Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 3/15 kur. 4-7
  • Je! Kusema Katika Lugha Leo—Kunatoka kwa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kusema Katika Lugha Leo—Kunatoka kwa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA SABABU GANI KARAMA HIYO ILITOLEWA?
  • JE! NI SEHEMU YA UKRISTO LEO?
  • “KWA MATUNDA YAO”
  • Je! Zawadi ya Ndimi Ni Sehemu ya Ukristo wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kusema kwa Lugha
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Uwezo wa Kusema kwa Lugha Je, Unatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kusema kwa Lugha?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 3/15 kur. 4-7

Je! Kusema Katika Lugha Leo​—Kunatoka kwa Mungu

“MAANDIKO yanafundisha kwamba ubatizo wa roho, unaoonyeshwa kwa kusema katika lugha, ni wa kanisa la kweli leo,” ndivyo anavyodai mhudumu Mpentekoste Marvin A. Hicks.

“Fundisho la msingi la kusema katika lugha si la kimaandiko na ni kosa,” ndivyo anavyobisha Dakt. W. A. Criswell wa Kanisa la Kwanza la Baptisti la Dallas. Yeye anaongeza hivi: “Ikiwa hiyo ndiyo imani ya Ukristo, basi mimi si Mkristo.”

Kwa sababu ya ubishano huo juu ya zoea la kusema katika lugha huenda ukataka kujua hivi: ‘Maandiko yanasema nini juu ya karama ya kusema katika lugha? Je! ni sehemu ya Ukristo leo?’ Ili kupata majibu, inasaidia kufahamu kwa nini Wakristo wa kwanza walipewa karama ya kusema katika lugha.

KWA SABABU GANI KARAMA HIYO ILITOLEWA?

Kwanza kabisa, mtume Paulo anaeleza katika Waebrania 2:2-4 kwamba karama za kimwujiza, ambazo zingetia karama ya kusema katika lugha, walipewa Wakristo wa karne ya kwanza ili wathibitishe kwamba kibali ya Mungu ilikuwa imehama kutoka kwa mpango wa ibada wa kale wa Wayahudi mpaka kwenye kundi la Kikristo lililokuwa limeanzishwa karibuni. Kuhamishwa kwa kibali ya kimungu kulithibitishwa vizuri na sehemu ya baada ya karne ya kwanza, wakati baadhi ya mitume wa Yesu Kristo walikuwa wangali hai.

Maneno ya Yesu aliyowaambia wanafunzi wake muda mfupi kabla ya kupaa aende mbinguni katika mwaka 33 W.K. yanaonyesha kwamba karama ya kusema katika lugha vilevile ilitumikia kusudi jingine. Yeye alisema hivi: “Mtapokea nguvu wakati roho takatifu itakapofika juu yenu ninyi, nanyi mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Yudea yote na katika Samaria na katika sehemu ya mbali sana ya dunia.” (Matendo 1:8, NW) Kikundi hicho kidogo cha wanafunzi hakikutia watu waliosema lugha za kila sehemu ya dunia. Walakini, ahadi ya Yesu ilitimia, kama siku kumi baadaye, katika sikukuu ya Pentekoste, roho takatifu ilimiminwa juu ya wanafunzi wake karibu 120 waliokuwa wamekusanyika katika chumba cha orofani katika Yerusalemu. Matokeo yalikuwa nini? ‘Walianza kusema kwa lugha nyingine’ na kwa hiyo wangeweza kuanza mara moja kutimiza mgawo wa kutoa ushuhuda.​—Matendo 2:1-4.

Wakati wanafunzi hao walipotoa ushuhuda katika Yerusalemu katika sikukuu ya Pentekoste, Wayahudi na waongofu waliokuwa wametoka sehemu za mbali ili wahudhurie sikukuu hiyo walisikika wakisema hivi: “Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? . . . tunawasikia hawa wakisema katika lugha zetu matendo makuu ya Mungu.” (Matendo 2:8-11) Ni wazi kwamba lugha zinazotajwa hapa zilikuwa lugha zenye kufahamika, haukuwa usemi usiofahamika. Na angalia kwamba karama hiyo ilitumiwa kupatana na kusudi lile ambalo Yesu alisema kwa ajili yalo roho takatifu ingetolewa, yaani, kutoa ushahidi kwa wengine. Kwa kutokeza kulitimiza kusudi hilo kwa maana “siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.”​—Matendo 2:41.

Kisa kingine wakati kumiminwa kwa roho takatifu kulifuatana na karama ya kusema katika lugha kinaripotiwa katika Matendo 10:44-46. Ukisoma masimulizi hayo utaona kwamba wakati roho ya Mungu ilipomiminwa juu ya Mtaifa Kornelio na watu wa nyumba yake, wao, pia, walianza ‘kusema katika lugha.’ Akitoa maelezo juu ya yale aliyokuwa ameona katika pindi hiyo, mtume Petro alisema hivi: ‘Roho takatifu ikawashukia kama ilivyoushukia sisi mwanzo.’ Basi, kulingana na Petro, karama ya kusema katika lugha iliyotolewa katika pindi hiyo ilikuwa karama ile ile iliyopokewa miaka kadha iliyotangulia katika Pentekoste​—uwezo wa kimwujiza wa kusema katika lugha za kigeni. Biblia inaonyesha kwamba karama ya kusema katika lugha aliyopewa Kornelio na watu wa nyumba yake ilimsadikisha Petro na wale waliokuwa pamoja naye kwamba sasa Mungu alikuwa akiwakubali katika kundi Mataifa wasiotahiriwa. Sasa Mungu alikuwa akilitumia kundi la Kikristo.​—Matendo 11:15-18.

‘Walakini ni nini maana ya maneno ya Paulo katika 1 Wakorintho 14:2?’ Huenda wengine wakauliza. ‘Je! Paulo hakusema hivi “Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu bali husema na Mungu”?’

Kwanza kabisa, lazima iangaliwe kwamba Paulo hapa hazungumzi juu ya sala kibinafsi, bali, mahali pake matumizi ya karama ya kusema katika lugha kwenye mkutano wa kundi. (Tazama 1 Wakorintho 14:23.) Zaidi ya hayo, maneno ya Paulo yanapatana kabisa na kusudi lile ambalo karama ya kusema katika lugha ilitolewa na masimulizi ya karama hiyo yanayotolewa katika kitabu cha Matendo. Ukisoma sura yote ya 14 ya 1 Wakorintho utaona kwamba (1) ndimi zinazotajwa zilikuwa lugha zenye kujulikana, wala si usemi usiofahamika, na (2) karama hiyo ilitumiwa, si kwa matumizi ya kibinafsi, bali kwa ajili ya faida ya wasioamini.

Ebu tusome mstari wa 2 wote. Unasema hivi: “Maana yeye anenaye kwa lugha [ndimi, NW], hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake.” Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kuwa ‘ndimi’ (“lugha”), glossa, ndilo neno lile lile linalotumiwa katika Matendo 2:4, 11, ambapo kwa wazi ni kuhusu lugha zilizojulikana. Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kuwa “asikiaye” laweza kumaanisha kusikia jambo fulani pasipo kufahamu yaliyosikiwa. Hayo yanaweza kufahamika vizuri zaidi kwa msaada wa mistari, 13, 16 na 17 ya 1 Wakorintho, sura ya 14, ambapo twasoma hivi: “Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha aombe apewe kufasiri. Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye mahali pa [mtu wa kawaida au, mtu asiyeamini; tazama mistari 22-25.] ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, ikiwa hayajui usemayo? Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi.”

Kwa kusema kwa njia rahisi, yule anayesema katika lugha anasema kwa Mungu mahali pa kusema kwa watu ikiwa watu wale wanaosikiliza hawafahamu anayosema. Paulo alikuwa akifikiria lugha za kigeni ambazo zingeweza kufahamika na wengine, bali si usemi usiofahamika. Walakini ikiwa, kwa kweli, hakuna ye yote kati ya waliopo angeweza kufahamu lugha hiyo na ikiwa hakukuwapo wafasiri, basi yule aliyesema katika lugha angepaswa kuomba aweze kuifasiri na hivyo awajenge wengine, sana-sana wasioamini. Iwapo hapakuwapo mtu wa kufasiri, basi, kama andiko linavyosema, ingekuwa afadhali anyamaze.​—1 Kor. 14:28.

Namna gani leo? Je! karama kama kusema katika lugha hazingekuwa za lazima ili ‘kuonyesha kuwapo kwa roho takatifu’ katika mtu?

JE! NI SEHEMU YA UKRISTO LEO?

Maandiko yanaonyesha kwamba karama za kimwujiza walizopewa Wakristo wa karne ya kwanza zilikuwa za muda tu. “Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma.” (1 Kor. 13:8) Je! Biblia inatoa wonyesho wo wote juu ya wakati ambapo karama hizo zingekoma? Ndiyo, inatoa.

Jisomee mwenyewe visa vinavyoripotiwa wakati karama ya kusema katika lugha ilifuatana na kumiminwa kwa roho takatifu: Matendo 2:1-4, 14; 10:44-48; 19:6. Utaona kwamba katika kila kisa, mmoja au zaidi kati ya mitume wa Yesu Kristo alikuwapo. Kulingana na Matendo 8:18, ‘walipewa roho takatifu kwa kuwekelewa mikono ya mitume.’ Basi ni jambo la akili kwamba baada ya kufa kwa mitume, kupeana karama za roho, kutia karama ya kusema katika lugha, zilikoma. Karama ya kusema katika lugha ilikuwa imetimiza kusudi yayo. Ilikuwa imethibitishwa kabisa kwamba kundi la Kikristo lilikuwa na kibali ya Mungu na lilitegemezwa naye. Zaidi ya hayo, Wakristo walikuwa wameongezeka katika hesabu nao walikuwa wametawanyika katika nchi nyingi, wakipeleka “habari njema” pamoja nao.​—Linganisha Wakolosai 1:23, NW.

‘Lakini ikiwa karama hizi zilikwisha basi ni nini kinachotokeza kusema katika lugha kwa leo?’ huenda wengine wakauliza.

“Tunafahamu pia kwamba tukio la ajabu kama hilo linaweza kutokea chini ya uongozi wa mafumbo/mashetani,” ndivyo ulivyokubali usemi wa umoja wa Shirika la Chemchemi na Chama Cha Evanjeli cha Kanisa la Uingereza. (Maneno yaliyolazwa yameongezwa.)

Je! yaweza kuwa kwamba karama ya kusema katika lugha ya kisasa haitoki kwa Mungu? Inafahamika kwamba huenda ikawa vigumu kwa wale wanaodai kuwa na karama hiyo kukubali jambo hilo. Kati ya watu wazima 5,000,000 wanaodai kuwa wanasema katika lugha, asilimia 33 hata hawaamini Ibilisi ni mtu na kwamba aweza kuongoza wengine. Basi, unawezaje kujua kwa hakika kusema katika lugha kwa kisasa kunatoka katika chanzo gani?

“KWA MATUNDA YAO”

Yesu alitoa ufunguo wa kutambua Wakristo wa kweli alipotangaza hivi: “Kila mti mwema huzaa matunda mazuri (Mt. 7:17) Ndiyo, kungepasa kuwepo matunda, au ushuhuda, kwamba roho takatifu ya Mungu ilikuwa ikiwaunga mkono. Tunapata ufahamu kwa kuchunguza ushuhuda wa Kimaandiko wa mambo hayo kwa msaada wa Uchunguzi wa maoni ya watu uliofanywa chini ya uongozi wa gazeti Christianity Today uliochapishwa katika toleo lake la Februari 22, 1980.

Hata mara moja Maandiko hayaonyeshi ye yote mwenye kukubali au kuzoea dhambi akipewa karama ya kimwujiza. Kundi la Kikristo la karne ya kwanza katika Korintho lilijumuishwa (lilifanyizwa) na watu ambao hapo kwanza walikuwa wenye mwenendo uliopotoka walakini walikuwa wamebadilika baada ya kuwa Wakristo. Sasa hawakuwa wakijiingiza katika maisha yaliyopotoka ya uasherati. (1 Kor. 6:9-11) Na, bado, kulingana na uchunguzi huo asilimia 19 ya wale wanaosema katika lugha leo wanakubali ngono kabla ya ndoa.

Wakristo wa kweli wangeiheshimu Biblia kuwa Neno la Mungu. Yesu Kristo aliyataja Maandiko na kuyaona kuwa neno la Mungu. (Yohana 17:17) Walakini, kulingana na uchunguzi huo, asilimia 44 ya wale wanaosema katika lugha katika siku zetu hawaioni Biblia kuwa mamlaka ya kidini ya maana zaidi yenye kutoa uongozi.

“Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,” akaamuru Yesu. (Mt. 28:19, 20, NW) Na yeye alitabiri kwamba “habari njema” za ufalme wa Mungu zingehubiriwa katika “dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda,” (Mt. 24:14, NW) Wakristo wa kweli wanapaswa kuwa wakitenda jambo hilo. Hata hivyo, kulingana na uchunguzi huo, asilimia 51 ya wale wanaosema katika lugha hawasemi juu ya imani yao angaa mara moja kwa juma, na asilimia 58 hawaliweki liwe jambo la kwanza kuwasaidia wengine wamfuate Kristo.

“Wao si [sehemu ya ulimwengu]” ndivyo alivyosema Yesu kuhusu wafuasi wake. (Yohana 17:16) Walakini mahali pa kutokuwa ‘sehemu ya ulimwengu,’ “katika kujiunga na siasa” watu wanaosema katika lugha “wanajipatanisha kabisa na kawaida ya watu kwa jumla,” ndivyo gazeti Christianity Today linavyoripoti.

“Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi,” ndivyo alivyosema Yesu. (Yohana 13:35) Mtume Yohana aliongeza kusema hivi: “Tupendane sisi kwa sisi; si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake.” (1 Yohana 3:11, 12) Wakristo wa kweli wana upendo wa kweli kati ya wao kwa wao. Wao hawatenganishwi na rangi, taifa au cheo katika ujamii. Hata katika nyakati za vita, wanakataa kuchinja waamini wenzao katika nchi nyingine. Je! hivyo ndivyo ilivyo kwa watu wote kwa jumla? Ndivyo ilivyo kwa wale wanaodai kuwa na karama ya kusema katika lugha?

Basi, ushuhuda unaonyesha nini? Kwa kuwa wale wanaosema katika lugha wakiwa kama kikundi “hawazai matunda” yanayotambulisha Wakristo wa kweli, ni wazi kwamba wale wanaodai kuwa na karama ya kusema katika lugha, haiwezi kuwa wameipokea kutoka chanzo kile kile kama Wakristo wa kwanza.

Maandiko yana maonyo makali yanayoonyesha kuwa chanzo kingine kinahusika. Yesu alitabiri hivi: “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo; na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe.” (Mt. 7:22, 23) Mtume Paulo alionya kwamba wakati ungekuja ambapo ‘kazi kubwa sana’ na ‘ishara za kudanganya’ zingetokea zikiwa ni ‘utendaji wa Shetani.’​—2 The. 2:9, 10, NW.

Basi, unawezaje kuwatambua wafuasi wa kweli wa Kristo ikiwa si kwa karama za kimwujiza za kusema katika lugha? Kwa “matunda,” ushuhuda wa Kimaandiko, tuliouchunguza.

Tunakualika uichunguze Biblia na kisha uilinganishe na mafundisho na mazoea ya Mashahidi wa Yehova. Jionee mwenyewe ikiwa yale unayochunguza yatakusukuma useme hivi juu yao, “Mungu yu kati yenu bila shaka.”​—1 Kor. 14:25.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

“Yaliyonipata Hayakutoka kwa Mungu”

“Andiko katika 1 Wakorintho 14:27, 28 . . . lilinisadikisha kwamba yaliyonipata hayakutoka kwa Mungu. . . . Shauri la Paulo hapo lilikuwa . . . kinyume kabisa cha yale yaliyonipata. Mahali pa kuwa wawili au watatu iwapo tu wengi zaidi, tulikuwa na vikundi vikubwa. Wala hatukuwa na ye yote wa kufasiri, kwa hiyo ni nani aliyekuwa akijengwa?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki