Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 2/1 uku. 22
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NI HEKIMA GANI ILIYO YA MAANA?
  • Je, Unatimiza Wajibu Wako Wote kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kitabu Cha Biblia Namba 21—Mhubiri
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Mhubiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 2/1 uku. 22

Mwenye Hekima Alikuwa na Maana Gani?

NI HEKIMA GANI ILIYO YA MAANA?

Baada ya uchunguzi kamili wa mambo yote ya kibinadamu, Mfalme Sulemani aliandika yale aliyoyaona. Kwa habari ya jitihada zake za kusaidia wengine wafaidike na uchunguzi wake, yeye aliandika hivi: “Walakini, kwa sababu huyo Mhubiri alikuwa na hekima, aliendelea kuwafundisha watu maarifa; naam, akatafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi. Huyo Mhubiri akatafuta-tafuta ili apate kuona maneno yapendezayo, na yale yaliyoandikwa kwa unyofu, yaani, maneno ya kweli.”​—⁠Mhu. 12:9, 10.

Mhubiri 12:9 na 10 katika Septuagint Version ya Kigiriki linasomwa hivi: “Na zaidi ya hayo, kwa kuwa mhubiri alikuwa mwenye hekima, kwa kuwa aliwafundisha wanadamu hekima; ili sikio lipate yaliyo mema katika mithali, mhubiri alifanya uchunguzi wa bidii apate maneno yenye kupendeza na kuandika maneno ya kweli.” (Thomson; 1 Fal. 4:29-34; tazama pia The New English Bible pamoja na kitabu cha maelezo cha Ginsburg). Katika maandishi yake yeye alijaribu kufikia wasomaji kwa maneno yenye kupendeza, kwa habari zenye kupendeza na zenye maana kweli kweli. Kwa kuwa alisaidiwa na roho ya Mungu, sisi leo tunaweza kukubali aliyopata kuona Sulemani bila kuwa na mashaka. Licha ya hayo, yamelipita jaribu la wakati.

Sulemani alifikia uamuzi gani kwa habari ya vitabu vingi vilivyokuwako siku zake? Anaandika hivi: “Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja. Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.”​—⁠Mhu. 12:​11, 12.

Kwa hiyo, maandishi yenye faida zaidi ni yale yanayoonyesha hekima ya “mchungaji mmoja,” Yehova Mungu. Walakini, kujishughulisha kupita kiasi na vyanzo vingine vya mafundisho kunaweza kuchosha mtu bure, bila kupata faida yo yote yenye maana au yenye kudumu. Sana sana wakati maandishi hayo yanapokuwa yameandikwa kwa akili za wanadamu, na yawe yanapingana na hekima ya kimungu, yanakuwa yasiyofaa nayo yanaangamiza imani. Kwa upande mwingine, maneno ya wale walio na hekima ya kimungu, kama vile michokoo, yatachoma masikio ya wasikilizaji au wasomaji wasonge mbele kulingana na hekima iliyomo. Vilevile, wale wanaojishughulisha katika kukusanya mafungu ya maneno, yaani, mithali zinazofaa kweli kweli na zenye hekima, ni kama misumari. Hii yaweza kuwa hivyo kwa sababu maneno yao mema, yanayoonyesha hekima ya Yehova Mungu, yanaweza kutegemeza wasikilizaji.

Akitoa muhtasari wa uchunguzi wake wote, Sulemani anasema hivi: “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu. Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.” (Mhu. 12:​13, 14) Woga unaofaa au heshima kwa Muumba itatulinda tusichukue mwendo wa maisha wa upumbavu unaoweza kutuletea taabu kubwa sana. Vilevile, kufahamu kwamba hakuna jambo lisiloonekana machoni pa Muumba kunaweza kutushawishi tutii amri zake. Aliye Juu Zaidi atahukumu mambo yote, kutia na yale yanayofichwa wanadamu. Kwa kuwa amri zake zimekusudiwa ziongeze hali yetu njema ya milele, je! si jambo linalofaa tena la hekima kweli kweli kuzishika?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki