Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 10/1 kur. 13-18
  • Ikiwa Mungu Ana Tengenezo, Ni Tengenezo Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ikiwa Mungu Ana Tengenezo, Ni Tengenezo Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YULE “MWANAMKE” ALIYE MBINGUNI
  • Mbegu ya Nyoka—Yafunuliwaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Upatano wa Biblia Yote
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Ufalme wa Mungu Wazaliwa!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 10/1 kur. 13-18

Ikiwa Mungu Ana Tengenezo, Ni Tengenezo Gani?

1. Maoni ya wengine ni nini leo kuelekea usemi “tengenezo la Mungu,” na kwa sababu gani?

KWA kushangaza, katika kizazi hiki chenye akili nyingi, wengi wamekuwa na mashaka juu ya kama Mungu ana tengenezo. Wengine wanasita, ndiyo, sasa wanaogopa kutumia usemi “tengenezo la Mungu,” kwa sababu wameona kwamba tafsiri ya Biblia yao haitumii neno “tengenezo” kuhusiana na Mungu hata kidogo.

2. (a) Kwa sababu ya Warumi 13:1, 2, je! inaweza kuthibitishwa kwamba serikali za Jumuiya ya Wakristo ndizo tengenezo la Mungu linaloonekana? (b) Ni maulizo gani yanayotokea kuhusu Mashahidi wa Yehova ambao wamekuwa na utaratibu wa kutimiza Mathayo 24:14 tangu mwaka 1922?

2 Hakika hakuna mtu mwenye akili atakayekazania kwamba serikali zenye utaratibu sana za leo, hata zile za Jumuiya ya Wakristo, ni tengenezo la Mungu au hata sehemu ya tengenezo lake. Hakuna mtu anayeweza kuthibitisha jambo hilo hata kwa kuendea maneno ya mtume Paulo katika Warumi 13:1, 2: “Hakuna mamlaka, isipokuwa kwa njia ya Mungu, Na ile iliyopo imepangwa na Mungu,​—Hivyo yeye anayejiweka kupingana na mamlaka Anapingana na mpango wa Mungu.” (Rotherham) Wakati uo huo, sana-sana tangu mwaka 1922, Mashahidi wa Yehova wamekuwa wenye utaratibu mzuri ili kutimiza unabii wa Yesu, katika Mathayo 24:14, NW: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” Kwa hiyo jambo hilo linafanya msimamo wao kuhusiana na Mungu, Yehova wa majeshi, uwe gani? Je! wao ni tengenezo lililofanywa na wanadamu tu ambalo Mungu anaweza kutumia, akichagua kufanya hivyo, au wao ni sehemu ya kidunia inayoonekana ya tengenezo la Mungu? Acha mambo ya hakika yaseme!

3, 4. (a) Ujumbe huo ambao umetangazwa na Jumuiya ya Wakristo wakati wa karne zote zilizopita, ukilinganishwa na “injili” ambayo Mashahidi wa Yehova wametangaza tangu mwaka 1914 unakuwaje? (b) Ni kwa njia gani moja tu ambayo kwayo jambo hilo lingeweza kutimizwa chini ya mateso na upinzani, nao Ufunuo 14:6, 7 unaonyesha nini?

3 Mtu mwenye moyo mnyofu na alinganishe namna ya kuhubiri habari njema za Ufalme ambayo imefanywa na taratibu za kidini za Jumuiya ya Wakristo wakati wa karne zote na ile ambayo imefanywa na mashahidi wa Yehova tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya 1918. Si zile zile wala hazifanani. Ile ya Mashahidi wa Yehova ni “injili” au “habari njema” kweli kweli, juu ya ufalme wa kimbinguni wa Mungu uliosimamishwa kwa Mwanawe Yesu Kristo kutawazwa mwishoni mwa Majira ya Mataifa mwaka 1914. (Luka 21:24) Ushuhuda wa ulimwenguni pote ambao umetolewa kuhusu jambo hilo chini ya shambulio la mataifa yote la mateso na upinzani umewezekana tu kwa msaada wa roho ya Mungu yenye kushinda mambo yote. Haukutolewa kwa roho ya wanadamu wala kwa ile ya Shetani Ibilisi. Ulitolewa kwa msaada wa malaika watakatifu wa Mungu, kama inavyoonyeshwa katika Ufunuo 14:6, 7:

4 “Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.”

5. (a) Ni mtengenezaji yupi anayepaswa kuogopwa katika wakati huu wa kufanya uamuzi? (b) Mtengenezaji adui alijidukiza kwenye mkutano gani wa kimbinguni, kulingana na Ayubu, sura za 1 na 2?

5 Kwa hiyo Yeye anayepaswa kuogopwa sasa katika wakati huu wa uamuzi wa mtu binafsi ni Muumba, Mtengenezaji wa Ulimwengu Wote. Katika kitabu cha Ayubu tunaonyeshwa kidogo jamaa yake ya kimbinguni ya wana wa kimalaika. Mtengenezaji wa taratibu ya mambo ya kilimwengu tangu gharika ya siku za Noa, Shetani Ibilisi, wakati mmoja alikuwa mshiriki wa jamaa hiyo. Katika Ayubu 1:6, 7 anafananishwa na mdukizi katika mambo yanayohusu jamaa, maana twasoma hivi hapo: “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za [Yehova], Shetani naye akaenda kati yao. [Yehova] akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu [Yehova], na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.” Katika Ayubu 2:1, 2 jambo kama ilo hilo linaonyeshwa wakati wa mkutano wa baadaye wa wana wa Mungu wa kweli katika mbingu zisizoonekana.

6. (a) Mkutano huo wa “wana wa Mungu” wa kweli, unaosimamiwa na Yehova Mungu, unaonyesha nini? (b) Hao “wana wa Mungu” wa kweli walitiwaje moyo na mfano uliotolewa na Ayubu?

6 Mikusanyiko hiyo miwili ya wana wa Yehova Mungu inaonyesha nini, na ingefaa wale walio washiriki wa kikundi hicho cha kijamaa waitweje? Ni neno au maneno gani yanayofaa yanayokuja akilini? Twamwachia msomaji aseme. Mikutano hiyo ilikuwa ya kawaida, ikisimamiwa kwa kufaa na Mungu. Kuruhusiwa kwa Shetani katika mikutano hiyo hakumaanishi kwamba yeye alikuwa angali anaonwa kuwa mmoja wa “wana wa Mungu” na kwamba angali alikuwa sehemu ya jamaa ya kimbinguni ya Mungu. Jina lake lenyewe, “Shetani,” linaonyesha kwamba si hivyo ilivyokuwa, maana jina hilo linamaanisha “Mpinzani.” Kwa hiyo hakuwa na kusudi zuri kuzunguka uku na huku duniani akiwa roho asiyeonekana na wanadamu. Alikuwa anapinga mtu ye yote aliyejaribu kuwa mkamilifu kwa Mungu wa kweli. Kwa ruhusa ya Mungu, alishambulia mwanamume yule mwenye haki, mwenye kumwogopa Mungu, ambaye jina lake aliitwa Ayubu wa nchi ya Uzi. Walakini kusudi lake bovu la kuletea dharau enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova Mungu mbele ya watu duniani pamoja na malaika mbinguni lilishindwa. Mfano wa uaminifu wa Ayubu ulitia moyo sana jamaa ya kimbinguni ya Yehova ya wana wa kimalaika.

7. Kutokutii kwa Adamu na Hawa kuliwaondoa katika jamaa gani, na ni viumbe wangapi waliotoka katika makao ya roho ili wafanye kazi ya kulinda?

7 Pengine Shetani alidhani kwamba atashinda kama alivyoshinda wakati wa mwanamume wa kwanza duniani, Adamu mwana wa Mungu. Mwishoni-mwishoni mwa siku ya sita ya uumbaji, wakati ambapo hapakuwapo mtu au kiumbe ye yote wa kibinadamu duniani, Mungu alisema hivi: “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu.” Mungu hapo hakuwa anatumia usemi “sisi,” akiwa anajisemea mwenyewe. Yeye alikuwa anazungumza na mtu mwingine ambaye alimtaka ashiriki utendaji wa kuumba. (Mwa. 1:26) Hakuna mtu anayekubali kweli atakayekana kwamba jambo hilo lilitaka ushirikiano wa kimbinguni. Kwa kusikitisha wanadamu wawili wa kwanza, Adamu na Hawa, walikwenda upande wa mtu wa kiroho asiyeonekana mwenye kutumia nyoka mwenye kuonekana, akamfanya amwite Mungu mwongo. Kutokumtii Mungu kukawaondoa katika jamaa ya watoto wa Mungu ya ulimwengu wote, nao wakafukuzwa katika shamba la Edeni. Kisha Mungu “akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima” uliokuwa ndani ya shamba hilo. (Mwa. 3:24) Palikuwako angaa makerubi wawili, nao walikuwa washiriki wa jamaa ya Mungu ya kimbinguni ambao walikuwa wamepewa ruhusa ya kuvaa miili na kujitokeza kwa wanadamu.

8. Basi wakati huo, je! ilikuwa wazi kwamba kuna wengine katika jamaa ya Mungu, na Ayubu 38:6, 7 inaonyesha nini juu ya hilo?

8 Hivyo inakuwa wazi kwamba wakati huo wa mapema wa kuwapo kwa wanadamu tayari kulikuwako wengine katika jamaa ya Mungu ya kimbinguni. Ndiyo sababu, wakati Yehova Mungu alipokuwa akiuliza maulizo kuhusiana na kuweka msingi wa dunia, alisema hivi: “Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?”​—Ayubu 38:6, 7.

9. Ni vyeo vipi vya viumbe wa kimbinguni vinavyotajwa katika Zaburi, katika Isaya 6:2, na katika unabii wa Danieli?

9 Zaburi 80:1 na 99:1 husema kwamba Yehova ‘anaketi juu ya makerubi.’ Masimulizi hayo yaelekea yametolewa kuhusiana na sanduku takatifu la agano lililokuwa katika Patakatifu Zaidi pa hekalu huko Yerusalemu. Juu ya sanduku hilo palikuwako makerubi wawili wa dhahabu mbawa zao zikiwa zimenyoshwa zikiwa zimeelekea za mwingine, na, juu katikati, palitokea mwanga ulioitwa Shekina ambao uliwakilisha kuwapo kwa Yehova Mungu katika hekalu lake. Akionyeshwa njozi ya kimwujiza ya sehemu ya ndani ya hekalu nabii Isaya alimwona Yehova juu ya kiti chake cha enzi akihudumiwa na viumbe wa roho wanaoitwa maserafi. (Isa. sura 6) Licha ya maserafi na makerubi, kuna malaika wengine, kama wale wanaosemwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo. Asiye wa kusahauliwa au kuachwa, ni kiumbe wa kimbinguni anayeitwa jina lake Mikaeli. Anasemekana kuwa ni “mmoja wa hao wakuu wa mbele” na “mkuu wenu,” yaani, watu wa Danieli. (Dan. 10:13, 21; 12:1) Kwa kufaa Yuda 9 anamwita “Mikaeli, malaika mkuu.”

10. Katika njozi inayosimuliwa katika Danieli 7:1-10, sababu gani pawepo utaratibu wakati wa kikao cha Mahakma?

10 Kuhusiana na njozi ya pekee ya ukuu wa kimbinguni, nabii Danieli anasema hivi: “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” (Dan. 7:9, 10) Katika Mahakma hiyo ya kimungu, kulikuwako utaratibu, sana-sana kwa sababu ya Hakimu huyo kutumikiwa na 10,000 x 10,000.

11. Kupatana na hayo yaliyotangulia, Zaburi 103:19-21 inasema nini, naye Yehova anaitwa nani kuanzia 1 Samweli 1:3 na kuendelea?

11 Kupatana na hilo inasemekana hivi katika Zaburi 103:19-21, NW: “Yehova mwenyewe ameimarisha kabisa kiti chake cha enzi kule mbinguni; nao ufalme wake mwenyewe umetawala kila kitu. Mbarikini Yehova, Enyi malaika zake, wenye nguvu nyingi, wenye kufikiliza neno lake, kwa kusikiliza sauti ya neno lake. Mbarikini Yehova, enyi majeshi yake yote, ninyi wahudumu wake, mnaofanya mapenzi yake.” Kwa kufaa kabisa, tangu kuandikwa kwa 1 Samweli 1:3 na kuendelea, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote ameitwa “Yehova wa majeshi.”​—Yak. 5:4, New World Translation.

12. Uhakika wa kwamba kuna wale wenye vyeo, ndiyo, “majeshi” kati ya jamaa ya Mungu ya kimbinguni, unaonyesha kuna jambo gani mbinguni?

12 Basi sasa, kwa msaada wa mitajo hiyo ya Maandiko iliyotangulia, twaambiwa nini na uhakika wa kwamba jamaa ya Mungu ya kimbinguni inatia ndani malaika mkuu wa wote, wana wa kifalme, makerubi, maserafi, malaika, majeshi, wenye vyeo na wenye madaraka hayo wakiwa wanatenda kwa upatano kabisa na kumtii kabisa Mzee wa Siku, Yehova Mungu? Unatuambia kwamba tengenezo la wale wote walio wa jamaa ya Mungu ya kimbinguni linahitajiwa liwepo. Jamaa hiyo ya kimbinguni ni tengenezo la Mungu. Inamaanisha kwamba Mungu ana tengenezo, neno ambalo kwa Kiebrania ni his.ta.druth’ nalo neno la Kigiriki ni or.gan’o.sis.

YULE “MWANAMKE” ALIYE MBINGUNI

13. (a) Adamu na Hawa walipofanya dhambi, jambo hilo lilikuwa na matokeo juu ya tengenezo la Mungu kwa njia gani? (b) Mungu alisema nini kama kwamba kwa nyoka, walakini maneno asiyoweza kufahamu?

13 Adamu na Hawa walipomtenda Mungu dhambi, jambo hilo likawa na matokeo juu ya tengenezo Lake la ulimwengu wote, ambalo walikuwa sehemu yake. Wakawa si washiriki wa jamaa hiyo ambayo yeye ndiye Baba wa kimbinguni Muumba. Walikwenda upande wa kiumbe wa roho asiyeonekana aliyetumia nyoka yule mwenye kusema uongo. Hakika nyoka yule wa halisi hakufahamu yale Mungu aliyokuwa akimaanisha ilipokuwa ni kama anamwambia hivi: “Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.”​—Mwa. 3:14, 15.

14. Sababu gani kutumia kwa halisi maneno ya Mungu yamhusu nyoka hakufai, na lazima awe ni nyoka na mwanamke wa namna gani wanamaanishwa hapo?

14 Tukiyachukua maneno hayo kwa halisi, maneno hayo yangekuwa na maana gani? Kwamba kungekuwako chuki mbaya sana kati ya nyoka huyo wa halisi na mwanamke huyo wa halisi. Vilevile, kwamba uzao wa Hawa ungeendelea kuwa adui wa nyoka huyo; na kwamba nyoka huyo angeendelea kuishi mpaka uzao wa mwanamke utokee. Kisha “uzao” huo ungejeruhiwa kisigino cha halisi na nyoka huyo, nao “uzao” uliojeruhiwa ungemponda nyoka huyo kichwani, yaani, kumwua. Lakini kufanya hivyo kungeletea wanadamu wote faraja kadiri gani au faida kadiri gani? Kwa kweli, maelezo hayo ya halisi si ya akili. Yanatokeza magumu mengi sana ambayo mwanafunzi ye yote wa Biblia mwenye usawa analazimika kukubali kwamba maneno ya Mungu katika Mwanzo 3:14, 15 lazima yawe na maana ya mfano. Kwa hiyo nyoka aliyemwuliza Hawa ulizo hilo lenye kutega lazima awe anafananisha jambo kuu zaidi, na vilevile “mwanamke” anayetajwa katika habari hii lazima awe ni “mwanamke” wa mfano.

15. Sababu gani hatuna lazima ya kukisia nyoka huyo wa mfano ni nani, na akiwa ni yule “nyoka wa zamani” anakuwa mwenye umri wa miaka mingapi wakati huu?

15 Basi, sasa, je! tunalazimika kukisia nyoka huyo wa mfano ni nani? Hapana! Biblia yenyewe inatuambia. Katika Ufunuo 12:9 inasema juu ya nyoka huyo wa siri kuwa ‘joka mkubwa,’ “nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani.” Hapo mwanzo alikuwa nyoka wa mfano, na kufikia mwaka 96 W.K., wapata wakati ambao mtume Yohana aliandika kitabu cha Ufunuo, Shetani Ibilisi akiwa nyoka mfano alikuwa na umri wa miaka zaidi ya 4,100. Sasa, wakati ambapo njozi ya Ufunuo inakaribia kutimizwa, huyo “nyoka wa zamani” ni mwenye umri wa miaka 6,000 hivi, miaka mingi kuliko namna nyoka ye yote amepata kuishi. Yohana 8:44 husema kwamba “yeye ni mwongo, na baba wa [uongo].”

16. (a) Ufunuo, sura 12, unaonyesha pambano kati ya wakuu wawili gani, na hata hivyo ni kitu gani kinachofanikiwa kuzaliwa? (b) Mama wa mfano analazimika kulishwa kiroho wapi na kwa sababu gani?

16 Kwa kuwa “mwanamke” anayetajwa katika Mwanzo 3:15 si Hawa aliyedanganywa na Shetani Ibilisi kupitia kwa nyoka, yeye ni nani? Kwa mara nyingine kitabu cha Ufunuo kinatusaidia tupate ufahamu sahihi. Sura ya 12 inasimulia pambano kati ya Shetani Ibilisi na “mwanamke” ambaye, tangu kichwani mpaka mguuni, amevikwa kwa nuru ya jua, mwezi na nyota (vitu hivyo vikiwa 12). Kuwaza kwa akili kunatuambia kwamba lazima huyo awe ni “mwanamke” wa mfano huko mbinguni, maana hakuna ye yote wa malaika wa kimbinguni anayesemwa kuwa ni wa kike. Yeye ana mimba, na akiwa kama joka mwenye kunyafua, Shetani Ibilisi anangojea ameze mzao atakayezaliwa. Walakini Baba wa kimbinguni wa mzaliwa huyo anaangalia na kumzuia Shetani, hata kwamba mzaliwa wa kiume azaliwapo ‘anyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi,’ ili akiwa huko ‘ayachunge mataifa yote kwa fimbo ya chuma.’ (Ufu. 12:1-5) Uzao huo wa kifalme haukomeshi uadui wa Shetani kumwelekea “mwanamke” huyo wa mfano, maana analazimika kulishwa kiroho chini ya ulinzi wa kimungu kutoka kwa Shetani. Vita yafuata mbinguni.

17. Je! yule “nyoka wa zamani” alipondwa kichwani na matokeo ya vita mbinguni, nayo matokeo hayo yaliwahusuje watu duniani na katika bahari?

17 Mikaeli malaika mkuu ndiye anayeamuru vikosi vya “majeshi ya Yehova.” Akiwa na majeshi hayo ya kimalaika Mikaeli anapigania mtoto wa “mwanamke” huyo aliyezaliwa hivi karibuni na kutawazwa. Shetani, “nyoka wa zamani,” hana budi kupondwa kichwa, naye pamoja na malaika zake wa kishetani wanavurumishwa chini kwenye dunia yetu. Walakini Shetani hapondwi kichwa wakati huo, maana yungali anaishi. Basi, haishangazi kwamba kilio kinasikika kutoka mbinguni, kikisema: “Ole wa nchi na bahari! kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.”​—Ufu. 12:7-12.

18. Ushindi wa Mikaeli na majeshi yake ulihakikishia “ufalme wa Mungu wetu” jambo gani, na kwa sababu hiyo ni nani ambao wangeweza kufurahi?

18 Kwa kuwa Mikaeli malaika mkuu wa wote, na malaika zake wanapata ushindi, naye “mtoto”? wa kifalme hanyang’anywi kiti chake cha enzi cha kimbinguni kando ya Mungu, tangazo la kimbinguni linafaa: “Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu . . . Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu.”

19. “Mwanamke” huyo anayetunza “mtoto” huyo wa kiume anafananisha nani, na sababu gani hivyo?

19 “Mtoto” huyo wa kiume anayetajwa katika Ufunuo 12:5 kwa wazi ni wa mfano. Mambo yote yanayosemwa kuhusiana na jambo hilo yanafunua kwamba anafananisha ufalme wa Mungu wenye Mwana wake Yesu Kristo akiwa na mamlaka ya kuchunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma, kuyavunja-vunja vipande katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni itakayokuwa wakati ujao, wala hafananishi mtu mmoja. (Ufu. 16:14-16) Kama vile “mtoto” huyo asivyokuwa mtu mmoja, ndivyo mama yake, “mwanamke” yule aliye mbinguni, asivyokuwa mtu mmoja. Kwa kuwa “mwanamke” huyo wa mfano alitungwa mimba na Mungu akiwa mume wake, lazima awe anafananisha tengenezo la Mungu la kiroho. Tengenezo hilo ndilo linalotokeza jamii ya ufalme huo wa kimbinguni, si Yesu Kristo aliyetukuzwa peke yake, mwenye cheo cha Mikaeli aliye malaika mkuu wa wote, bali pia “ndugu” zake wa kiroho, ambao vilevile ni “ndugu” wa tengenezo la Mungu la kiroho.​—Ufu 12:10, 11.

20. Ufunuo 12:17 unaonyeshaje iwapo kungali “ndugu” za tengenezo la Mungu la kiroho hapa duniani?

20 Kungali mabaki ya “ndugu” hao wa kiroho juu ya dunia yetu yenye ole. Maana Ufunuo 12:17 unaendelea kusema hivi: “Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu.” Wakiwa sehemu ya uzao wa “mwanamke” wa Mungu, wana tumaini la Ufalme.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki