Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 9/15 kur. 10-16
  • Tumaini la Viumbe—Latazamia Kutimizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumaini la Viumbe—Latazamia Kutimizwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MUNGU ATOA TUMAINI
  • KUUMBA KWA KIBINADAMU ‘KULITIISHWA KATIKA UBATLI’ KUKIWA NA TUMAINI LA KUWEKWA HURU
  • Matazamio ya Paradiso Ni Halali Kujapokuwako Kutotii kwa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Adui wa Mwisho, Kifo, Aangamizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Twaweza Kujifunza Kutokana na Wenzi Wawili wa Kwanza wa Kibinadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kwa Nini Ni Muhimu Kujua Yaliyotukia Edeni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 9/15 kur. 10-16

Tumaini la Viumbe​—Latazamia Kutimizwa

“Tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.”​—Rum. 8:20, 21.

1, 2. Sisi tunatofautianaje na walimwengu ‘wanaotumaini bila tumaini’ kwa habari ya kuumba kwa kibinadamu?

TUMAINI kwa wanadamu laonekana kuwa kazi bure! Watu wengi wanadhani hivyo.

2 Hata hivyo kuna wengine ‘wanaotumaini bila tumaini.’ Yaani, wanatumaini bila msingi wa kutazamia utimizo. Walakini, sisi tunatumaini tukiwa na msingi imara wa kutazamia kutimizwa kwa tumaini letu tukufu. Kwa habari hii twafanana na mwanamume mmoja wa nyakati za kale.

3. Kwa habari ya jambo hili, tunafanana na nani, nalo tumaini la mzee huyo wa ukoo wa kale lililokuwa na msingi mzuri lilitimizwaje?

3 Mwanamume huyo alikuwa mtu wa kutoka Mashariki aliyeitwa Ibrahimu, ambaye kwanza aliishi katika nchi inayoitwa sasa Iraq. Akiliamini tumaini la pekee lililowekwa mbele yake, alihamia kwenye ujirani wa mji mdogo uitwao Beer-Sheba, kuelekea kaskazini mwa Sinai, nchi iliyozungukwa na bahari karibu pande zote. Kwa habari ya Ibrahimu, tumaini la mataifa fulani lilishikamanishwa na kuzaliwa kwa kitoto kivulana kupitia kwa mke wake Sara. Miaka 99 ya kuishi ilikuwa imepita juu yake, na 89 juu ya mke wake. Kwa kawaida, umri mkubwa wa uzee ungekuwa umeharibu matumaini yao ya kuzaliwa kwa mwana. Walakini Ibrahimu alikuwa amepewa ahadi hiyo na Mtu asiyekosa kutimiza ahadi yake, yaani, Mungu wake, Yehova. Basi, Ibrahimu alifanya nini? Alilishikilia tumaini alilopewa na Mungu. Maandishi ya kihistoria katika Biblia yasema: “Abrahamu aliamini na kutumaini ingawa hali yenyewe ilikuwa bila matumaini, na hivyo amekuwa baba wa mataifa mengi kama Maandiko matakatifu yalivyosema [kama ilivyokuwa imesemwa (na Mungu); Ndivyo uzao wako utakavyokuwa].” (Rom. 4:18, HNWW) Tumaini la Ibrahimu halikukosa kutimizwa, kwa kuwa Isaka mwanawe, alizaliwa kimwujiza kwa mke wake Sara. Kutokana na kuzaliwa huko mataifa yalitokea!

4. (a) Kuumba kote kwa kibinadamu kumeshikamanishwa na nini, na wala si wale tu wanaoishi sasa lakini hata wale wa kurudi nyuma mpaka wakati gani? (b) Ni maulizo gani yanayotokea kwa habari ya mwanamume wa kwanza alipokuwa akiishi peke yake katika makao yake ya kidunia?

4 Leo kuumba kote kwa kibinadamu kumeshikamanishwa na tumaini lililotolewa na Mungu! Linahusu, si idadi tu ya watu wanaoishi duniani wakati huu, bali kuumba kote kwa kibinadamu tangu uzao wa moja kwa moja wa mwanamume wa kwanza duniani, Adamu. Kwa sifa ya Muumba wake, mwanamume huyo wa kwanza alitokezwa akiwa mkamilifu kabisa katika mwili na akili. Aliwekwa katika makao makamilifu ya kidunia, bustani ya Edeni, pamoja na misaada yote ya kuendeleza uhai mkamilifu wa kibinadamu katika furaha. Muumba wake, Baba yake wa kimbinguni, alikuwa rafiki yake, akizungumza naye kwa ukawaida kutoka katika makao yasiyoonekana. Zaidi ya hayo, akiwa na wanyama wote wa nchi kavu, ndege na samaki kumzunguka katika bustani ya Edeni, Adamu alikuwa na vitu vingi vya kumzuia asiwe mpweke. Walakini kwa nini Baba wa kimbinguni wa Adamu alimweka katika Paradiso hiyo ya kupendeza? Awe mtunza msitu au mtunza bustani mpweke? Alikuwa amekusudiwa aishi na kufurahia muda mrefu kadiri gani wema huu wote kutoka kwa Mtoaji-Uzima wake?

5. Majibu ya maulizo hayo yalimtegemea mtu yupi mmoja, nalo ni shauri gani lililofaa ambalo Adamu aliyekuwa mkamilifu angeweza kukumbuka?

5 Adamu alijulishwa kwamba kila kitu kilimtegemea yeye! Akiwa na kumbukumbu lake kamilifu Adamu asingeweza kusahau kamwe shauri ambalo Baba yake wa kimbinguni alimpa: “Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.​—Mwa. 2:16, 17,

6. Amri hiyo ya kimungu iliwafungulia wanadamu jambo gani, nao wazao ya Adamu wangetokeaje?

6 Amri hiyo ya kimungu ilimfungulia Adamu njia ya kuishi milele, ikiwa hivyo ndivyo Mungu alivyotaka afanye. Kama ambavyo maandishi yanaonyesha baadaye, Adamu aliishi miaka 930, walakini angeweza kuishi wakati mwingi zaidi usiojulikana. Ndiye aliyefanya sisi tuwe tunakufa leo. Kama sote tunavyopaswa kutambua, mwanamume huyo wa kwanza duniani alikuwa na uzao; ama sivyo tusingepaswa kuwa hapa. Walakini haikuwa kwa njia isiyo ya kibinadamu ambayo wenye kufanya majaribio ya kisayansi leo huita kutokeza jamaa bila ya kufanya ngono, kama ilivyo kwa mimea fulani. Badala yake, kama ilivyo kwa ndege na wanyama wa nchi kavu Mungu alimwumbia mwenzi wa kike, mke, akachukua ubavu kutoka kwa upande mmoja wa Adamu ili akuanzishe kuumba kwake. Baada ya kumwoza mwanamume wa kwanza kwa mwanamke wa kwanza duniani, Mungu aliweka mbele yao tumaini la uzima usio na mwisho juu ya dunia ya paradiso. Aliwabariki na kuwaambia wazae namna yao kusudi dunia yote ijazwe, ambayo paradiso yao ingeenezwa.​—Mwa. 2:18-24; 1:26-28.

7. Ni hali gani ya mambo ya wanadamu ambayo Adamu na Hawa hawakutazamia itokee, na kwa sababu gani nyoka hapaswi kulaumiwa kwa sababu ya mwendo wa mambo ya wanadamu?

7 Tazamio la wanadamu wote wakati huo lilikuwa lenye kutumainisha sana. Adamu na Hawa hawakutazamia kuona wazao wao ‘wakiugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja’ kwa sababu ya hali ya kimwili, kiadili na kijamii ambayo katika hiyo tumo leo. Kwa kutokutii na kula matunda ya mti wa kujua mema na mabaya huenda ingeonekana kuwa kama kitu kadogo tu, walakini hako ndiko kalitokeza hali ya sasa. Kwa kula kidhambi, kwanza Hawa, kisha Adamu, wakaharibu tumaini lao walilopewa na Mungu, wakati wangali hawana watoto. Kama Mungu asingejiingiza kwa njia fulani, sisi leo tungekuwa hoi kabisa. Ni kweli, nyoka katika Edeni alihusika na yaliyotokea, walakini tusimwekelee lawama yote kiumbe huyo mtambaazi. Mahali pake, Biblia inatutajia roho asiyeonekana aliyekuwa na hila ya kuongoza nyoka huyo. Alikuwa nani? Malaika wa kimbinguni, ambaye alikuwa ameazimia kupotoa Adamu na Hawa wasimfanye Yehova Mungu tumaini lao.

8. Hawa alishawishwa akafanya jambo gani, na ni kwa sababu gani sisi leo hatujikuti tukiwa katika ile bustani ya Edeni ya kwanza?

8 Mfanya hila huyo mwasi aliyezungumza kupitia kwa nyoka, alimdanganya Hawa ajaribu kujifanya kuwa kama Mungu. Akiwa hivyo, angeweza kujifanyia tumaini lake mwenyewe alilojichagulia. Mpaka wakati huo mume wake Adamu, alikuwa amekuwa nabii wa Mungu kwake. Adamu alikuwa ametenda kama mnenaji wa Mungu katika kumwambia Hawa juu ya amri ya Mungu ya kutokula tunda lililokatazwa. Walakini baada ya kujifanyia mradi wa kujifanya mwenyewe kuwa mungu-mke kwa kula tunda lililokatazwa, Hawa alijifanya kuwa nabii-mke wa nyoka kwa kutumia sauti yake nzuri amshawishi Adamu, ajiunge naye katika kuasi. Mwishowe, kwa sababu za kumvunjia Mungu heshima, Adamu ‘alisikiliza sauti ya mke wake,’ nabii-mke mwongo. (Mwa. 3:17) Kwa sababu hiyo Yehova Mungu alitoa hukumu ya haki ya kifo juu ya nabii Wake asiyekuwa mwaminifu, Adamu. Mke wake, Hawa, akahukumiwa hivyo. Sasa wakiwa kama wamekufa, walifukuzwa kutoka katika bustani ya Edeni wapate kuishi nje katika ardhi isiyolimwa muda wote wa maisha. Sote, tukiwa bado kuzaliwa katika viungo vya uzazi vya Adamu na Hawa, tulifukuzwa pamoja nao.

9. Je! wanadamu wawili waliotenda dhambi kwa kukusudia waliwekewa tumaini tofauti na lile lililokuwa limeonyeshwa katika amri ya Mungu aliyokuwa amepewa Adamu, nayo hali iliachwaje kwa habari yetu sisi tulio wazao wao?

9 Wavunja-sheria hao wa kukusudia, Adamu na Hawa, hawakuwekewa tazamio tofauti na lile lililotolewa katika amri ya Mungu aliyompa Adamu. Kwa kufaa, hakuna tumaini lililowekwa mbele yao, kwa sababu walitupilia mbali tumaini la awali lililotolewa na Mungu. Walakini, je! mambo yaliachwa bila tumaini kwetu sote, sisi wazao wasiohusika? Kwa furaha yetu, Hasha!

MUNGU ATOA TUMAINI

10. Ni nani aliyekuwa wa kwanza kuhukumiwa huko Edeni, naye alikuja kuitwaje, nalo ni jambo gani ambalo lingempata katika vita hiyo iliyotabiriwa?

10 Maneno ya tumaini hayakuelekezwa kwa Adamu na Hawa binafsi; wao waliyasikia tu. Maneno ya Mungu yaliyokuwa na msingi kwetu kuwa na tumaini yalielekezwa kwa roho mwasi ambaye kwa ujanja alimtumia nyoka katika kumshawishi Hawa awe nabii wake wa kike mwenye kufaulu. Huyo alishutumiwa kwa kupewa jina Shetani Ibilisi. Kwa sababu ya kuanzisha mwendo wa ujanja na hila kwa kusudi la kudanganya, hata kumtumia nyoka katika Edeni, vilevile yeye aliitwa “nyoka wa zamani.” (Ufu. 12:9; 20:2) Kiumbe huyo wa kiroho mwenye kujifanya kuwa kamungu, ambaye alikuwa wa kwanza kusema uongo juu ya Mungu na juu ya mwanamke, ndiye aliyekuwa wa kwanza kupata hukumu kutoka kwa Mungu katika Edeni. Juu yake Mungu alitamka laana yake, kisha akatabiri vita ambavyo katika hivyo “nyoka wa zamani” huyo na wale wanaosimama upande mmoja naye katika mzozo huo wangeshindwa.

11. Maneno yaliyoelekezwa kwa “nyoka wa zamani” yalitoaje tumaini kwa wazao wa Adamu na Hawa?

11 Kwa huyo “nyoka wa zamani” Mungu alisema: “Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” (Mwa. 3:14, 15) Hii maana yake ilikuwa kuangamizwa kwa huyo “nyoka wa zamani” na uzao wake. Walakini, je! hukumu hii ya Mungu iliacha msingi wa tumaini kwa ajili ya wazao wa wakati ujao wa Adamu na Hawa? Hasha, si moja kwa moja, bali kwa kudokezea au kukata shauri tu.

12. Maneno ya Mungu kwa Shetani yalimleta “mwanamke” wa namna gani katika kisa hicho, na ni kwa sababu gani Mariamu mama ya Yesu Kristo hangefaa kuwa “mwanamke” huyo?

12 Aha! mwanamke aingizwa katika habari hii. Yeye angekuwa nani? Alipaswa kuwa yule ambaye angeonyesha “nyoka wa zamani” na uzao wake uadui, chuki. Hawa, ambaye alikuwa amejifanya nabii-mke wa uongo wa huyo “nyoka wa zamani,” asingeweza kufaa. Alishawishwa kuamini kwamba Yehova Mungu alikuwa mwongo. Hata Mariamu, mama wa Yesu Kristo, asingeweza kufaa. Miaka elfu nne ingepita kabla ya msichana huyo Myahudi kuzaliwa kama mzao wa Ibrahimu na akiwa chini ya Torati ya Kiyahudi. Mwana wake wa kwanza Yesu aliishi duniani miaka 33 1⁄2 peke yake. Wakati mama yake wa kidunia alipoona aliyofanya “nyoka wa zamani” atendewe mwana huyo aliyetolewa kwa mwujiza huko Kalvari, alikuwa amekwisha kuishi sehemu iliyokuwa ndefu zaidi ya maisha yake. Kwa hiyo yeye mwenyewe angaliweza kuonyesha uadui kwa huyo “nyoka wa zamani” kwa makumi machache tu ya miaka ya kuishi.

13. “Mwanamke” huyo aliyetajwa angeweza kuwa nani au nini, naye alifurahia kuwekwa katika hali gani kuhusiana na huyo nyoka wa mfano na uzao wake?

13 Ni jambo la akili kwamba, “mwanamke” wa unabii wa Mungu angekuwa yeye aliyekuwa hai na akisikiliza wakati Mungu alipomzungumzia “nyoka wa zamani” katika Edeni. “Mwanamke” huyo wa mfano angeishi muda mrefu zaidi baada ya kufa kwa Hawa, ndiyo, mpaka wakati wa Mungu wa kumfanya “mwanamke” huyo atokeze “uzao” ulioahidiwa, ambao ulitokea zaidi ya miaka elfu tatu baada ya kufa kwa Hawa. Kwa hiyo, “mwanamke” huyo wa mfano hangeweza kuwa mwingine isipokuwa “mwanamke” wa Mungu mwenyewe, yaani, tengenezo lake la kimbinguni la viumbe vitakatifu vya kiroho, vilivyokataa kujiunga na “nyoka wa zamani” katika uasi wake. Waliheshimu ndoa ya Mungu aliyofanya na tengenezo lake jaminifu la ulimwengu wote, nao hawakujitaliki kutoka Kwake wajiunge na tengenezo ambalo lingeolewa na “nyoka wa zamani.” Walifurahia sana kwa vile Mungu alivyoweka uadui kati yao na “uzao” uliotengenezwa wa “nyoka wa zamani.”

14. (a) Hivyo ni tazamio gani lililowekwa mbele ya “mwanamke” huyo pamoja na jambo gani la baadaye linalowapata wanawake wote? (b) Je! sisi tulizaliwa tukiwa na uhusiano wa kuwa watoto wa Mungu, na hata hivyo ni tumaini gani ambalo limewekwa mbele ya wanadamu?

14 Basi, katika Edeni, Mungu aliweka taraja la kuwa mama watoto mbele ya tengenezo lake la kimbinguni lililo kama mke. Kuanzia wakati huo na kuendelea angeweza kutumaini kuwa mama wa “uzao” ambao Bwana wake Yehova Mungu, angekuwa Baba yake. Kutimizwa kwa tumaini hilo kulifaa kungojewe na “mwanamke” wake muda wa miaka 4,000. Mwanamke huyo alikuwa na nia ya kuvumilia utungu wo wote wa kuzaa ambao ungeletwa na hilo, kama vile ilivyo kwa habari ya mwanamke wa mfano anayeonwa katika njozi inayosimuliwa na mtume Mkristo Yohana katika Ufunuo 12:1-5. Kwa sababu kuwa mama watoto ndiyo tamaa ya kawaida wanawake wote ambao ni wazima. Kwa sababu gani asiweke hali ya kuwa mama watoto mbele ya tengenezo la Mungu la kimbinguni la namna ya “mwanamke”? Kwa kufaa tumaini la kuwa mama watoto lilitolewa kwa “mwanamke” wa Mungu kabla ya Mungu kumruhusu kwa rehema Hawa, mke wa Adamu aliye sasa mwenye dhambi, kuwa mama watoto nje ya Edeni. Walakini Mungu hakutoa baraka kwa kumwambia Hawa mkosaji hivi: “Nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto.” (Mwa. 3:16 kwa kutofautisha na 1:28) Kwa kupitishia wazao wao habari ya unabii wa Mungu kuhusu “uzao” wa “mwanamke,” Adamu hakutenda kama nabii wa Mungu; wala mke wake, Hawa, hakutenda kama nabii-mke wa Mungu. Adamu na Hawa wawe waliamini ahadi ya Mungu iliyoandikwa katika Mwanzo 3:15 au hapana, Mungu alitaka wazao wao waweke tumaini juu ya msingi wa ahadi hiyo. Ijapokuwa Adamu aliumbwa kama “mwana wa Mungu,” sisi, wazao wake wasiokamilika, wenye dhambi, hatukuzaliwa na hali ya kuwa wana wa Yehova Mungu. (Luka 3:38, NW) Kwa hiyo, kwa asili sisi hatuwi na ushuhuda wa roho takatifu ya Mungu, kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Hata hivyo, je! tuna tumaini lo lote la kurudi tena kwenye jamaa ya Mungu ya wana? Naam, lipo!

15. Uhakika wa kwamba leo kuna zaidi ya wanadamu milioni 4,000 ambao wangali wakiishi duniani unaonyesha nini kwa habari ya wanadamu?

15 Ikiwa tusingekuwa na tumaini, kwa nini Mungu aliruhusu walio wengi sana kati yetu wazaliwe na Adamu na Hawa—zaidi ya vizazi 100 kufikia sasa? Leo, baada ya vita vyote na misiba mingine zaidi ya magonjwa na kifo cha kawaida, kuna mamilioni ya sisi tulio hai zaidi ya milioni 4,200, na inatabiriwa kwamba kufikia mwaka 2000 W.K., kutakuwako duniani wanadamu milioni 6,000. Je! yote hayo yamekuwa kazi bure? Kwa wazi, hapana!

16. (a) Kwa sababu ya kutojiweza kwa wanadamu, kutimizwa kwa tumaini la kuumba kunategemea uwezo wa nani wa kutenda? (b) Ni kuzaliwa na maisha ya nani duniani yaliyopata kuwa tukio kubwa katika historia ya wanadamu?

16 Bila shaka, mwanadamu hawezi kujiokoa kwa uwezo wake. Hata hivyo, habari hii ya kuumba kwa kibinadamu ina tumaini, ijapokuwa hali ya mambo isiyotumainisha. Hii si kwa sababu ya jambo lo lote ambalo wanadamu wenyewe wanaweza kufanya, bali msingi wake imara ni yale ambayo Mungu amekwisha kufanya na yale ambayo atafanya kulingana na ahadi yake isiyoweza kuvunjwa. Kwa sababu Mungu aliruhusu vizazi kama 70 vizaliwe kutokana na Adamu na Hawa, jambo hilo liliruhusu Mwanawe kutoka mbinguni azaliwe awe mwanadamu Yesu Kristo. Akiwa duniani, Mwana huyu wa Mungu alitimiza mapenzi ya Mungu kwa ajili ya faida ya wanadamu wote. Hii ilitokeza jambo kuu katika historia yetu sisi wanadamu!

KUUMBA KWA KIBINADAMU ‘KULITIISHWA KATIKA UBATLI’ KUKIWA NA TUMAINI LA KUWEKWA HURU

17. Katika Warumi 8:19-24, mtume Paulo aliandika nini kwa habari ya kutiishwa kwa wanadamu katika ubatili wa kujitahidi kwao na kwa habari ya kuumba kukingojea nini kwa kuugua?

17 Miaka 23 baada ya Yesu Kristo kumaliza mwendo wake wa kidunia na kupaa kurudi mbinguni, mtume Mkristo Paulo aliandikia kundi lililokuwa katika Rumi, Italia, na kusema: “Kwa maana viumbe vyote [vya kibinadamu] pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha katika tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu. Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa. Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho, sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia kufanywa wana, yaani, ukombozi wa mwili wetu. Kwa maana tuliokolewa kwa [tumaini].”—Rum. 8:19-24.

18. (a) Ni nani aliyevitiisha viumbe vyote vya kibinadamu katika ubatili, na kwa namna gani? (b)  Matengenezo ya wanadamu yametufikisha wapi leo, na je! yale yanayotazamiwa kutokea yaweza kuelezwa kuwa ‘tazamio la shauku’ la viumbe vyenye kuugua?

18 Yule ambaye kupitia kwake kuumba kwa kibinadamu kulitiishwa chini ya ubatili ni Mungu. Hatukutiishwa chini yake kwa mapenzi yetu wenyewe, kama vile tusivyotaka kwa mapenzi yetu tuzaliwe. Mungu alipenda tuzaliwe, ajapowahukumia Adamu na Hawa kifo. (Mwa. 3:16-24; 5:1-4) Hata hivyo, hatukuzaliwa na “utukufu” ambao Adamu na Hawa walikuwa nao hapo kwanza katika bustani ya Edeni kama “wana wa Mungu.” Sisi tulizaliwa katika “utumwa wa uharibifu,” chini ya laana ya wazao wote wa Adamu ya kifo. (Rum. 5:12) Hivyo tusingeweza kujiokoa. Jitihada zetu zote za kujiokoa wenyewe zilikuwa ni ubatili tu. Jitihada zote za serikali za kibinadamu zimetufikisha wapi? Mipango yote ya wanadamu wenye kutaka makuu ya kijamii, kiuchumi, kifedha, kiutabibu na kisayansi, imetufikisha wapi mpaka siku hii? Sote tungali tunapatwa na uharibifu wa akili, mwili na adili. Vilevile, sasa inaonekana kwamba vita vya atomiki pamoja na mizinga ya kulipuka iwezayo kutupwa kutoka bara moja mpaka bara nyingine, ikitoka baharini na kutelemka chini kutoka mawinguni, vitamaanisha mwisho wa ghafula kwetu sisi sote. Je! jambo hilo laweza kuelezwa kuwa ‘tazamio la shauku’ la viumbe vyenye kuugua?

19. Mungu aliwatiisha wanadamu wasiokamilika katika ubatili kwa kusudi gani, naye alifanya hivyo kukiwa na tumaini gani?

19 Hata hivyo, Muumba wa wanadamu mwenyewe hakutiishwa chini ya ubatili. Wanadamu wapotovu hawawezi kuzuia kusudi la Muumba. Hivyo yeye mwenyewe ni tumaini kwetu. Kwa hiyo, anataka tumtumaini yeye, si kujitumaini sisi wenyewe. Sisi sote alitutiisha chini ya kutojiweza kwa kibinadamu, ili tusiwe na msingi wo wote wa kujitumaini wenyewe. Akiwa Chanzo cha pekee cha tumaini, Yeye aliwatiisha wanadamu chini ya ubatili walakini si juu ya msingi usio na tumaini. Badala yake, kama vile Warumi 8:20, 21 lisemavyo, ‘katika tumaini la kwamba viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.’

20. (a) Je! ule unaoitwa “ulimwengu ulio huru” unafurahia “dhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu”? (b) ’Viumbe vyote vinatazamia kwa shauku nyingi’ kufunuliwa kwa nani kufanywe?

20 Leo watawala wenye kufuata siasa za namna fulani wanaweka milki yao katika jamii ya “ulimwengu ulio huru tofauti na watu walio chini ya tawala zilizo tofauti. Walakini, hata madai ya vikundi vya kisiasa vinavyopingana yaweje, hakuna cho chote kilicho na “uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.” Mungu na Baba wa Bwana Yesu Kristo ndiye peke yake anayetolea jamii ya kibinadamu tumaini la kurudishwa kwenye uhusiano ambao Adamu na Hawa walikuwa nao alipowaumba katika Edeni. Walakini, kurudishwa huko kwapaswa kungojee tendo la wakati ujao upande wa Mungu. Jambo lenyewe hilo twalisoma katika maneno ya mtume huyo: “Viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.” (Rum. 8:19) Mtume Paulo ambaye ndiye aliyeandika maneno hayo, alijiweka upande wa hao “watoto wa Mungu,” katika Warumi 8:15-17.

21. Ni nani aliye mkuu wa hawa “wana wa Mungu,” nalo jeraha la kisigino chake liliponywaje, kukiwa na kusudi gani kulingana na Waebrania 2:14, 15?

21 Hao “watoto [wa pekee] wa Mungu,” ndio uzao wa “mwanamke” wa Mungu, kama unavyotajwa katika unabii wa Mungu katika Edeni, katika Mwanzo 3:15. Aliye mkuu wa “uzao” huo wa tengenezo la Mungu la kimbinguni ni Yesu Kristo, yule ambaye Mungu aliruhusu “nyoka wa zamani” amjeruhi katika kisigino wakati wa kifo chake juu ya mti wa mateso katika mwaka 33 W.K. Walakini, Mungu aliponya jeraha hilo la kisigino kwa kumfufua Mwanawe mwaminifu siku ya tatu ya kufa kwake. Kwa kufufuliwa kama Mwana wa Mungu wa kiroho wa kimbinguni, si kama Mwana wa kibinadamu, yeye angeweza kupokelewa na “mwanamke” wa Mungu wa kimbinguni. Huyu atamharibu, kama Waebrania 2:14, 15 lisemavyo, “yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.”

22. Ni nani walio washiriki wadogo wa huo “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu?

22 Washiriki wadogo wa “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu wa mwungano wa jamii ya malaika watakatifu, ni wanafunzi wa Yesu Kristo, wale ambao wanazaliwa kwa roho ya Mungu wawe “watoto wa Mungu” wa kiroho na warithi washirika wa ndugu yao mkubwa, Yesu Kristo, mbinguni.

23. Kulingana na 1 Petro 1:3, 4, Mungu aliwazaa washiriki wadogo wa huo “uzao” wapate tumaini la namna gani, na je! tumaini hilo lingali likitenda kazi katika wakati huu ulioendelea sana?

23 Mtume Petro anazungumza juu ya tumaini lao la kimbinguni kuwa “lenye uzima” anapowaandikia hivi: “Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.” (1 Pet. 1:3, 4) Tumaini lao hili lingali, tumaini “lenye uzima” leo. Halijakufa kwa vile linaonekana kwa mabaki yao duniani kama kwamba limekawia kutimizwa. Wanatazamia kuona tumaini hili likitimizwa karibuni katika wakati wake uliowekwa na Mungu na Baba yao, Yehova. Mtume Paulo atukumbusha Mwanzo 3:15, anapoliandikia kundi lililozaliwa kwa roho katika Rumi, akisema hivi: “Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.”​—Rum. 16:20.

24. Kufunuliwa kwa hawa “wana wa Mungu” kunangojewa na nani kwa shauku nyingi, nako kufunuliwa huko kutatokea baada ya tukio gani?

24 “Kufunuliwa” kwa hawa “wana wa Mungu” pamoja na kwa Mwana aliye mkuu wa Mungu, Yesu Kristo, katika wakati ujao ulio karibu, ‘kunatazamiwa kwa shauku nyingi na viumbe [vya kibinadamu],’ vikikungojea kwa shauku nyingi. Walakini karibuni, kabla ya tukio hilo tunaitazamia “dhiki ile iliyo kuu” ambayo Yehova Mungu, Baba wa kimbinguni ataachilia iwajie wapinzani na watesi wanaowataabisha wana wake wa kiroho pamoja na washiriki wenzao washikamanifu.​—Ufu. 7:14, 15; 2 The. 1:6-10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki