusudi ya kodi. Mkubwa alitaka Shahidi aipigie benki simu na kuonyesha masikitiko kwa ‘kosa lake kubwa sana’ na kuhakikisha tarakimu zilizogeuzwa ni za kweli. Shahidi akaeleza kwa sababu gani asingeweza kufanya hivi, naye alipoona kwamba mkubwa wake hakuiheshimu kweli, akaiacha kazi yake.

Mara nyingi inahitaji nguvu kweli kweli kusema kweli. Je! upendo wako wa kweli ni wenye nguvu za kadiri gani? Je! unasema kweli inapofaa tu? Ikiwa ndivyo, unatofautianaje na watu wanaoufuatia uaminifu kama “mashauri mema,” lakini wanaosema uongo inapoelekea kwamba itawafaidi?

Sababu yetu ya kusema kweli yapaswa kuwa kwamba ndilo jambo lifaalo kufanya; linampendeza Mungu. Ikiwa mtu anampenda Yehova Mungu kweli kweli na, juu ya kila kitu kinginecho, anataka kumpendeza yeye, basi hata mkazo wa mapendezi ya kichoyo uwe wenye nguvu namna gani, yeye hatakuwa mwongo wa kukusudia. Yeye atahakikisha kwa matendo yake kwamba ni mtumishi wa “[Yehova], Mungu wa kweli.”​—Zab. 31:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki