Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 8/1 kur. 23-24
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Baba na Mzee—Kutimiza Mafungu Yote Mawili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Watumishi wa Huduma Hufanya Utumishi Muhimu
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kudumisha Upatano Kati ya Wazee na Watumishi wa Huduma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je! Wewe Wastahili Kutumikia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 8/1 kur. 23-24

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Ikiwa watoto katika jamaa ya wazee au watumishi wa huduma ‘wanashitakiwa kuwa ni wafisadi,’ ni jambo gani linaloamua kama kichwa cha jamaa kitaendelea kutumikia katika cheo kundini?

Maandiko yanaonyesha wazi sana kwamba wanaume waliooa wanaotumikia kundini wamepaswa wawe vichwa vya jamaa vyenye mfano mwema. Tunasoma hivi: “Kwa hiyo imempasa mwangalizi awe . . . mwanamume mwenye kusimamia nyumba yake mwenyewe katika adabu nzuri, mwenye kutiisha watoto kwa uzito wote; (ikiwa kweli mwanamume ye yote hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, yeye ataliangaliaje kundi la Mungu?).” (1 Tim. 3:2, 4, 5, NW) “Watumishi wa huduma na wawe waume wa mke mmoja, wenye kusimamia katika adabu nzuri watoto na nyumba zao wenyewe.”​—⁠1 Tim. 3:12, NW.

Kundi lina haki ya kutazamia wazee, watumishi wa huduma na jamaa zao kuwa mifano myema ya maisha ya Kikristo. (Linganisha 1 Timotheo 1:12; 1 Petro 5:3.) Ikiwa haiwi hivyo, inaweza kuwa na matokeo ya kuharibu hali ya kiroho ya kundi. Kwa mfano, ikiwa watoto wa wazee na watumishi wa huduma hawafuati kanuni za Maandiko, hilo laweza kufanya watoto wengine katika kundi wafanye vivyo hivyo na kutetea mwenendo wao mbaya. (Linganisha 1 Wakorintho 8:9-13; 10:31, 32.) Hali inakuwa nzito hata zaidi wakati watoto wa wazee na watumishi wa huduma wanapotenda makosa mazito.

Basi, watoto hao wanapoaibisha jamaa na kundi, imeipasa baraza ya wazee iamue kama baba anastahili kuendelea kutumikia kama mzee au kama mtumishi wa huduma. Maoni yake mwenyewe ya kwamba anastahili kutumikia ijapokuwa mambo ambayo yametukia katika jamaa yake hayatageuza uamuzi uliofikiwa na baraza ya wazee.

Ili mwanamume aendelee kutumikia, umepaswa uweko ushuhuda unaoonyesha kwamba anaweza kuipa jamaa yake msaada wa kiroho wanaohitaji na kwamba hakukosa kufanya hivyo. Baba aliye macho anaweza kwa kawaida kuchunguza magumu yaliyo katika jamaa yake wakati hayajaendelea zaidi. Akiwa mwanamume anayejua namna ya kusimamia nyumba yake, anaweza kuchukua hatua za kuzuia hali zisizofaa katika jamaa yake. Ijapokuwa watoto wake wanaweza kufanya makosa, imempasa awe na uwezo wa kuwaongoza na kuwaadibisha kama inavyotakiwa ili wasiwe “wafisadi.”​—⁠Tito 1:6.

Bila shaka, zaweza kuwako nyakati mtoto anapoiacha kweli au anapotumbukia katika kosa ijapokuwa baba anafanya bidii inayofaa kusaidia jamaa yake kiroho. Huenda watoto wake wengine wakawa mifano mizuri katika maisha ya Kikristo, wakishuhudia kwamba wanapokea mafundisho mema kutoka kwa wazazi wao. Kwa upande mwingine, mtoto mchanga baada ya mwingine mwenye umri fulani akipata magumu ya kiroho anapokaa nyumbani pamoja na wazazi, na jambo hilo linaleta suto juu ya jamaa na kundi, hapo pana shaka juu ya kama baba ‘anasimamia nyumba yake katika njia nzuri.’ Ni lazima kutumia uangalifu hali hiyo isiachiliwe kwa kutoa mifano ya Maandiko inayoonyesha watoto waliogeuka wakawa wabaya, kutia na Esau, wana wa Samweli na wanaofanana na hao. (Mwa. 25:27-34; 26:34, 35; 1 Sam. 8:2, 3, 5) Na ikumbukwe kwamba wengi kati ya wale wanaotajwa katika Biblia kuwa walipotoka, walikuwa watu wazima walio na uwezo wa kujifanyia maamuzi wenyewe. Hawakuwa chini ya mamlaka ile ile na uongozi ule ule kama watoto wadogo walio katika nyumba tunaozungumza hapa.

Kwa sababu ya hatari ya kiroho inayoweza kutokea kwenye kundi wakati watoto wa wazee au watumishi wa huduma wanapofanya makosa mazito, wanaume wenye watoto hao wamepaswa washirikiane sana na baraza ya wazee katika kuchunguza mambo ya hakika. Haiwapasi waone kosa hilo la watoto wao kuwa dogo au kujaribu kulificha ili waendelea na cheo chao. Imewapasa vilevile waepuke kukasirikia watoto isivyofaa. (Efe. 6:4) Akina baba hawa wamepaswa wapendezwe sana katika kusaidia kiroho watoto wao wapotovu kwa kadiri hali zitakavyoruhusu. Jambo la kwanza kufikiriwa limepaswa liwe hali ya kiroho ya jamaa yao si kufikiria kama wanaweza kuendelea kutumikia katika cheo ama sivyo,​—⁠ Linganisha 1 Timotheo 5:8.

Kwa sababu hiyo, ikiwa kosa zito la watoto walio katika jamaa hiyo linatokeza mashaka mazito katika kundi juu ya kama mwanamume anasimamia jamaa yake katika njia nzuri, haimpasi aendelee kutumikia kama mzee au mtumishi wa huduma. Mwanamume anapotumika kama mzee na wazee wenzake wanaruhusu urafiki au maono fulani yapotoe hukumu na uamuzi wao na kukosa kufuata kanuni za Maandiko, kuendelea kwake kutumika kama mzee, ijapokuwa hastahili, kunaweza kuharibu kundi kiroho. Sababu ni kwamba hilo laweza kuvunja heshima ya baraza nzima ya wazee. Linaweza kuwapa watoto wengine katika kundi sababu ya kufanya makosa. Hivyo, inafaa kukumbuka kwamba uwezo wa mwanamume huyo kama mtoaji wa hotuba au kama mtu anayejua kupanga mambo vizuri wala hali yake yenye kupendeza watu silo jambo linaloamua. Jambo linaloamua ni kama anatimiza daraka lake katika njia nzuri kama baba. Anaweza kuendelea kutumika ikiwa anatimiza hayo tu. Bila shaka, inapokuwa hivyo, baraza ya wazee imepaswa iepuke kumlaumu isivyofaa wakati wanapochunguza hali ya jamaa yake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki