Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 9/1 kur. 3-4
  • Je! Dini Zote Zawaongoza Watu Kwa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Dini Zote Zawaongoza Watu Kwa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SABABU MAONI HAYO YANAPENDWA NA WENGI
  • NA WALE “WENGI” AU NA WALE “WACHACHE”?
  • MAARIFA SAHIHI AMBAYO HUONGOZA KWA MUNGU
  • Je! Kuna Wema Katika Dini Zote?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Je, Dini Zote Ni Barabara Mbalimbali Zinazoongoza kwa Mungu?
    Amkeni!—2001
  • Dini Yako Inapasa Kufikiriwa Sana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Dini Yao Tu Ndiyo Dini ya Kweli?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 9/1 kur. 3-4

Je! Dini Zote Zawaongoza Watu Kwa Mungu?

JE! WEWE ulijua kwamba kuna dini inayoitwa “Wamwabuduo Kennedy”? Waifuatayo wanaamini kwamba marehemu John F. Kennedy aliyekuwa rais wa United States ya Amerika anaweza ‘kuwaponya magonjwa waliozaliwa nayo na hata magonjwa yenye kuua.’

Au namna gani juu ya lile linaloitwa kanisa la Huduma ya Hekima ya Ulimwengu wote? Msingi wake ni imani ya kwamba kuna visahani vyenye kuelea angani, naye mwanzilishi wake hudai kwamba alipata kubebwa katika kimojawapo saa 8 za usiku.

Naye ni nani ambaye hajasikia, na kugutushwa na kujiua kwa wingi sana katika Guyana kwa washiriki zaidi ya 900 wa “People’s Temple” ya “Reverend” Jim Jones?

Mifano ya namna hiyo yaweza kutokeza maulizo mazito juu ya maoni yanayoshikiliwa kila mahali, maoni ambayo huenda ukawa umeyasikia. Mara nyingi maoni hayo yanasemwa hivi, ‘Dini zote ni njia tofauti-tofauti tu za kuwaongoza watu kwa Mungu.’

SABABU MAONI HAYO YANAPENDWA NA WENGI

Sababu moja kwa nini wengi wanaamini katika njia hiyo leo ni kwamba kuna ‘roho ya kujitegemea’ inayozidi kuongezeka. Watu wanakuwa waangalifu sana wasionwe na wengine kuwa wajinga au wenye kushikilia dini sana bila akili.

Sababu nyingine kwa nini wengine wanasema kwamba ‘kuna wema fulani katika dini zote’ ni kwa vile makanisa yaliyo mengi huzungumza juu ya upendo na kufundisha kwamba ni vibaya kuwaumiza wengine, kuua, kusema uongo au kuiba. Makanisa yamejenga mahospitali na shule ili kusaidia walio na uhitaji. Navyo vikundi vya kidini vimefasiri na kueneza Biblia, na hivyo kusaidia watu wengi wajifunze juu ya Mungu wa kweli na Mwanawe, Yesu.

Walakini, ikiwa yuko Mungu wa kweli ambaye ametoa uongozi katika Neno lake lililoandikwa, na Mwanawe aliyefundisha juu ya dini kwa usahihi, twauliza hivi: “Mungu na Yesu wanazionaje dini hizo tofauti-tofauti? Je! wao wanakubali kwamba ‘dini zote zawaongoza watu kwa Mungu’ “?

NA WALE “WENGI” AU NA WALE “WACHACHE”?

Kuzunguka dunia yote Yesu Kristo anaheshimiwa kuwa alikuwa mwalimu mwenye hekima na mwenye kumwogopa Mungu, bila shaka yeye hakuwa mjinga. Hata hivyo, Yesu alisema waziwazi hivi katika Mahubiri yake ya Mlimani yenye kujulikana sana:

“Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya . . . kwa jina lako . . . miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu.”​—Mt. 7;21-23.

Angalia kwamba Yesu hakuchukua maoni yanayopendwa na wengi na yaliyo ya ulimwenguni pote ya kwamba watu wengi wanaofuata dini fulani katika njia yao wenyewe wanampendeza Mungu. Badala yake, Yesu alisema kwamba “wengi” hata miongoni mwa wale wanaodai kumkubali Yesu kuwa Bwana au Kristo hawakubaliki.

Katika mahubiri ayo hayo, Yesu alishauri waziwazi hivi:

“Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.”​—Mt. 7:13, 14.

Unadhani ni kwa sababu gani Yesu alichukua maoni ya namna hiyo? Maandiko yanaonyesha wazi kwamba Yesu alijua kwamba ili kumpendeza Mungu mtu anahitaji ‘kufanya mapenzi ya Baba yake,’ yanayoonyeshwa katika Biblia. Akiunga mkono jambo hilo, Yesu alilaumu kuzoea na kufundisha mambo yanayopingana na Neno la Mungu. Ilifaa kwake kufanya hivyo kwa kuwa yeye alijua kwamba dini ingeweza kutumiwa kuwatega watu na kuwaongoza vibaya. (Mt. 23:13; 2 Kor. 4:4) Yakilinganishwa na Maandiko, mengi yanayofundishwa makanisani leo yanaonekana kuwa yanasingizia njia za ukarimu na upendo za Mungu wa kweli.

Kwa hiyo, inaonekana wazi kwamba haingemtosha ye yote, kutia na sisi wenyewe, kufuatana tu na dini ya wazazi wetu au kufuata tu dini kubwa iliyo karibu yetu. Kwa kuwa hata kama tungefanya hivyo kwa unyofu, hiyo ingetuweka tu kati ya “wengi” ambao Yesu alisema kwamba wako kwenye ‘njia pana inayoongoza kwenye uharibifu.’

Bila shaka wewe ungependelea kuwa kati ya wale “wachache” ambao Mungu huwaona kuwa katika “njia” ambayo kweli kweli inaongoza kwake. Vilevile ndiyo njia ambayo Yesu alisema kwamba inaongoza kwenye “uzima,” uzima wa milele.​—Yohana 3:16; 17:3.

MAARIFA SAHIHI AMBAYO HUONGOZA KWA MUNGU

Bila shaka unaweza kuona kwamba lazima tuwe wataalamu wa elimu ya dini au tuwe na maarifa mengi sana ya kidini ili tuepuke makanisa yenye imani katika miujiza kutoka kwa mwanasiasa marehemu, au kusafiri kwa visahani vyenye kuelea angani, au ile inayoongoza kwenye kujiua kiwazimu. Hata hivyo tunahitaji maarifa—maarifa sahihi.

Tuna ushuhuda ulio wazi wa jambo hili katika habari ya mwanasheria Myahudi wa karne ya kwanza aitwaye Sauli (au Paulo) aliyepata kuwa mtume Mkristo. Yeye alikuwa na juhudi sana katika imani yake ya hapo kwanza, hata akajaribu kufutilia mbali ibada aliyoona kuwa haifai. Hata hivyo kupitia kwa rehema ya Mungu, Paulo alipata kujua kwamba watu wenye kufuata dini sana, kutia na yeye, wanaweza kuwa na “juhudi kwa ajili ya Mungu; walakini si kulingana na maarifa sahihi.” Paulo alipozidi katika maarifa ya mapenzi ya Mungu na anavyowatendea watu wake, akawa mfuasi wa ibada iliyo sahihi zaidi.​—Matendo 8:1-3; 9:1,2; Rum. 10:2, NW; 1 Tim. 1:12-16.

Jambo hilo lapaswa kuongoza namna tunavyofikiri leo, kwa kuwa ni mapenzi ya Mungu kwamba watu wote ‘wapate maarifa sahihi ya kweli’ na kumwabudu kulingana nayo. (1 Tim. 2:3, 4, NW) Mungu alimwongoza Paulo atabiri kwamba katika wakati wetu watu wengi wangekuwa “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake.” Tumeamriwa hivi: “Hao nao ujiepushe nao.”​—2 Tim. 3:1-5.

Basi, tunahitaji sana sana kujua kama sisi tunafuata dini au njia ya ibada ambayo inaongoza kweli kweli kwa Mungu. Lakini tunawezaje kuwa na hakika?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki