Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 3/15 kur. 143-144
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Habari Zinazolingana
  • Mwongozo Wenye Hekima kwa Wenzi wa Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Usitenganishe Kile Ambacho Mungu Ameunganisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wazionaje Mali?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Fanya Ndoa Yako Iwe Muungano Wenye Kudumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 3/15 kur. 143-144

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Ni nini linalomaanishwa na maneno ya Paulo katika 1 Wakorintho 7:29, “Wale walio na wake na wawe kama hawana”?

Shauri la mtume Paulo lililoongozwa na Mungu ni sehemu ya mazungumzo yanayoshauri kutokuoa au kutokuolewa kama mwendo ulio bora, kwa vile kwamruhusu Mkristo apate “kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine.” (1 Kor. 7:32-35) Shauri kwa waume kuwa ‘kama hawana wake’ basi lahusiana na kumtumikia Yehova Mungu kwa kujitoa kabisa.

Watu wengi waliooana wanaongoza mambo yao kana kwamba ndoa yao ndilo jambo lenye maana peke yake katika maisha. Wanashughulika sana na kuwapendeza wenzi wao hata mambo ya kiroho yanaachwa. Lakini, mume Mkristo anafahamu kwamba ni lazima uhusiano wake na Mungu utangulie katika maisha yake. Yampasa aishi kwa kujitoa kabisa kwa Yehova. (Rum. 14:8) Yampasa ampende Mungu kabisa kama wale wasiooa na wasioolewa. Bila kujali yanayoweza kutukia, haimpasi aruhusu ndoa yake izuie asimtumikie Mungu kwa kufaa kama mwanafunzi aliyejitoa wa Bwana Yesu Kristo. Hili lingepatana na maneno ya Yesu: “Kama mtu akija kwangu naye hamchukii [hampendi kidogo] baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.”​—Luka 14:26; linganisha Mathayo 10:37.

Shauri la Paulo lisifahamike kuwa lamaanisha kwamba yawapasa waume wa Kikristo wawaachilie wake zao, wakiwatendea kana kwamba si watu. Kwa kinyume, Paulo aliwaagiza Wakristo katika Efeso hivi: “Imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza.” (Efe. 5:28, 29) Hivyo haimpasi mume Mkristo akose kuangalia madaraka yake ya ndoa. Walakini, yampasa nyakati zote afuate shauri la Paulo kwa kuweka maisha yake yote juu ya uhusiano wake na Mungu. Haimpasi afanye ndoa yake kuwa ndiyo maisha yake yote bali ahakikishe kwamba ndoa yake yaongeza uhusiano wake na Mungu, kadiri iwezekanavyo.

Shauri lililopewa na mtume Paulo lapaswa pia lionwe kupatana na tumaini la wale alioandikia. Walioandikiwa (waume, wake, na pia watu wasiooa na wasioolewa) walikuwa Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho waliokuwa wamewekewa tumaini la kuungana pamoja na Bwana Yesu Kristo katika mbingu baada ya kufa na kufufuliwa kwao. Hivyo, vifungo vyote vya kidunia, kutia na vifungo vya ndoa, hatimaye vingekoma kabisa, visianzishwe tena. Hakuna huzuni, furaha au mali za kidunia ambazo zingefuatana nao mbinguni. Kwa kuwa ingewapasa kuacha kila kitu chenye asili ya kidunia, haiwapasi waruhusu vitu hivyo viwe vyenye maana sana isivyofaa katika maisha yao.

Halafu, pia, hata wakati wa kuishi kwao duniani, mambo hayangekuwa namna ile ile. Kama mtume Paulo alivyoeleza: “Mambo ya ulimwengu huu yanapita.” Hivyo halikuwa jambo lenye hekima kwa Wakristo kushikamana isivyofaa na uhusiano na mali ambazo hazikuwa za milele. Kama wangefanya hivyo, kupoteza kwao mke, rafiki au hata mali za kimwili kungeweza kuwavunja moyo sana hata kuuacha uhusiano wao wenye thamani na Mungu.​—1 Kor. 7:30, 31.

Leo watumishi wa Yehova Mungu wanaotumaini kupata uzima duniani wanaweza pia kufaidika na shauri la Paulo lililoongozwa na Mungu. Pia, kwa habari yao mali na uhusiano wa kidunia si wa milele. Wakati na matukio yasiyotazamiwa yanawapata watu wote, nyakati nyingine yakiwanyang’anya mali, rafiki na wenzi wa ndoa. Kwa habari ya mali za kimwili, kusiwe mtu wa kumtazamia Yehova kuzihifadhi hizi katika “dhiki kubwa.” Yehova ameahidi kuhifadhi uhai, si mali za kimwili. Basi jambo lenye maana kuu kuliko yote katika maisha ya kila Mkristo lisiwe ndoa, mali au jambo jingine lo lote la kidunia, bali uhusiano wake mzuri na Mungu. Uhai wetu wategemea kudumisha uhusiano huo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki