Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 5/15 kur. 237-238
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kitabu Cha Biblia Namba 28—Ezekieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • “Sasa Mwisho Umekufikia”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Sikiliza—Mlinzi wa Yehova Anena!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 5/15 kur. 237-238

Maswali kutoka kwa Wasomaji

● Alipokuwa uhamishoni Babeli, Ezekieli angewezaje kuwa na wajibu juu ya maisha za watu wa Mungu katika Yerusalemu akiwa “mlinzi kwa nyumba ya Israeli”?​—Eze. 33:7.

Ezekieli alikuwa mmoja wa Waisraeli wale 18,000 ambao Nebukadreza, mfalme wa Babeli, aliwahamisha Yerusalemu akawapeleka Babeli mwaka 617 K.W.K. (2 Fal. 24:14-16) Hilo lilitukia miaka kumi kabla ya uharibifu kamili wa Yerusalemu mwaka 607 K.W.K., wakati ambao Waisraeli wengi zaidi walipelekwa Babeli wakiwa mateka.

Njia za kupashana habari kwa kutumia wajumbe na barua kati ya miji mikuu ya Babeli na Yerusalemu zilikuwa nzuri kulingana na mahitaji ya siku hizo na umbali uliohusika. (Eze. 21:7; 33:21; 2 Fal. 25:8-10) Ilikuwako misafara ya kawaida katika njia za kufanyia biashara za Eneo lenye Rutuba, ambayo ingeweza kupeleka habari na ujumbe kati ya Yerusalemu na Babeli. (Linganisha Mwanzo 11:31; 12:1-5; Ezekieli 27:3, 17-24.) Mambo ambayo Ezekieli aliona katika njozi na kuyatenda Babeli (Eze. 24:24), na hata yaliyosemwa na manabii wa uongo katika mji huo, yalijulikana Yerusalemu. (Yer. 29:20-23) Vivyo hivyo, mambo ambayo nabii Yeremia alitangaza akiwa huko huko Yerusalemu yalijulikana vyepesi na wahamishwa Waisraeli waliokuwa Babeli.​—Yer. 29:1.

Kwa hiyo, Ezekieli alipofanya ishara za kuonya wahamishwa katika Babeli, habari hizo zilifika Yerusalemu kwa urefu. Ilikuwako njozi ya machukizo yaliyoonekana hekaluni (Eze. 8:1-18), maelezo juu ya mtu aliyevaa kitani mwenye kutia alama katika vipaji vya nyuso za watu waliokuwa wakipiga kite Yerusalemu (Eze. 9:1-11), na tangazo lililotolewa kuhusu Yerusalemu lililoandikwa katika Ezekieli 12:10-16.

Hivyo, Waisraeli katika Babeli na Yuda pia walionywa rasmi na Yehova. Basi, Ezekieli hakuwa ‘mlinzi mwaminifu tu kwa nyumba ya Israeli,’ bali pia alijiondolea hatia ya damu ya maelfu waliouawa mwaka 607 K.W.K. (Eze. 3:17-19; 33:9) Vivyo hivyo leo, Mashahidi wa Yehova wa jamii ya Ezekieli iliyotiwa mafuta na wa “mkutano mkubwa” wanajiepusha na hatia ya damu kwa kutangaza ulimwenguni “siku ya kisasi” cha Yehova, kwa sababu wanawahubiri wakaaji wa dunia onyo la Yehova.​—Isa. 61:3; Mt. 24:14.

Hekima ya Yehova yaonekana katika yote hayo. Kwa sababu ya Ezekieli kufanya utumishi wake wenye utajiri wa kiroho katika Babeli, wahamishwa fulani waliokuwa huko wangewekwa katika hali ya kuendelea kuwa hai kiroho kwa ajili ya utendaji wa wakati ujao, zaidi ya kuonywa habari za hukumu za Yehova juu ya Yerusalemu wenye kuasi imani. Jinsi gani hivyo? Yehova alikusudia kurudisha mabaki hao matajiri wa kiroho katika nchi ya Israeli wakiwa kama “miti” iliyopata nguvu mpya, baada ya miaka 70. (Isa. 61:3) Ni kweli kwamba wahamishwa wengi hawakumsikiliza sana Ezekieli. Watu hao walishangaa sana walipoletewa uhakikisho wa kwamba Yerusalemu ulikuwa umeharibiwa kweli. Walishtuka mno kwa sababu kutoamini kuliwazuia wasiwe tayari kuyasikia mambo hayo. Lakini, walilazimika kukubali kwamba kweli Ezekieli alikuwa amekuwa nabii wa kweli katikati yao. Bila shaka jambo hilo lenye kushangaza sana lilifufua kiroho wengi ambao wangetiwa nguvu kiroho pamoja na watoto wao wawe kama “tini nzuri” ambazo Yeremia alitabiri zingerudi Israeli kufanyiza “nchi mpya” iliyokusudiwa kuanzwa baada ya mwaka 537 K.W.K.​—Yer. 24:1-7; 28:4; Isa. 65:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki